url
stringlengths
18
212
text
stringlengths
608
373k
index
stringlengths
64
64
word_count
int64
100
24.7k
mean_word_length
float64
4.5
15.8
num_sentence
int64
3
547
character_count
int64
502
349k
line_count
int64
1
1
fraction_of_duplicate_lines
float64
0
0
fraction_of_characters_in_duplicate_lines
float64
0
0
symbol_to_word_ratio
float64
0
1
fraction_of_words_without_alpha
float64
0
10
num_of_stop_words
int64
10
2.51k
https://www.cosota.go.tz/pages/introduction
##### Utangulizi Utangulizi Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) ipo chini ya Wizara ya Utamaduni , Sanaa na Michezo na imeanzishwa chini ya Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki na 7 ya Mwaka 1999. COSOTA ilianza rasmi mwaka 2001 ikiwa na majukumu makuu mawili , usimamizi wa Hakimiliki nchini lakini pia ukusanyaji na ugawaji mirabaha. Kufuatia mabadiliko ya Sheria ya fedha ya mwaka 2022 (Finance Act 2022) ilitenganisha majukumu hayo na kuanzisha makampuni binafsi ya kukusanya na kugawa mirabaha nchini (CMO),ambapo kwa sasa Ofisi ya Hakimiliki imebaki kusimamia masuala ya Hakimiliki na kutoa leseni kwa Makampuni yanayohusika na kukusanya na kugawa mirabaha (CMO) pamoja na kusimamia masuala ya uharamia wa kazi za wabunifu
8fd07f15fb1536fa832e5f076f13e2c25e4982e7d13aeea59244f207728d990f
111
5.576577
3
619
1
0
0
0.900901
7.21
18
https://www.cosota.go.tz/pages/function-of-cosota
##### Majukumu ya COSOTA Majukumu ya COSOTA **Functions of Copyright Office Of Tanzania (COSOTA)** As provided for under Section 47 of the Copyright and Neighbouring Rights Act, No.7 of 1999 (CAP 218 RE 2002).the functions of the Society are as follows: - To promote and protect the interests of authors, performers, translators, producers of sound recordings, broadcasters, publishers, and, in particular, to collect and distribute any royalties or other remuneration accorded to them in respect of their rights provided for in this Act. - To maintain registers of works, productions and associations of authors, performers, translators, producers of sound recordings, broadcasters and publishers. - To search for, identify and publicize the rights of owners and give evidence of the ownership of these where there is a dispute or an infringement. - To print, publish, issue or circulate any information, report, periodical, books, pamphlet, leaflet or any other material relating to copyright and rights of performers, producers of recordings and broadcasters. - To advise the Minister on all matters under this Act. __KAZI ZINAZOLINDWA NA SHERIA YA HAKIMILIKI__ - - Vitabu, vitini na maandishi mengine ikiwa ni pamoja na programu za kompyuta; - Mihadhara, hotuba, mahubiri na kazi nyingine zenye uelekeo huo; - Kazi za *drama*na zile za muziki wa*drama;* - Kazi za kimuziki (kwa sauti na ala) zenye kujumuisha au bila kujumuisha Maneno; - Kazi za kikolegrafia na michezo bubu ya kuigiza; - Kazi za upigaji picha za sinema na kazi zingine za vielelezo vya kuona na kusikia; - Kazi za kuchora kwa kutumia rangi, usanifu wa majengo, sanaa ya uchongaji vinyago, sanaa ya uchongaji nakshi, sanaa ya litographia na mapambo; - Kazi za sanaa ya kupiga picha ikiwa ni pamoja na kazi zinazotolewa kwa njia zinazoambatana na upigaji picha; - Kazi za sanaa tumizi, ziwe kazi za mikono au zinazotengenezwa katika viwango vya viwandani; na - Vielelezo, ramani, *plan*, michoro na kazi za mawanda matatu zinazohusiana na jiographia, topographia, usanifu wa majengo au sayansi.
b4dfe0942d97e7f81c31ca33b26081d8d66efea8ed71a2fb59ecbeeb489c50ff
325
5.353846
6
1,740
1
0
0
0.307692
6.15
25
https://www.cosota.go.tz/services/legal-and-disputes-resolution
##### Msaada wa Kisheria na Utatuzi wa Migogoro **Msaada wa Kisheria na Utatuzi wa Migogoro** Pamoja na majukumu mengine Ofisi ya Hakimiliki kupitia Kitengo cha Sheria inahusika na usuluhishi wa Migogoro mbalimbali inayohusu uvunjifu wa hakimiliki inayoletwa na wanachama katika Ofisi ya Hakimiliki (COSOTA). __ Utaratibu wa Kushuhulikia Lalamiko__. 1.Mlalamikaji anatakiwa kumwandikia barua Afisa Mtendaji Mkuu wa COSOTA kuhusu lalamiko lake dhidi ya mtu binafsi au Taasisi ambayo anaona kwa namna moja ama nyingine imevunja haki zake za kiubunifu. 2. Mara baada ya kupokea barua ya lalamiko idara huandaa barua ya wito kwa mlalamikiwa ili aweze kufika katika ofisi za Hakimiliki kujibu malalamiko dhidi yake ama kumpa muda wa siku zisizopungua saba ili aweze kujibia uhalali wa yeye kumiliki na kutumia kazi husuka. 3.Katika utatuzi wa migogoro ya kazi za wabunifu pande zote hukaa meza moja na maafisa wa sheria na wataalamu mbali mbali wa Hakimiliki ili kusuluhuhisha mgogoro huo, 4.COSOTA uhakikisha pande zote mbili zinamaliza tofauti zao kwa njia ya amani, na iwapo mmoja wao hajaridhika na usuluhishi huo anaweza kwenda mahakamani na COSOTA inaweza kwenda kutoa ushahidi wa kitaalamu.
d4899015170b1c25f1265b8a9886209d11bd5cdadf1115654f4373169bfb9127
181
5.59116
6
1,012
1
0
0
0.552486
1.66
27
https://www.cosota.go.tz/news/cosota-kushirikiana-na-nbs-kufanya-utafiti-wa-kuhuisha-taarifa-ya-mwaka-2012-ya-mchango-wa-hakimiliki-katika-pato-la-taifa
##### COSOTA KUSHIRIKIANA NA NBS KUFANYA UTAFITI WA KUHUISHA TAARIFA YA MWAKA 2012 YA MCHANGO WA HAKIMILIKI KATIKA PATO LA TAIFA Ofisi ya Hakimiliki Tanzania - COSOTA yafanya mazungumzo na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kuhusu kushirikiana katika kufanya utafiti wa kuhuisha taarifa ya mwaka 2012 ili kuangalia namna hakimiliki inavyochangia katika pato la taifa. Kikao hicho kimefanyika leo Disemba 05, 2023 baina ya Afisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa Hakimiliki wa COSOTA Bi. Doreen Anthony Sinare na Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt. Albina Chuwa wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Jijini Dodoma pamoja na timu ya wataalamu kutoka COSOTA, NBS na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo. Akizungumza katika kikao hicho Afisa Mtendaji Mkuu wa COSOTA alieleza kuwa Shirika la Miliki Bunifu Duniani kwa kushirikiana na COSOTA na BRELA walifanya utafiti huo nchini Tanzania kwa taarifa ya jinsi Hakimiliki ilivyochangia katika pato la taifa mwaka 2009 - 2010 na ripoti yake ilitoka mwaka 2012. "Tukiangalia ripoti hii ya utafiti ni ya muda mrefu na mambo mengi yamebadilika hivi sasa, nimewasiliana na WIPO kwa ajili ya kushirikiana nao katika kufanya utafiti huu na wameridhia kutoa ushirikiano. Hivyo kwa sasa Lengo ni tuandae timu ya Wataalamu wa Takwimu, Uchumi na Hakimiliki na kuweka mkakati wa namna ya kutimiza Lengo hilo. Utafiti huu pia utapelekea utolewaji wa tuzo kwa wale waliochangia zaidi katika pato la taifa na itajenga uelewa na kutoa picha halisi ya umuhimu wa hakimiliki katika Taifa," alisema Doreen. Kwa upande wa Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt.Albina Chuwa (NBS) alisema Ofisi ya Takwimu itatoa ushirikiano katika kufanikisha utafiti huo na kuwa utafiti huu ni muhimu sana. "Suala la kuandaa mpango wa utekelezaji wa utafiti huu ufanyike Kwa haraka na Maafisa waliopewa jukumu hili mtoe kipaumbele n kujito katika kazi hii ili kuleta tija iliyokusudiwa bila kuchelewa" alisema Dkt.Albina. Naye Mkurugenzi wa Idara ya Uchumi na Takwimu Bw. Daniel Msolwa alipongeza COSOTA kwa jitihada za kufikiria kuhuisha utafiti huo, na kusema kweli kuna umuhimu mkubwa wakufanya utafiti huo sababu kwa sasa kuna changamoto ya taarifa za eneo hilo kukosekana. "Ni vyema kwa sasa tuweke mkakati wa namna ya kufanya hii kazi na kujua kuhusu upatikanaji wa rasilimali za kufanya kazi hii sababu ni kazi kubwa na tunaamini WIPO pamoja na Shirika la Kikanda la Afrika la (ARIPO) watasaidia katika kufanikisha suala hili,"alisema Msolwa. Pamoja na hayo Doreen alishukuru utayari wa NBS na BRELA ambaye ndio Msimamizi Mkuu wa Miliki Bunifu Tanzania (Intellectual Property Office) kushirikiana na COSOTA.
c4d183b990a2c8cb7de1ef6f105d402350bae6c3073a4eac08652c9a44700e65
407
5.371007
14
2,186
1
0
0
0.2457
2.46
62
https://www.cosota.go.tz/news/msigwa-aitaka-cosota-kuongeza-mapato-na-kuandaa-miradi
##### MSIGWA AITAKA COSOTA KUONGEZA MAPATO NA KUANDAA MIRADI Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndg.Gerson Msigwa atoa maelekezo kwa Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) kuongeza vyanzo mapato pamoja na kuanzisha miradi mbalimbali itakayosaidia kuboresha utekelezaji wa majukumu. Mheshimiwa Msigwa ametoa maelekezo hayo Oktoba 31, 2023 katika kikao chake na Menejimenti ya COSOTA alipotembelea Ofisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam. "Katika kipindi cha uongozi wangu ninahitaji sana kuona Wizara na Taasisi zinaonekana na zinasema utekelezaji wa shughuli zake, na kwa upande wa COSOTA mnahitaji kujitangaza zaidi na kutoa elimu masuala haya ya hakimiliki bado jamii haijui vizuri mnakazi kubwa katika kutekeleza hili" alisema Msigwa. Akiendelea kuzungumza Katibu Mkuu huyo alishauri COSOTA kutazama Sheria kama inaruhusu ili kuweza kufikiria suala la kupambana na uharamia utekelezaji wake ufanywe Kampuni binafsi kwa usimamizi wa COSOTA ili kuweza kutekeleza kwa ufanisi jukumu hilo kwa Tanzania nzima na kudhibiti watu wanaofanya shughuli hizo. Naye Afisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa Hakimiliki Bi. Doreen Anthony Sinare alimshukuru Katibu Mkuu huyo na kupokea maelekezo na ushauri ambapo aliahidi kuyafanyia kazi na kutoa mrejesho. Halikadhalika Doreen alieleza kuhusu Tozo ya Hakimiliki kuwa makusanyo yameanza tarehe 01.09.2023 kwa ushirikiano na TRA ambayo vifaa vilivyoingizwa bado ni vichache na aliomba nyongeza ya vifaa vingine ambavyo vinaendana na wakati wasasa kuongezwa ili kusaidia ongezeko la makusanyo na kuboresha mapato ya serikali, wasanii, waandishi na wabunifu mbalimbali katika masuala ya hakimiliki.izara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.
bcbec545f7d404ea11e30f7024c1c84942a751cdd2f7a05119d31a7111d02e3f
237
6.092827
7
1,444
1
0
0
0.421941
1.69
42
https://www.cosota.go.tz/news/waziri-dkt-ndumbaro-asisitiza-wabunifu-kazi-za-sanaa-kujisajili
##### WAZIRI DKT. NDUMBARO ASISITIZA WABUNIFU KAZI ZA SANAA KUJISAJILI Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amewasisitiza wasanii, wandishi wa vitabu na wabunifu kujisajili na kusajili kazi zao katika ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) ili waweze kunufaika na kazi zao pamoja na fursa za mikopo zinazotolewa na taasisi za fedha. Mhe. Ndumbaro amesema hayo tarehe 27, 2024 mjini Songea wakati akifungua mafunzo ya urasimishaji wa kazi za sanaa, uandishi na ugawaji wa vitabu na vifaa vya majaribio vya kusaidia kusoma kwa shule zenye wanafunzi wenye uhitaji maalum. Ametoa rai kwa wadau hao kujirasimisha na kurasimisha kazi zao ili zitambulike rasmi, huku akiwaagiza COSOTA na Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania kuwafikia wadau hao hasa waliopo mikoa ya pembezoni ili waweze kuwa na uelewa na faida ya urasimishaji. "Urasimishaji una faida nyingi ikiwemo usimamizi wa kazi zenu kwa ufanisi, kulindwa na sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki na fursa za biashara zaidi kwa kuwa mtakua mnatambulika, pia mtaweza kuongeza kipato binafsi na Taifa kwa ujumla na kupanua soko la kazi zenu", amesisitiza Mhe. Ndumbaro. Ameongeza kuwa, Sekta ya Utamaduni na Sanaa inaongoza kwa ukuaji kwa asilimia 19, ambapo amesema Ilani ya Chama Cha Mapinduzi inaelekeza sekta hiyo kukua na kuajiri vijana wengi ambapo wizara inaendelea kutekeleza. Kwa upande wake, Mkurugenzi Idara ya Sanaa, Dkt. Emmanuel Ishengoma amesema sekta ya ubunifu ina vipaji vingi ambavyo vinahitaji elimu ya kurasimisha kazi hiyo na wao kama wizara watahakikisha wanaendelea kutoa elimu ya urasimishaji. Awali Afisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa HakiMiliki, Bi. Doreen Sinare amesema mafunzo hayo pia yameambatana na utoaji wa vifaa vya majaribio kwa ajili ya kusaidia wanafunzi wenye uoni hafifu kwa baadhi ya shule za mkoa huo ambavyo vitawasaidia kuandaa rejea na masomo katika kuandaa vitini. Mafunzo hayo yamejikita katika mada mbalimbali ikiwemo umuhimu wa kujisajili BASATA, huduma zinazotolewa na Bodi ya Filamu, Hakimiliki na umuhimu wa usajili wa kazi za sanaa na uandishi pamoja na fursa za mitaji kupitia Mfuko wa Utamaduni na Sanaa.
a31b5d8a834b8a37aaf45fe00425d2ee5360fad7aa03ea9371acbda4f9a61d03
327
5.522936
15
1,806
1
0
0
0.30581
1.22
52
https://www.bmt.go.tz/pages/who-we-are
### Sisi ni nani **Baraza la Michezo la Taifa (BMT)** ni Taasisi ya Serikali iliyoundwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Sheria Na.12 ya Mwaka 1967 na Marekebisho yake Na. 6 ya 1971 na No. 3 ya 2018 ya Baraza la Michezo la Taifa. Baraza la Michezo la Taifa limepewa jukumu la kusimamia michezo yote Tanzania. **“DIRA”** ” *Kuwa na Taifa lenye watu wenye Afya, wakakamavu na ufanisi kwenye michezo kwa maendeleo ya jamii, umoja na taifa**“* **“DHAMIRA”** ” *Kutoa fursa sawa ya ushiriki kwa watu wote katika michezo ili kuongeza ufanisi”* **MAJUKUMU YA BARAZA LA MICHEZO LA TAIFA** - Kuendeleza, kustawisha na kudhibiti aina zote za Michezo kitaifa kwa ushirikiano na vyama au vikundi vya michezo - Kuhimiza na kutoa fursa za ushirikiano miongoni mwa vyama mbalimbali vya Taifa. - Kuidhinisha mashindano ya kitaifa na ya kimataifa katika michezo na matamasha yaliyoandaliwa na vyama vya kitaifa na vyama vingine. - Kupanga kwa kushirikiana na serikali za mitaa kwa ajili ya kutenga maeneo kwa ajili ya michezo. - Kuhamasisha ushiriki wa jamii katika michezo. - Kupanga na kuishauri Wizara yenye dhamana ya Michezo juu sera ya ukuzaji wa michezo nchini.
a5b68578315441611922dcba1987caf1bbeca84b310d2e35a1d32add4956885c
193
5.046632
9
974
1
0
0
0.518135
7.25
32
https://www.bmt.go.tz/pages/roles-of-nsc
### KAZI ZA BMT **MAJUKUMU YA BMT KAMA ILIVYOBAINISHWA NA SHERIA YA BMT Na. 12 ya 1967 NA KAMA ILIVYOBORESHWA NA SHERIA YA 1967 NI: ** - Kuendeleza, kustawisha na kudhibiti aina zote za michezo ya ridhaa kwa kushirikiana na Vyama vya Michezo - Kuhimiza na kutoa fursa na ushirikiano miongoni mwa Vyama vya michezo - Kuidhinisha mashindano ya kitaifa na kimataifa ya michezo na matamasha yanayoandaliwa na Vyama vya michezo. - Kuandaa baada ya kushauriana na Vyama vya michezo vinavyohusika mashindano ya kitaifa na kimataifa nia ikiwa ni kubadilishana uzoefu na kukuza mahusiano ya kirafiki na mataifa mengine. - Kuamsha ari ya kupenda aina zote za michezo kwa ngazi zote. - Kutoa baada ya kushauriana na vyama vya Taifa,Nishani, stashahada,vyeti,vikombe na vivutio vingine kwa ajili ya kuhimiza na kukuza shughuli za michezo - Kudhamini nafasi za masomo kwa ajili ya mafunzo ya walimu wa michezo na waandaaji - Kumshauri Waziri kuhusu mahusiano ya nje katika uwanja wa Michezo. - Kushirikiana na mamlaka za serikali za mitaa ili kuwezesha kuwepo kwa fursa za michezo kwa ngazi zote na kujatahidi kujenga moyo wa uanamichezo na nidhamu kwa wanamichezo wote - Kushauriana na vyama, taasisi au watu wengine kuhusiana na michezo ya ridhaa
a650382a920e753f7a832a91da037ccb8f14f59296bb97fce8242f6dcdb167ce
201
5.149254
6
1,035
1
0
0
0.497512
7.46
35
https://www.bmt.go.tz/pages/sports-management-coordination
### Kusimamia na Kuratibu Michezo **Katika kusimamia na kuratatibu michezo Baraza linatekeleza kazi zifuatazo:- ** i. Kuendeleza, kustawisha na kudhibiti aina zote za michezo ya Ridhaa Kitaifa kwa ushirikiano na Vyama au Vikundi vya Michezo vya Ridhaa ya Hiari kwa kutoa:- a. Mafunzo na watumishi wengine. b. Misaada kwa Vyama au Vikundi vya Kitaifa; c. Viwanja vya Michezo na fursa nyinginezo; d. Vifaa vya michezo na vitu vingine ambavyo ni muhimu kwa ajili ya kuendeleza michezo ii. Kuidhinisha mashindano ya Taifa na ya Kimataifa katika michezo na Tamasha vilivyoandaliwa na Vyama vya Taifa na Vyama vingine. iii. Kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu maswala ya michezo na ufundi iv. Kuandaa baada ya kushauriana na Vyama vya Taifa vinavyohusika, Mashindano na Tamasha vya Kitaifa na Kimataifa kwa nia ya kubadilishana uzoefu na kukuza mahusiano ya Kirafiki na mataifa mengine. v. Kuhimiza na kutoa fursa za Ushirikiano miongoni mwa Vyama mbalimbali vya Taifa; vi. Kusimamia na kuratibu chaguz za Vyama/ Mashirikisho ya Michezo ili kupata viongozi bora. vii. Kuamsha ari ya kupenda aina zote za michezo kwa ngazi zote na; viii. Kutunga Sera ya ukuzaji michezo
fa9345d40114f03e6da98295c22b2406eb1c3c4bee6ec3a7f6064664f2e33979
183
5.344262
11
978
1
0
0
0.546448
1.09
31
https://www.bmt.go.tz/pages/research-documentation-training-and-accreditation-schedule
### UTAFITI, UTUNZAJI WA KUMBUKUMBU, MAFUNZO NA UTOAJI WA VIBALI **Utafiti, Utunzaji Wa Kumbukumbu, Mafunzo Na Vibali** Jedwali hili linaonesha shughuli zifuatazo: - (i) Kuandaa kanuni za michezo kwa ajili ya maendeleo ya michezo; (ii) Kuandaa na Kudhibiti Matumizi ya fedha za mfuko wa Maendeleo ya michezo (iii) Kuhamisha ushiriki wa Umma katika michezo na Kuimarisha ubora wa viwango vya michezo (iv) Kuwatambua wanamichezo wenye vipaji naKuendeleza vipawa vyao kupitia Utekelezaji wa Mfumo rasmi (v) Kudhibiti, Kuratibu utoaji wa huduma katika sayansi ya michezo na huduma ya tiba kwa ajili ya maendeleo ya wachezaji wenye vipawa na timu. (vi) Kuratibu utoaji wa Tuzo kwa wanamichezo (vii) Kuratibu mafunzo na shughuli za kuwajengea uwezo wa kiutendaji wadau wa michezo Na utendaji kazi wa Mashirikisho na Vyama vya Michezo, na (viii) Kuratibu Tafiti mbalimbali za michezo na uhifadhi wa kumbukumbu za masuala ya michezo. **Taarifa za Mipango Na Miradi ** Taarifa za Mashindano ya ‘’Ladies first 2019 & 2022’’ Taarifa za Mashindano ya ‘Tanzanite Women Sports Festival 2021 & 2022 ‘ Taarifa ya Mashindano ya Taifa ‘Taifa Cup 2022’ Taarifa ya Mashindano ya ‘National Sports Award 2022’’
dc0e264185ae4d55f0f3957d5feaeb93ae08a328510c92778e889afc306e6e74
185
5.427027
3
1,004
1
0
0
0.540541
6.49
13
https://www.bmt.go.tz/pages/taratibu-za-usajili
### Kuhusu USAJILI **Utaratibu wa Kusajili Vyama/Mashirikisho, Taasisi za Michezo kwa mujibu wa Kanuni za Usjaili Na. 442 za mwaka 1999 ni kama ifuatavyo** 3.(I) Chama chochote kinachotaka kusajiliwa kitapeleka maombi yake kwa Msajili Msaidizi aliyeko katika Wilaya ambayo ni makao makuu ya chama hicho. Maombi haya yaambatanishwe na: - Muhtasari wa kikao cha wanachama kilichofikia uamuzi wa kuunda chama, - Katiba iliyopitishwa na kikao; - Nakala tatu za Katiba ya chama; - Nakala tatu za kanuni za fedha za chama; - Nakala tatu za kanuni za uendeshaji shughuli za chama; - Orodha ya majina ya uanachama wake na namba ya uanachama kwa msajili ## (II) Baada ya kuwasilishwa maombi, Msajili Msaidizi aliyeoko katika Wilaya atawapatia viongozi wa chama **Fomu Na. BMT 1** na **Fomu Na. BMT 2** wazijaze na kisha kupelekwa kwa Msajili wa Vyama vya Michezo BMT (III) Msajili akishayapokea maombi hayo, atayahakiki na endapo hataona upungufu wowote, atakisajili chama hicho kwa kufanya yafuatayo: **Kuingiza jina la Chama katika daftari la Usajili wa Vyama vya Michezo; na****Kutoa hati ya Usajili.** (IV) Endapo **Msajili **atabaini upungufu kwenye maombi yaliyowasilishwa kwake na Msajili Msaidizi, atawajulisha wahusika upungufu uliopo kwa kutumia * Fomu Na. BMT 3* ili wakafanyie marekebisho. (V) Endapo **Msajili** atakataa kukisajili chama, atatoa taarifa kwa chama husika kwa kutumia **Fomu Na .4 BMT** (VI) Chama cha mchezo wowote hakitaruhusiwa kuendesha shughuli za Michezo bila kusajiliwa. Aidha, chama kilichosajiliwa hakiruhusiwi kuwa na ushirikiano wa kimichezo na chama ambacho hakijasajiliwa. 4(I) Kila katiba ya chama inatakiwa kuonyesha kwa uwazi mambo yafuatayo: **Jina la Chama****Anuani kamili, ikiwa na mate au kijiji, namba ya nyumba au ofisi, namba ya sanduku la Posta na Simu kama ipo na pia Mji, Wilaya na Mkoa.****Idadi na aina ya michezo****Muundo wa chama****Wajibu na kazi za kamati mbalimbali.****wajibu na kazi za viongozi na Wanachama****Kalenda ya :****Mikutano ya kamati ndogondogo;****Mikutano ya kamati ya Utendaji;****Mkutano Mkuu wa uchaguzi.****Taratibu za kushughulikia migogoro na rufaa;** **Sifa za wagombea uongozi zimewekwa bayana kulingana na aina ya mchezo, utaalam, uzoefu, kiwango cha elimu na ngazi ya chama husika kwa mujibu wa sera ya maendeleo ya michezo.**
e493c67506e6fb3c7c4a933503997626724088c0bf44538aa67a32d9a09f8e60
343
5.725948
15
1,964
1
0
0
0.58309
4.37
46
https://www.bmt.go.tz/faqs/where-do-we-go-afatet-wijnnvbhbn-2
### Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara ##### Taratibu namna ya kusajili Chama/Mashirikisho/Taasisi za Michezo? __ A. KUSAJILI KWA KUPITIA MFUMO WA SARS : __SaRS ni mfumo wa kidigitali unaomwezesha mdau/mteja wa michezo kuweza kujisajili online, pamoja na kupata huduma zote zinazohusu usajili kwa kutumia mfumo. Mteja/mdau ataweza kujisajili kwa kutumia mfumo. Taratibu za Kujisajili kwa Kupitia Mfumo wa SaRS:- Mteja/Mdau wa Michezo anatakiwa afanya yafuatayo:- i. Afungue akaunti katika mfumo wa SaRS ili aweze kuingia ndani ya mfumo ii. Aingie ndani ya mfumo na kuweza kuchagua aina ya huduma anayotaka kuifanya. Huduma zilipo ndani ya mfumo huu wa SaRS ni: ** a. Maombi ya Usajili (Application for registration)** ** b. Maombi ya kubadilisha katiba ( Correcting constitution)** ** c. Maombi ya kubadilisha kifungu ( Change ofn Articles)** ** d. Maombi ya kubadilisha Jina ( Change of Name)** **e. Maombi ya kubadilisha anuani ( Change of Address)** **iii.** Kuwa na nakala laini ya viambatanisho muhimu vya Kusajili Vyama/Mashirikisho/ Taasisi za Michezo. Viambatanisho hivyo ni kama ifuatavyo:- ** a. Nakala laini ya Muhtasari wa kikao cha wanachama kilichofikia uamuzi wa kuunda chama na kupitisha katiba. ** ** b. Nakala laini ya Katiba. ** ** c. Nakala laini ya Kanuni za fedha za chama. ** ** d. Nakala laini ya Kanuni za uendeshaji wa shughuli za Chama ** ** e. Orodha ya majina ya wanachama wake na namba za wanachama ** ** f. TIN Namba ** ** g. Cheti cha usajili wa Kampuni BRELA** ** h. Nakala laini ya sahihi za mwenyekiti pamoja na katibu wa chama . ** iv. Nyaraka hizi laini zinatakiwa zipandishwe katika mfumo. Baada ya kukamilisha kupandisha taarifa, mdau/mteja ataweza kutengeneza control number ( namba ya malipo) ili aweze kulipia gharama za usajili au huduma atakayokuwa ameomba. v. Baada ya kukamilisha malipo mteja atatoka nje ya mfumo na kusubiri taratibu za kusajiliwa zikamilike. **B. KUSAJILI KWA KUTUMIA UTARATIBU WA KAWAIDA ** 3.(I) Chama chochote kinachotaka kusajiliwa kitapeleka maombi yake kwa Msajili Msaidizi aliyeko katika Wilaya ambayo ni makao makuu ya chama hicho. Maombi haya yaambatanishwe na: - Muhtasari wa kikao cha wanachama kilichofikia uamuzi wa kuunda chama, - Katiba iliyopitishwa na kikao; - Nakala tatu za Katiba ya chama; - Nakala tatu za kanuni za fedha za chama; - Nakala tatu za kanuni za uendeshaji shughuli za chama; - Orodha ya majina ya uanachama wake na namba ya uanachama kwa msajili (II) Baada ya kuwasilishwa maombi, **Msajili Msaidizi** aliyeoko katika Wilaya atawapatia viongozi wa chama **Fomu Na. BMT 1** na **Fomu Na. BMT 2** wazijaze na kisha kupelekwa kwa **Msajili wa Vyama vya Michezo BMT** (III) **Msajili** akishayapokea maombi hayo, atayahakiki na endapo hataona upungufu wowote, atakisajili chama hicho kwa kufanya yafuatayo: **Kuingiza jina la Chama katika daftari la Usajili wa Vyama vya Michezo; na****Kutoa hati ya Usajili.** (IV) Endapo** Msajili **atabaini upungufu kwenye maombi yaliyowasilishwa kwake na **Msajili Msaidizi,** atawajulisha wahusika upungufu uliopo kwa kutumia * Fomu Na. BMT 3* ili wakafanyie marekebisho. (V) Endapo** Msajili** atakataa kukisajili chama, atatoa taarifa kwa chama husika kwa kutumia **Fomu Na .4 BMT** (VI) Chama cha mchezo wowote hakitaruhusiwa kuendesha shughuli za Michezo bila kusajiliwa. Aidha, chama kilichosajiliwa hakiruhusiwi kuwa na ushirikiano wa kimichezo na chama ambacho hakijasajiliwa. 4(I) Kila katiba ya chama inatakiwa kuonyesha kwa uwazi mambo yafuatayo: **Jina la Chama****Anuani kamili, ikiwa na mate au kijiji, namba ya nyumba au ofisi, namba ya sanduku la Posta na Simu kama ipo na pia Mji, Wilaya na Mkoa.****Idadi na aina ya michezo****Muundo wa chama****Wajibu na kazi za kamati mbalimbali.****wajibu na kazi za viongozi na Wanachama****Kalenda ya :****Mikutano ya kamati ndogondogo;****Mikutano ya kamati ya Utendaji;****Mkutano Mkuu wa uchaguzi.****Taratibu za kushughulikia migogoro na rufaa;** **Sifa za wagombea uongozi zimewekwa bayana kulingana na aina ya mchezo, utaalam, uzoefu, kiwango cha elimu na ngazi ya chama husika kwa mujibu wa sera ya maendeleo ya michezo.**
10ca6df6976c572cf236f24b44fde06c654c7af4bab8d314d3df80538d48a875
630
5.538095
29
3,489
1
0
0
0.31746
6.51
68
https://www.basata.go.tz/pages/mandate
**Mamlaka na Kazi za Baraza la Sanaa la Taifa** Kwa mujibu wa Sheria ya 23 ya 1984, ambayo NAC ilianzishwa, kazi za Baraza ni pamoja na: - i. Kufufua na kukuza maendeleo na utengenezaji wa kazi za kisanii ikiwa ni pamoja na utengenezaji na matumizi ya ala za muziki za asili na asili, nyimbo, ushairi na ngoma za asili kwa nia ya kufufua na kukuza Utamaduni wa Tanzania; - ii. Kufanya utafiti juu ya maendeleo, uzalishaji na uuzaji wa kazi za kisanii; - iii. Kutoa huduma za ushauri na usaidizi wa kiufundi kwa ajili ya maendeleo ya makampuni ya kisanii; - iv. Kupanga na kuratibu shughuli za kisanii; - v. Kuishauri Serikali katika masuala yote yanayohusu ukuzaji na utengenezaji wa kazi za sanaa; - vi. Kutoa na kukuza programu na vifaa vya mafunzo; - vii. Kufanya uzalishaji, uingizaji, usafirishaji na uuzaji wa kazi za kisanii; - viii. Kufanya maonyesho, maonyesho, maonyesho, warsha, semina na mashindano; na - ix. Kuandaa kanuni za usajili wa watu na mashirika yanayojihusisha na sanaa.
540edb88b7dd639bdde6ef37792db6844e3a3f6fca3adaef9b981eb3b9204869
169
4.881657
8
825
1
0
0
0
6.51
26
https://www.basata.go.tz/pages/history
Historia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ni Shirika la umma lililoundwa kwa Sheria ya Bunge Na. 23 ya Mwaka 1984 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 5 ya Mwaka 2019. Historia inaonyesha kuwa, Sheria ya kuunda upya Baraza hili ilifanywa kwa kuunganishwa Sheria ya Baraza la Sanaa la Taifa ya Mwaka 1974 na Baraza la Muziki la Taifa (BAMUTA) ya Mwaka 1974. Baraza liliundwa ili lisimamie maendeleo ya sanaa nchini Kazi za Baraza Kwa mujibu wa Sheria Na. 23 ya mwaka 1984 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 5 ya Mwaka 2019, ambayo kwayo Baraza liliundwa, Majukumu ya Baraza ni pamoja na : Muundo wa Baraza Baraza la Sanaa la Taifa lina wajumbe wa Baraza ambao uteuliwa na Waziri anayehusika na masuala ya Sanaa. Mwenyekiti wa Baraza uteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mwenyekiti pamoja na wajumbe wa Baraza uteuliwa kwa kipindi cha miaka mitatu. Wakati ambapo vipindi vya kuteuliwa kwa wajumbe havina ukomo, uteuzi wa Mwenyekiti wa Baraza ni kwa vipindi viwili tu vinavyofuatana. Kwa kawaida wajumbe wa Baraza uteuliwa kwa msingi wa uwakilishi wa mikoa, asasi, asasi zinazofundisha Sanaa, idara za Serikali na asasi zisizo za Serikali. Baraza linaongozwa na Katibu Mtendaji, ambaye ndiye Afisa mtendaji mkuu. Baraza lina idara Mbili zifuatazo: Licha ya idara hizo Mbili, kuna vitengo vitano ambavyo hufanya kazi moja kwa moja chini ya Katibu Mtendaji. Vitengo hivyo ni ; Sanaa hujumuisha Ambao unaweza kuwa wa kuimba na wa vyombo uliorekodiwa kwa sauti au utunzi wa muziki ulioandikwa, bendi, muziki wa jazi, ala, uliorekodiwa, video, taarabu, kwaya, gwaride,muziki wa asili wa ngoma na unaoambatana na maigizo na thamthiliya. Hujumuisha picha za kuchorwa kwa rangi, uchoraji wa kawaida, michoro ya majalada, vitabu au magazeti, uchoraji wa kwenye vitu vigumu kama metali au mbao, uandishi wa herufi ulionakishiwa, sanaa za vikaragosi kwa kutumia kompyuta na michoro iliyochapishwa. Ramani, michoro ya majengo na vielelezo, sanaa za kuumba na kuchonga, picha mgando za kamera, Kazi za usanifu majengo katika maumbo Sanaa za viwandani ikiwa pamoja na zilizo katika picha au zilizofumwa na urembo, na ubunifu wa mavazi, ususi na useketaji wa nguo. Michezo ya kuigiza ya jukwaani, maigizo bubu, usanifu wa majukwaa, maleba, mapambo, uandishi wa tamthiliya, ngoma na ubunifu wake, sauti na vifaa vya jukwaani, sarakasi za binadamu au za wanyama, michezo ya redio.
19f24b341663a69deeeca3b7f7e99290b9639dae95df2cd95839369d0106ab7e
381
5.288714
17
2,015
1
0
0
0
3.15
56
https://www.basata.go.tz/pages/department
**Idara ya Huduma za Taasisi** Kuwajibika kwa shughuli za kila siku na usimamizi wa Kurugenzi ya Huduma za Biashara. **Vitengo vitano ni;** - Kitengo cha Ukaguzi wa ndani. - Kitengo cha Huduma za Sheria. - Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma. - Kitengo cha Manunuzi. - Kitengo cha TEHAMA na Takwimu. **Majukumu;** - Kuandaa mikakati ya uwekezaji na ushauri juu ya uwekezaji katika masuala ya uwekezaji - Kuendeleza na kudumisha mfumo wa uhasibu na usimamizi wa fedha (Malipo ya akaunti, mapokezi, udhibiti wa mikopo na fedha ndogo ndogo) - Kusimamia mahitaji ya kisheria ikiwa ni pamoja na VAT na malipo ya ndani ya mamlaka yanatimizwa - Kuandaa na kutoa ushauri juu ya mikakati bunifu ili kuhakikisha uendelevu wa kifedha wa Halmashauri - Kufuatilia, kutathmini na kudumisha hesabu za Baraza kwa mujibu wa taratibu za uhasibu zinazokubalika na kanuni za Serikali. - Kuendeleza, kudumisha na kutumia mifumo ya juu na jumuishi ya usimamizi wa fedha - Kutekeleza sera na taratibu za fedha na uhasibu zilizoidhinishwa kama zinavyotolewa na mamlaka husika - Kusimamia utoaji wa fedha kwa wakati kulingana na mipango na bajeti iliyoidhinishwa - Kuratibu masuala yote ya fedha na utayarishaji wa taarifa za fedha - Kushughulikia masuala ya nidhamu na ustawi wa wafanyakazi kwa mujibu wa sheria; - Kushughulikia masuala yote ya itifaki; - Kusambaza taarifa za rasilimali watu kwa wadau wa ndani na nje hasa kuhusu nafasi za kazi, fursa za mafunzo na miradi maalumu. - Kuendeleza, kufanya kazi na kusimamia mfumo wa usimamizi wa rasilimali watu kwa kuzingatia sera, sheria na maagizo ya kitaifa - Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa mpango mkakati wa maendeleo endelevu ya taasisi - Kutoa usimamizi wa rasilimali watu na huduma za usaidizi wa kiutawala; - Kuandaa na kutekeleza sera za rasilimali watu kama vile kuajiri, mafunzo, mishahara, mpango wa huduma, kanuni za wafanyikazi na mipango ya uboreshaji wa masharti na masharti ya utumishi. - Kuratibu utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kupambana na rushwa - Kusimamia, kuratibu na kusimamia shughuli za kupanga, kuendesha magari na tathmini
a9be3ec16a5cba49d94995181f8d2331f48ed98d5ebeb4f09b20db62dae29959
334
5.275449
10
1,762
1
0
0
0
6.89
54
https://www.basata.go.tz/pages/arts-promotion-and-development
**Ukuzaji na Maendeleo ya Sanaa** Kuwajibika kwa shughuli za kila siku na usimamizi wa Kurugenzi ya Ukuzaji na Maendeleo ya Sanaa. Idara inaongozwa na mkuu ambaye ni Mkurugenzi wa Ukuzaji na maendeleo ya Sanaa na kusimamia sehemu nne, ambazo ni; **Sehemu nne;** - Sehemu ya sanaa za Maonesho - Sehemu ya sanaa za Ufundi - Sehemu ya Utafiti na Masoko - Sehemu ya Muziki. **Majukumu** - Kumshauri Katibu Mtendaji kuhusu masuala yanayohusu ukuzaji na maendeleo ya sanaa - Kuandaa mikakati ya kukuza na kuendeleza sanaa - Kuratibu shughuli za muziki, Sanaa za ufundi na Sanaa za maonesho; - Kudhibiti ubora na viwango vya kazi ya sanaa - Kutoa ushauri wa kiufundi kwa wasanii na wadau wa sanaa kuhusu Muziki, Sanaa za Maonyesho, Ufundi na Utafiti na Masoko - Kutambua na kusajili wasanii na wadau wa sanaa - Kutangaza kazi za sanaa kwa wasanii waliosajiliwa, vikundi vya sanaa, vyama vya sanaa, mashirikisho ya sanaa na wadau wa sanaa - Kufanya utafiti, uhifadhi wa kumbukumbu za matukio ya wasanii kwa wasanii binafsi waliosajiliwa, vikundi vya sanaa, vyama vya sanaa, mashirikisho ya sanaa na wadau wa sanaa;
5ada58f5c379c9bf5c376afe1f71474aadac2569c6e270395771cdaa558e0733
184
5.016304
3
923
1
0
0
0
6.52
23
https://www.basata.go.tz/news/naibu-katibu-mkuu-methusela-ntonda-aipongeza-basata
**Naibu katibu Mkuu aipongeza BASATA ** Naibu Katibu mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Methusela Stephen Ntonda ameipongeza Menejimenti ya baraza la sanaa la TAifa na kuwataka waongeze ubunifu katika utekelezzaji wa shughuli za kuenedleza sekta ya sanaa nchiniili kuongeza msukomo kwa wasanii katika kujiongezea kipato. Ameyasema hayo tarehe 10 Agosti, 2024 wakati anaongea na timu ya wakuu wa idara na vitengo baada ya kutembelea ofisini hapo kwa minajili ya kujitambulisha na kutambua majukumu ya kuendeleza zsekta ya sanaa yaliyowasilishwa na Katibu Mtendaji Dkt. Kedmon Mapana katika taarifa ya utekelezaji. Naibu Katibu mkuu ametanabaisha misingi ya utendaji wa kazi iambatane na ubunifu wa majukumu bila kuathiri taratibu huku lengo likiwa kukamilisha kwa mafanikio mikakati yote iliyopangwa katika taasisi kwa kipindi husika cha utekelezaji. “Taasisi lazima iwe na mipango thabiti itakayokupa dira thabiti inayokuonesha umefika wapi na kama kuna mkwamo upo sehemu gani ili iwe arahisi kupata suluhisho, kwahiyo watumishi waongeze ubunifu ili kuweza kupiga hatua mbele zaidi” amesema Bw. Ntonda. Alipogusiwa suala la changamoto ya mmomonyoko wa maadili katika sekta ya sanaa, Bw. Ntonda ameipongeza BASATA kwa kuwa na mwongozo wa uzingatiaji wa maadili katika shughuli za sanaa ambao umesambazwa kwa wadau wake, ila amesisitiza kuwa jambo hili ni mtambuka isiishie hapa washirikishwe na taasisi zingine ili na wao waweze kuwafikia jamii mzima. “Suala la maadili linaendana na tabia ya mtu, watu na jamii kwa ujumla hivyo yapasa kuongeza nguvu katika ushirikishwaji ili kuwafikia taasisi zingine zisaidie kupaza sauti kwa jamii yote” ameongeza Ntonda. Naibu Katibu Mkuu amefanya ziara hiyo ikiwa ni sehemu ya kutembelea na kujitambulisha kwa watumishi wa taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo mara baada ya kuteuliwa kushika nyadhifa hiyo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na kuapishwa Agosti mwaka huu.
8f7afb554c269470f655cff4250688acc388d96a489fa8c280e404b63f47bcb3
297
5.683502
12
1,688
1
0
0
0
1.01
55
https://www.basata.go.tz/news/hawa-hapa-wanaowania-tuzo-za-tma2023
**Hawa hapa wanaowania tuzo za TMA2023** *Isack N. Bilali.* Dirisha la kuwapigia kura wanamuziki watakaowania Tuzo za muziki Tanzania (TMA) limefunguliwa rasmi tarehe 03 Septemba, 2024 saa 5 usiku mara baada ya kamati inayoratibu TMA chini ya uenyekiti wa David Minja na Makamu mwenyekiti Seven Mosha kuweka wazi vipengele vyote vinavyoshindaniwa na wasanii mbalimbali. Kipengele cha mwanamuziki bora wa kiume wa mwaka wanaowania ni Marioo wimbo wa “Shisha”, Diamond “Shuu”, Harmonize “Single again”, Ali Kiba “Sumu” na mwisho ni Jay Melody na wimbo wake wa “Nitasema”. Aidha, Kipengele cha mwanamuxziki bora wa kike wa mwaka wanaowania ni Zuchu “Honey”, Anjela “Blessing”, Malkia Leyla Rashid “wat una viatu” na Nandy “Falling”. Kwa upande wa Bongo fleva mwimbaji bora wa kiume wa mwaka kinashindaniwa na Diamond “Yatapita”, Jay Melody “Sawa”, Alikiba “Mahaba”, Marioo “Love Song” na Harmonize “Single again”. Mwimbaji bora wa kike wa bongo fleva wa mwaka ni Zuchu “Naringa”, Appy “Watu feki”, Nandy “Falling”, Phina “Sisi ni wale” na Anjela “Blessing”. Kwa upande wa wimbo bora wa ushirikiano wa mwaka wanaochuana katika kipengele hiki bni Alikiba ft. Marioo “Sumu”, Mboso ft. Chley “Sele”, Abigail Chams ft. Marioo “Nani”, Jux ft. Diamond “Enjoy” na Diamond ft. Koffi Olomide “Achii”. Katika kipengele cha Albamu bora yam waka walioingia katika mchuano ni Abigail Chams “5”, D Voice “Swahili Kid”, Navy Kenzo “Most People Want this”, Harmonize “Visit Bongo” na Ray Vanny “Flowers III”. Mwanamuziki bora chipukizi wa mwaka wanaoshindania nafasi hiyo ni Pamoja na Xouh “Lalala”, Chino Kid “Gibela”, Appy “Watu feki”, Mocco Genius “Mi Nawe” na Yammi “Namchukia”. Mtifuano wa ngumu kumeza katika wimbo bora wa HipHop wa mwaka unapigwa vikali na wasanii kama Rapcha “Uongo”, Country Wizzy “Current situation”, Young Lunya “Stupid”, Stamina ft Bushoke “Machozi” na Joh Makini “Bobea”. Mwimbaji bora wa Hip Hop ni Young Lunya “Stupid”, Kontawa “Dunga mawe”, Stamina “Machozi”, Joh Makini “Bobea” na Rosa Ree “Mama Omollo”. Huku Mtozi bora wa muziki wa Hip hop wa mwaka wanaowania kipengele hicho ni Black Beatsa “Warrior”, S2Kizzy “Maokoto”, Ommydaddy “Wanangu kibao”, Ringle beatz “Tribulation” na Dupy Beatz “Mr. Christmas part 5”. Kipengele cha Dj bora wa mwaka katika tuzo za TMA kinashindaniwa na Dj D Ommy, Dj Seven Worldwide, Dj Shana Mnyamwezi, Dj Hijab na Dj Mamie. Upande wa utumbuizaji bora wa kike wa mwaka waliotajwa ni Zuchu “Nani remix”, Phina “Do Salale”, Abigail Chams “Milele” na Da Princess “Lolo”. Mtumbuizaji bora wa kiume wa mwaka kipengele hiki kinawaniwa na Mboso “Sele”, Christian Bela “Tamu”, Harmonize “Single again”, Alikiba “Sumu” na Diamond “Shu”. Mtunzi bora wa muziki wa dansi wa mwaka inawaniwa na wanamuziki wafuatao Master Keys, Dad One Touch, Erast o Mashine, na Christian Bela. Juu ya hapo mwandishi bora wa mwaka waliowekwa katika ushindani ni Pamoja na Mbosso, Dulla Makabila, Thabit Abdul, Jay Melody na Marioo. Mtozi bora wa muziki wa bongo fleva wa mwaka wanaoshindanishwa ni Ibrah Jacko, Aloneym, Trone, S2Kizzy, na Mr. L huku wanaowania tuzo ya Mtozi bora wa muziki wa mwaka wakiwemo S2Kizzy, Mr. LG, Laizer, Thabit Abdul na Trone. Mwongozaji bora w avideo wa mwaka ni Hanscana “Maokoto”, Nicklass “Dungamawe”, Ivan “Sele”, Folex “Achii” na Director Wayan “Huku”. Mwanmuziki bora wa mwaka wa nyimbo za asili wanaowania ni Elizabeth Malinganya “Boda boda”, Erica Lulakwa “Aragoba”, Sinaubi Zawose ”Peasa”, Ngapi group “berita” na Wamwiduka band “Usizime Muziki”. Wanaowania wimbo bora wa mwaka wa asili ni Sinaubi Zawose ”Peasa”, Man Fongo na Nyati group “Sauti ya Kumoyo”, Erica Lulakwa “Aragoba”, Wazawa music band “Muziki hauna mwenyewe” na Wamwiduka band “Usizime Muziki”. Mwimbaji bora wa muziki wa dansi wa mwaka ni Christian Bella “Kanivuruga”, Melody Mbassa “Hellena”, Papi Kocha “Jela ya Mapenzi”, Charlz Baba “Mmbeya” na Sarah Masauti “Popo”. Wimbo bora wa dansi wa mwaka wanaowania ni Diamond ft Koffie olomide “Achii”, Melody Mbassa “Nyoka”, Malaika Band “Kanivuruga” na Twanga pepeta “Mmbea”. Kwenye upande wa mwanamuziki bora wa dancehall wa mwaka wanaowania nafasi hiyo ni Pamoja na Dj Davizo “Dance hall”, Badest 47 “Zagamua”, Appy “Mr Hatter”na Bayo the great “Nakupenda”. Upande wa wimbo bora wa Dance hall wa mwaka unashindaniwa na Planner “You”, Dj Davizo “Dance hall”, Badest 47 “Zagamua”, Appy “Mr Hatter”na Bayo the great “Nakupenda”. Sanjari na vipengele vilivyotajwa hapo mwanzo pia kuna kipengele cha mwanamuziki bora wa Reggae wa mwaka ambacho kinawaniwa na Akilimali “Africa Mama”, Dipper rato “Grateful”, Dimateo zion “Rhymes tonight”, Ras Nono “Andika” na Warrior from the East “Wewe”. Wimbo bora wa reggae wa mwaka wanaowania ni Warriors from the East “Wewe”, Akilimali “Africa Mama”, Dimateo zion “Rhymes tonight”, Mr Kamanzi “Give and Thanks” na Paul Mihambo “Salamu zako”. Kwa upande wa taarab vipo vipengele vitatu ambavyo ni Mtunzi bora wanaowania ni Father Mauji “umenibamba”, Bob Rama “Nkurumbi”, Babu Juha “Kisaka”, Thabit Abdul “DSM Sweetheart” na Mfalme Mzee Yusufu “Sina Wema“ Huku, Mwimbaji bora wa mwaka inawaniwa na Salha “DSM Sweetheart”, Mwinyimkuu “Bila yeye sijiwezi”, Malkia Leyla Rashid “Watu na Viatu”, Amina Kidevu “Hatuachani” na Mwansiti Mbwana “Sina wema”. Wimbo bora wa taarab wa mwaka unawaniwa ni Malkia Leyla Rashid “Watu na Viatu”, Salha “DSM Sweetheart”, Mwansiti Mbwana “Sina wema”, Mwinyimkuu “Bila yeye sijiwezi” na Amina Kidevu “Hatuachani”. Tuzo nyingine inaenda katika kipengele cha Mtanzania anayeipeperusha vema bendera ya Tanzania Kimataifa (Tanzania Global Icon Award) wanaowania Tuzo hii ni Pamoja na Mchezaji mpira wa miguu Mbwana Samatta, Mwanamitindo Flaviana Matata, Wanasarakasi Ramadhan Brothers Pamoja na Anisa Mpungwe na Clara Luvanda. Kipengele cha video bora ya muziki yam waka inashindaniwa na Billnass “Maokoto”, Mbosso “Sele”, Zuchu ft Innos B “Nani remix”, Diamond ft Koffie Olomide “Achii” na Harmonize “Single Again”. Turufu ya wimbo bora wa mwaka inachezwa na wasanii wafuatao Zuchu “Honey”, Harmonize “Single Again”, Jux ft Diamond “Enjoy”, Lavalava “Tajiri” na Diamond “Shu”. Kamati hiyo imetaja kipengele cha mwisho kuwa ni “Best song East west and southern Africa” wanaowania ni Libiana “People”, Qing Madi “American Love”, Asake “Lonely at the top”, David ft Musa Keys “Unavailable” na Tyler ICU and Tumelo ft Dj Maphorisa “Mnike”. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa kamati hiyo imeweka wazi kuwa upigaji kura utafikia tamati tarehe 28 Septemba, 2024 hivyo wadau wa sanaa waendelee kuwapigia kura wanamuziki katika vipengele walivyotokea kushindania huku usiku wa tuzo za muziki Tanzania ukitarajiwa kufanyika tarehe 29 Septemba, 2024.
967f0d31b3b11d364e3885ee0ea4422cd8012108fcc51b206d857b3d5e8229f4
1,024
5.529297
36
5,662
1
0
0
0
1.07
106
https://www.basata.go.tz/news/kutana-na-jilema-ng-wana-shija-mtaalam-wa-kuchalaza-zeze
*Isack Bilali, BASATA.* “Mnamo mwaka 1996 akiwa bado mtoto mdogo ndipo alipoanza kugundua kuwa ana mapenzi makubwa ya sanaa ya muziki hususani wa asili mara baada ya kumshuhudia baba yake akiwa analichalaza zeze katika matukio tofauti ya shughuli za kiutamaduni, kilimo na sherehe za kijamii ndani ya Kijiji cha Bukene wilayani Nzega, Mkoani Tabora ama kweli ile methali ya Mtoto wa nyoka ni nyoka imeakisi simulizi hii ya Gwiji wa Zeze” Jilema Ng’wana Shija ni mwanamuziki aliyetimia kutokana na umahiri wake wa kutunga na uandishi wa mashairi yenye kukonga nyoyo za watu, kwa hakika amejaaliwa sana kuwa na uwezo wa kulichalaza zeze kiasi kwamba linamtii na kutoa sauti murua kwa namna anavyoliamuru zinazosindikizwa na mpangilio safi wa sauti zenye kuhamasisha uzalendo na furaha. Utunzi na uwezo wake wa kuchalaza zeze umemuwezesha kumjengea ujasiri mkubwa wa kutoa tungo mbalimbali zilizokonga nyoyo za mashabiki wa muziki wa asili nchini kupitia nyimbo zake kama **vile vijana na ukimwi, chapa ya ng’ombe, Sophia, igembe, selena, mele, niyele **na** wewe mwananchi** ambapo mjumuiko wa nyimbo hizo zinaunda albamu yake aliyoitoa Novemba 4 mwaka 2018. Anakiri kuwa kwa kipindi hicho wakati anatoa albam ya “Jilema Ng’wana Shija“ hakufanikiwa kupata fedha zaidi ya umaarufu hivyo kumuwia vigumu sana kuendelea kumudu gharama ya kutoa albam nyingine ingawa uwezo bado anao, anaweza kufanya hayo yote kama tu akipata menejimenti nzuri yenye kuthamini maendeleo ya muziki wake. Mkusanyiko huu wa nyimbo za asili zenye maudhui ya uhamasishaji katika ufanyaji kazi kwa bidi ni mfumo uliomjenga tangu akiwa mdogo na ameurithi kutoka kwa watamngulizi wake hususani Baba yake mzaizi ambaye alikuwa anamshuhudia akitumbuiza katika nyakati za msimu wa kulima na hata kipindi kile cha mavuno ambapo kwa maeneo ya kijijini kwao walitumia mtindo wa kushindana hivyo kuongeza hamasa kwenye uzalishaji. Ng’wana Shija anaeleza kuwa, mwishoni mwa miaka ya 1980 alitumia muda mwingi kuambatana na Baba yake kila sehemu aliyoenda kutumbuiza kipindi cha msimu wa kilimo ndani ya Mkoa wa Geita, jambo hili lilisababish a kukosa muda wa kujiunga shule na kuhudhuria masomo ya darasani kwa wakati ule akili yake ilimuongoza na kumuaminisha kuwa ujuzi anaoupata ni elimu tosha itakayomsaidia katika Maisha yake hivyo akahamishia jitihada zote kwenye kucheza na zeze. “Nakumbuka nikiwa mdogo kabisa mwanzoni mwa miaka ya 1980 nilikuwa naambatana sana na Baba yangu kila anapoenda kuimba na kwa kule kijijini hayakuwa matamasha makubwa isipokuwa ni yale ya kushindana na kuhamasisha kufanya kazi kwa bidi hususani wakati wa kulima kwa makundi au mavuno maarufu kwa jina la **chapa ya ng’ombe** kutokana na kufurahia hali hiyo sikupata nafasi ya kusoma” amesema Jilema. Kuhama kwa wazazi wake kutoka Mkoa wa Geita kuelekea Wilaya ya Kaliua Mkoani Tabora miaka ya 2000 kulianza kumpa mwanga kwakuwa Baba yake alianza kumuamini na kumuachia asimamie kikundi chao cha muziki wa asili ambapo aliweza kufanya vizuri na kuibuka kidedea hasa kwenye mashindano ya kiutamaduni yaliyoshirikisha makundi mbalimbali ambayo yalihamasisha uzalishaji na uzalendo, umaarufu wake uliongezeka hadi akawa tishio kwa wengine kuogopa kuchuana nae. Maisha yalianza kubadilika pale alipoamua kwa mara ya kwanza kufunga safari kutoka Mkoani Tabora na kuja jijini Dar es salaam ilikuwa mwaka 2007 ambapo alikuja kwa lengo moja tu kuendeleza muziki wa asili ambapo aliamini kanda ya ziwa ameshajitangaza vya kutosha kilichobaki ni kumfikia kila mtanzania na sehemu peke ya kufanikisha mkakati wake ni Dar es salaam. Alipowasili jijini hakuapata changamoto sana kwakuwa alikuta wenyeji alioweza kushirikiana nao wakamuonesha njia na mbinu za upambanaji lakini kikwazo kikubwa kilikuwa ni udhaifu wake wa kutokujua kusoma wala kuandika, Maisha ya mjini yanaweza kuwa rahisi endapo kipaji kitaambatana na kujua kusoma na kuandika kwakuwa vitu havifanyiki kiholela hata kazi inapatikana kwa kusainiana mikataba hivyo ikamlazimu kuanza kujifunza kusoma na kuandika jambo ambalo halikumchukua muda mrefu. Mara nyingi aliweza kupata kazi za kupiga katika maeneo mbalimbali ya starehe zikiwemo hoteli kubwa na kwenye lumbi za burudani hizo kazi zilimsaidia kwa kiasi kikubwa kuweza kuendesha Maisha yake ya hapa mjini hasa kupata mahitaji ya msingi, aliweza kufanya kazi zake kwa miaka 6 akarejea tena kwao Tabora kabla ya kurudi tena Dar es salaam mwaka mmoja baadae yaani 2014. Jilema anaweka wazi kuwa mara baada ya kurejea mjini alianza kuona nyota imeanza kumuwakia kwani kazi zake zilianza kupata kibali cha mialiko ya kwenda kutumbuiza katika baadhi ya nchi za Afrika na Ulaya kwenye matamasha yenye hadhi ya kimataifa kutokana na mjumuiko wa washiriki wake kutoka maeneo mbalimbali Duniani ikiwemo Kenya 2016, Zambia 2017, Uturuki 2016, Denmark 2016, Ujerumani 2017, Norway 2019 zilimuwezesha kutanua wigo wa kufahamika kwa wadau mbalimbali ingawa hakuweza kuendelea kufanya nao kazi kutokana na kukosa menejimenti ya kumsimamia. Pamoja na kipindi kirefu kuwa kimya huku akiendesha shughuli zake kupitia kutumbuiza katika Hoteli mbalimbali lakini sasa ameona umefika muda wa yeye kusimama tena kwakuwa serikali imeshaanza kutilia mkazo sekta ya sanaa hivyo ana matumaini makubwa kuwa kila jambo litaendelea kufanyika kiiutaalama ili kuboresha mnyororo wa thamani utakaomnufaisha kuanzia mzalishaji hadi msikilizaji wa maudhui ya kazi za sanaa. Kutokana na hilo, ameiomba serikali kutilia mkazo mfumo wa elimu ya sanaa uwekwe katika somo kuanzia ngazi ya msingi ili kuwavuta wenye vipaji kama yeye wasikwepe kupata ujuzi huo kwa wakati, hapa, anaamini kwamba hata yeye wakati akiwa mdogo angeweza kuhudhuria masomo yake vizuri tu iwapo kungekuwa na elimu ya sanaa inayototolewa kikamilifu. Sanaa sasa hivi ajira hivyo tunatakiwa kujivunia utamaduni wetu ili uwe kielelezo kwa watu wengine pale endapo sanaa yetu itafanikiwa kuvuka mipaka, ingawa katika hili kuna kasumba inayotawala hata miongoni mwa wasanii wenyewe kuwa matumizi ya ala za asili katika sanaa ni “ushamba” hii inatokana na usasa na kutothamini cha kwako jambo ambalo analipinga vikali Jilema Ng’wana Shija huku akimpa Kongole mwanamuziki mahiri Marioo ambaye alidiriki kumshirikisha kuweka “kionjo” katika wimbo wake wa “Hakuna Matata” ambao unaendelea kukimbiza sokoni. Kwa sasa yupo katika hatua ya kutafuta wadau ambao wataweza kumsimamia kazi zake kulingana na mfumo wa soko la sasa kwakuwa bado ana utajiri mkubwa tungo zenye kusisimua, pia anakaribisha wasanii mbalimbali kushirikiana kwenye kazi kwakuwa utamduni ni kielelezo cha uzalendo, kujirasimisha ni msingi wa kuzikaribia fursa za sanaa zinazochagizwa na sera nzuri serikalini.
073982973abc690abf4b47ebb7355e4f40aa6e63e7b22109425b1ef03f77ca20
995
5.692462
16
5,664
1
0
0
0
1.51
151
https://www.tasuba.ac.tz/historical-background
TAASISI ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa)ni zao la kilichokuwa Chuo cha Sanaa Bagamoyo. Historia ya ya chuo cha Sanaa Bagamoyo ilianzia mnamo mwaka 1962 ambapo kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanganyika iliundwa wizara ya vijana na utamaduni. Mnamo mwaka 1972 ilionekana kuwa kuna uhitaji wa kuwa na mafunzo rasmi ya mambo ya Sanaa, hii ilipelekea kuanzishwa kwa chuo cha sanaa Bagamoyo(BCA). Kati ya mwaka 2003-2005 Chuo cha Sanaa Bagamoyo kilisajiliwa na Baraza la taifa la elimu ya ufundi (NACTE), na kuanzia hapo mitaala ya kufundishia iliandaliwa kikamilifu na kupata ithibati ya NACTE. Mwishoni mwa mwaka 2005 uamuzi ulifanywa na iliyokuwa Wizara ya Elimu na Utamaduni kwamba, Chuo cha Sanaa Bagamoyo kibadilishwe kuwa wakala wa Serikali chini ya mpango wa mabadiliko ya sekta ya umma,kwa hiyo Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo ilianzishwa mnamo tarehe 2 Novemba 2007, kwa tangazo namba 220 lililochapishwa kwenye gazeti la Serikali kwa mujibu wa sheria ya Wakala wa Serikali namba 30 ya mwaka 1997. Taasisi ya sanaa na utamaduni Bagamoyo ni kituo chenye ubora uliotukuka Afrika Mashariki katika kutoa mafunzo ya Sanaa za maonyesho na ufundi ambapo majukumu yake makubwa ni kuhudumia mahitaji ya nchi washirika wa jumuiya ya Afrika Mashariki katika kutunza, kuhamasisha na kuendeleza Sanaa za maonyesho na ufundi. **MAJUKUMU YA TaSUBa** Kutoa mafunzo Kufanya utafiti katika masuala yanayohusu Sanaa na Utamaduni Kutoa ushauri katika masuala yanayohusu Sanaa na Utamaduni Kaole Road **Anuani ya posta: ** P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania **Simu: ** +255 762544613 **Simu ya kiganjani: ** +255 766 264 581 **Barua pepe: ** [email protected] (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) [email protected] (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) [email protected] (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.
17dd14b030f0e04f71322344b0b85960363ef2425a5be3740d5b85655f1c5d78
298
5.634228
8
1,679
1
0
0
0
7.38
44
https://www.tasuba.ac.tz/about-festival
Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni la Bagamoyo hufanyika kila mwaka mwezi Oktoba katika mji mkongwe na wa kihostoria wa Bagamoyo - mji wenye historia adhimu na vivutio lukuki vya urithi wa utamaduni wa Mtanzania vinavyotambuliwa na Shirika la UNESCO. Tamasha hili huandaliwa na kuendeshwa na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa); Taasisi inayotoa mafunzo ya sanaa na utamaduni kwa vijana wenye vipaji. Wakati wote wa Tamasha, maeneo yote ya TaSUBa hupambwa na kazi za sanaa na maonesho mbalimbali ya sanaa. Wasanii mahiri kutoka sehemu mbalimbali za Dunia ambao hufika kuonesha kazi zao za ubunifu wa hali ya juu. Aidha, Tamasha hili huvutia watazamaji, wadau na wapenzi wa sanaa kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje yaTanzania. Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni la Bagamoyo lilianza mwaka 1981 kwa kushirikisha kazi za sanaa za wanafunzi na walimu wa TaSUBa pekee. Hata hivyo limeendelea kukua na kuwa maarufu sana na kuchukua sura ya Kitaifa kiasi cha kuwavutia watazamaji na wasanii wengi kutoka mataifa mbalimbali, hivyo kulifanya liwe la Kimataifa zaidi. Zaidi ya vikundi vya sanaa/ wasanii 1,500 wamepata nafasi ya kushiriki kwenye Tamasha hili tangu lianze; kati ya hawa, vikundi vya sanaa/ wasanii 1,300 wakiwa ni wa ndani na 200 ni kutoka nchi mbalimbali. Tamasha hili pia limekuwa kivutio kikubwa kwa watazamaji vijana kutoka katika shule na vyuo mbalimbali vya hapa nchini. Lengo kuu la Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni la Bagamoyo ni kutoa nafasi kwa wasanii wa ndani ya nchi na wale kutoka nje kukutana na kusherehekea uanuai wa utamaduni unaochagiza mshikamano na bunifu mbalimbali. Malengo mahsusi ya Tamasha ni haya yafuatayo: Mbali na kukusanya wasanii maarufu wa ndani na nje, Tamasha hili hutoa nafasi ya kuonyesha sanaa za ufundi na vifaa vingine vya kiutamaduni, vyakula vya asili, kutembelea vivutio vya kitalii nchini Tanzania, michezo ya watoto na mafunzo mafupi mafupi ya utengenezaji au uandaaji wa sanaa. ** ** Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo huandaliwa na: Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Barabara ya Kaole, S. L. P 32, Bagamoyo, Tanzanaia Barua Pepe: [email protected]/ [email protected] Wavuti: www.tasuba.ac.tz Kuhusu Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni la Bagamoyo.p.pdf Kaole Road **Anuani ya posta: ** P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania **Simu: ** +255 762544613 **Simu ya kiganjani: ** +255 766 264 581 **Barua pepe: ** [email protected] (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) [email protected] (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) [email protected] (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.
8b7d1a887ff84f40b4e36b3b184a74d34bb811c27ba2a9411a13fac1ac86ea9a
423
5.550827
13
2,348
1
0
0
0
4.96
55
https://www.filmboard.go.tz/pages/history-of-tanzania-film-board
#### Historia ya Bodi ya Filamu Tanzania Historia ya sekta ya filamu nchini inaweza kuelezewa kwa vipindi vitatu, yaani kipindi cha wakati wa Ukoloni (1880 – 1961), kipindi cha Uhuru (1961 – 1990) na kipindi cha Soko Huria (1990 hadi sasa). Wakati wa ukoloni, filamu zililetwa kwa ajili ya burudani, kwa dhana ya kuwastaarabisha* *Waafrika na kueneza *propaganda* kuhusu uwezo wa nchi zao katika masuala ya vita, hususani vita vya kutumia ndege. Aidha, mwaka 1930, Serikali ya kikoloni ilitunga Sheria ya Picha za Filamu, Sura ya 230 *(The Cinematograph Ordinance Cap. 230) *ambayo iliweka utaratibu wa nani atazame filamu zipi kati ya Wazungu, Waasia na Waafrika. Sheria hiyo iliunda bodi iliyojulikana kama *Film Licensing and Censorship Board*. Baada ya uhuru, taasisi binafsi zilijitokeza katika utengenezaji, uzalishaji, usambazaji na uoneshaji wa filamu. Aidha, Serikali ilianzisha taasisi na vitengo ambavyo vilitumika kutengeneza filamu zenye maudhui ya kuhamasisha maendeleo, umoja wa kitaifa na matukio mengine ya kiserikali. Taasisi zilizoanzishwa ni pamoja na Kampuni ya Filamu Tanzania (TFC) mwaka 1968 iliyokuwa na jukumu la kupata urari wa kazi za kitanzania, Taasisi ya vielelezo ya Dar es Salaam (AVI) mwaka 1974, Maktaba ya Filamu* *iliyoanzishwa mwaka 1972* *na Bodi ya Filamu iliyoanzishwa mwaka 1976. Pia, katika kipindi hicho, Sheria ya Filamu na Michezo ya Kuigiza Na. 4 ya Mwaka 1976 ilitungwa. Katika kipindi cha soko huria, sehemu kubwa ya uzalishaji, uagizaji na usambazaji wa kazi za filamu ulifanywa na sekta binafsi bila kulazimika kupitia katika kampuni ya filamu Tanzania (TFC). Baadhi ya Kampuni zilizokuwa zinajishughulisha na kazi hizo ni *Pan-African Film Distributors, United Film Distributors na Anglo-American Film Distributors*. Aidha, kuanzia miaka ya 2000, ukuaji wa sayansi na teknolojia umechochea kampuni binafsi za wazawa kupata mwamko wa kuendesha Sekta ya Filamu kibiashara kwa kuzalisha, kusambaza, kuonesha na kufadhili kazi za filamu. Vilevile, kumekuwapo na uanzishwaji wa vyombo vya wadau, vikiwemo Shirikisho la Filamu Tanzania na vyama vinavyounda shirikisho hilo, pamoja na asasi na taasisi binafsi zinazoshughulika na uendelezaji wa Sekta ya Filamu.
857943865def43a044415417fbce598531957709916ced903f2bd4d305cf2c9c
327
5.749235
14
1,880
1
0
0
0.30581
5.5
40
https://www.filmboard.go.tz/pages/objectives
#### Malengo Lengo Kuu Kuwa na sekta ya filamu iliyo madhubuti kwa maendeleo ya wanatasnia na taifa kwa ujumla. Majukumu ya Bodi ya Filamu - Kuishauri serikali kuhusu masuala ya filamu na michezo ya kuigiza nchini - Kusimamia na kuratibu maendeleo ya sekta ya filamu na michezo ya kuigiza - Kupanga madaraja ya viwango kwa wataalam na miundombinu: mfano watayarishaji, waigizaji, wasambazaji, wahariri, watafuta mandhari, waongozaji, wapiga picha, wasambazaji, studio, majumba ya uzalishaji filamu na maeneo ya uoneshaji - Kusimamia na kuratibu utengenezaji wa filamu na michezo ya kuigiza nchini - Kuandaa, kuratibu na kuendesha warsha,vikao, mijadala na mafunzo ya kujenga uwezo kwa wadau - Kuhakiki picha jongevu na michezo ya kuigiza yote, kuipangia madaraja na kuitolea vibali - Kusimamia usambazaji na uoneshaji wa kazi za picha jongevu na michezo ya kuigiza - Kusimamia na kutoa leseni za uendeshaji katika sekta ya filamu pomoja na vitambulisho kwa wadau wa sekta hiyo. Leseni husika zinatolewa kwa majumba ya filamu na michezo ya kuigiza,wasambazaji, maktaba, studio, uanzishaji na uendeshaji wa matamasha na tuzo, utayarishaji wa kazi za picha jongevu - Kusimamia na kuratibu matamasha na tuzo za filamu na michezo ya kuigiza - Kusimamia utendaji wa Shirikisho la Filamu na vyama vya wadau wa sekta ya filamu - Kutafuta fursa katika sekta na kuziwekeza kwa wadau - Kuratibu uibuaji wa vipaji kupitia michezo ya kuigiza na filamu - Majukumu mengine yoyote yanayohusiana na hayo
995581f5051ec2df8792a189b23fd7051b3ac288dbc017418145b66e84a40e7c
232
5.409483
3
1,255
1
0
0
0.431034
6.03
36
https://www.filmboard.go.tz/pages/film-certification-classification
#### Uhakiki na Madaraja ya Filamu Sheria ya Filamu na Michezo ya Kuigiza Na. 4 ya mwaka 1976 na kanuni zake za mwaka 2011 zimeipa bodi hii mamlaka ya kuhakikisha inasimamia maudhui ya picha jongevu nchini Tanzania inayotangaza mila, desturi, urithi wa asili, kutangaza na kudumisha amani na utulivu. Hivyo bodi imekabidhiwa mamlaka ya kuhakiki na kupangia madaraja filamu zote, video za muziki, vipindi vya televisheni, matangazo jongevu ya biashara, michezo ya video, vikaragosi jongevu, michezo ya kuigiza ya jukwaani pamoja na matangazo yake kabla ya kuoneshwa au kusambazwa kwa umma. Aidha, bodi imepewa mamlaka ya kutoa cheti cha uhakiki na alama ya madaraja kwa picha jongevu. *(Bonyeza hapa kupakua fomu)* **Madaraja ya Filamu** Filamu zinazohakikiwa na Bodi ya Filamu hupangiwa madaraja yafuatayo: **Alama ya Uhakiki** Alama ya Uhakiki inayotumika. **Muhimu:** Hakuna picha jongevu au mchezo wa kuigiza utakaosambazwa au kuoneshwa kwa umma bila kuhakikiwa, kupangiwa madaraja, kupewa cheti pamoja na Alama ya Uhakiki. **Taratibu za Uhakiki na Ada zake ** i. Kujaza fomu ya maombi, ii. Kuwasilisha fomu hiyo bodi pamoja na nakala mbili za filamu husika na nakala mbili za matangazo (mabango) yake. Aidha, ataambatisha vibali vya kutumia maeneo, vifaa au maleba maalumu. **Ada** *Muhimu: **Malipo yote yatafanyika kwa kutumia namba ya malipo (control number) inayotolewa na Bodi ya Filamu.*
d20941cedf362e8a177a17385edcd09cf5fd3d561da8136e165c4cfaf502a7c7
212
5.59434
11
1,186
1
0
0
0.471698
2.36
27
https://www.filmboard.go.tz/pages/practicing-licence
#### Leseni za Uendeshaji **Ithibati za u****endeshajiI wa shughuli za filamu** Wahusika ni wote wanaojishughulisha na kazi zozote za filamu na michezo ya kuigiza, matangazo, utayarishaji wa picha jongevu, miundombinu, studio,matamasha na tuzo za filamu. **Hatua za kupata leseni** - Kujaza fomu ya maombi - Kuwasilisha fomu ikiwa na viambatisho vilivyoainishwa - Kupatiwa leseni baada ya maombi kuridhiwa **Leseni, Ada na Vibali** - Kumbi za sinema: TZS. 500,000 kwa mwaka - Maeneo ya uzalishaji kama studios: TZS. 200,000 - Maeneo mengine: TZS. 36,000 Ada hii inalipwa kwa mwaka. Aidha tozo halisi hubainika baada ya uhakiki na ukaguzi wa taarifa za muombaji na/au miundombinu. (Bonyeza hapa kupakua leseni za uendeshaji shughuli za filamu)
060d4dd92a890bfbd8cdf9e65aaf1cb56630fd85f4e21f72ac064f1e8f9e4384
112
5.633929
7
631
1
0
0
0.892857
8.93
13
https://www.filmboard.go.tz/pages/film-location
#### Mandhari Tanzania ni nchi nzuri, ambayo inaweza kupewa daraja la juu katika maeneo ya uandaaji wa filamu ndani ya Afrika. Nchi hii imejaliwa tamaduni mbalimbali za makabila yenye ukarimu kutoka pwani hadi bara na mapori. Mgawanyiko wa hali ya hewa kutoka mkoa mmoja hadi mwingine ni kivutio cha ziada kwa waandaaji wa filamu. Miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza na Arusha inawapa fursa waandaaji kukutana na zaidi ya tamaduni 130 kutoka mataifa mbalimbali yenye kuvutia, kitu ambacho kinafanya miji hiyo kukua kimataifa zaidi, yenye kukaribisha na kuvutia. Mbali na uzuri huo: historia kubwa, fukwe za bahari, miji, vijiji na mapori, endapo utakuja kuandaa filamu ndani ya Tanzania utakuwa karibu sana na kilele cha Afrika. Tanzania ni nchi ya Kilimanjaro, kilele kirefu zaidi Afrika. Aidha, mbuga kubwa zaidi ya wanyama duniani Serengeti, iliyopewa jina na UNESCO kama hazina ya dunia, inahadithiwa kama ni nyumba ya misafara ya nyumbu ya mwisho wa mwaka ambayo ni kitu kinacholeta nakshi katika uandaaji wa filamu. Mbuga ya wanyama ya Serengeti ni maarufu kwa misafara ya nyumbu, kiasi cha milioni sita ya wanyama wakiwa nchi kavu, zaidi ya 200,000 pundamilia na 300,000 ya swala aina ya Thomson wanajumuika kwa pamoja kwa ajili ya kuota jua. Hata kama misafara ikiwa kimya, Serengeti inatoa nafasi nzuri kabisa ya kuandaa filamu Afrika: mikusanyiko mikubwa ya Nyati, makundi mdogo ya Tembo na Twiga, maelfu na maelfu ya ndege, Topi, Kongoni, Impala na Swala na Palahala. Nchi ina mbuga za wanyama kubwa na nzuri kama Selous yenye kuvutia na maeneo mengi ya uandaaji wa filamu ya uhakika. Kituo kilipewa jina la raia wa Uingereza, *Frederick Courtney Selous* ambaye alikuwa ni mwanamazingira, mwindaji, mvumbuzi na mwandishi. Vitabu vyake vya mafunzo kuhusu Afrika vilivyokua na mauzo makubwa ndani ya* Victorian*, Uingereza. Pia kuna kaldera za volkano kama kreta ya Ngorongoro ambacho ni kivutio kikubwa na maarufu duniani chenye mikusanyiko ya wanyama isiyo na uzio. Pia ni kituo kizuri ambacho mtu anaweza akaandaa filamu yake huku akivua samaki na kucheza michezo ya maji Afrika. Wote mnakaribishwa kuja kuandaa filamu katika maeneo mengine tofauti, pengine maeneo mazuri zaidi duniani kama mamia ya maili ya eneo la pwani ya bahari ya Hindi na maziwa yote makuu ya Afrika kama vile : ziwa Victoria, ziwa Tanganyika, na ziwa Nyasa (hakuna inchi yoyote inayokaribia zaidi hata ya moja ya maeneo haya). **Peruzi maeneo ya uandaaji wa filamu katika makundi yafuatayo:** **Hifadhi na Mbuga za Taifa** Mbuga ya wanyama ya Arusha, mbuga ya wanyama ya bonde la Gombe, mbuga ya wanyama ya Katavi, mbuga ya wanyama ya Kilimanjaro, mbuga ya wanyama ya Kitulo, mbuga ya wanyama ya ziwa Manyara, mbuga ya wanyama ya Mikumi, mbuga ya wanyama ya Mkomazi, mbuga ya wanyawa ya Ruaha, mbuga ya wanyama ya kisiwa cha Rubondo na mbuga ya wanyama ya Serengeti. **Utalii anuwai** Utalii anuwai wa ndani ya bonde Gombe, mradi wa utalii ya Kilimanjaro, kituo cha nyoka cha Meserani, utalii wa milima ya Usambara na utalii wa milima ya Udzungwa. **Sehemu za Kihistoria na Mali Kale** Maandishi ya mapangoni ya Kondoa Irangi, mabaki ya Kaole, mabaki ya Isimila, mabaki ya Engaruka, Mikindani, eneo la hifadhi Ngorongoro, mapango ya Amboni, mabaki ya Kidichi *Persian*, hifadhi ya michoro ya mapangoni Kondoa, mapango ya Matumbi, makumbusho ya Mwalimu Nyerere, makumbusho ya Taifa ya Tanzania, makumbusho ya bonde la Olduvai, makumbusho ya Wasukuma, kijiji cha Makumbusho Dar es Salaam, kisiwa cha Changuu (Prison Island), mabaki ya utumwa ya Mangapwani, mabaki ya kasri la Maruhubi, mabaki ya kasri la Mbweni, mabaki ya Mvuleni, Mji mkongwe Zanzibar, nyumba ya maajabu, mabaki ya ngome ya Kiarabu Bagamoyo na Zanzibar na kituo cha kihistoria cha Kalenga. ** Chemchem za Maji Moto** Chemchem ya moto ya Chemka, Chemchem ya moto ya Maji moto Tanga, Chemchem ya moto ya Songwe na Chemchem ya moto ya Kikuletwa. **Maziwa** Ziwa Manyara, ziwa Natron, ziwa Nyasa, ziwa Tanganyika, ziwa Victoria, ziwa Eyasi na ziwa Empakai. ** Misitu** Msitu wa Usambara mashariki, matunzo ya msitu wa Kimboza, eneo la mbao za Miombo ndani ya Tanzania, hifadhii ya msitu wa Mlinga na eneo tengefu la msitu wa Rondo. ** Maporomoko ya maji** Maporomoko ya Rusumo, maporomoko ya Kalambo, maporomoko ya Soni, maporomoko ya Ndoro Marangu, maporomoko ya Sanje Tanzania, maporomoko ya *Gibb’s Farm* Karatu na mengine mengi.
f63d4eb241a2c4e31ff0faafc6060be04dab5e83f0f4424623f6913657d30df4
702
5.246439
22
3,683
1
0
0
0.14245
1.14
80
https://emrejesho.gov.go.tz/maswali_ya_mara_kwa_mara
e-Mrejesho ni mfumo wa kutuma na kupokea malalamiko pamoja na Maulizo kutoka kwa wananchi. Ndio, unaweza kutuma lalamiko lako kwenye taasisi husika. Ili uweze kutuma lalamiko unatakiwa kuwa na simu ya mkononi (smartphone au simu kitochi) / kompyuta / kishikwambi (tablet). Unaweza kutuma lalamiko wakati wowote na mahali popote ila tu unatakiwa kuwa na mtandao mzuri kama unatumia Mobile App au tovuti. Ndio, unachotakiwa kufanya ni kubofya msimbo (*152*00#) kisha utachagua tuma lalamiko. Unachotakiwa kufanya ni kwenda kwenye tovuti ya emalalamiko (https://emalalamiko.gov.go.tz/), bonyeza sehemu iliyoandikwa e-Mrejesho App, pakua, na sanikisha (install) kwenye simu yako. Ndio, unaweza kutumia Mobile App au tovuti kufungua akaunti yako ya eMalalamiko unachotakiwa ni kujaza taaarifa zako kwa usahihi ili uweze kupata mrejesho wa pale unapotuma lalamiko lako. Hapana, huduma hii ni bure kabisa unachotakiwa ni kuwa na namba ya simu kwaajili ya kupata namba na mrejesho wa lalamiko lako. Ndio, unaweza kutuma lalamiko bila kujulikana unachotakiwa ni kuchagua sehemu ya tuma lalamiko bila kujulikana kwenye tovuti au Mobile App. Kuna njia 2 (mbili) za kujua lalamiko lako limepokelewa na kujibiwa au la! a) Kwanza kwa kutumiwa ujumbe mfupi kupitia simu yako ya mkononi endapo ulitumia akaunti yako ya eMalalamiko / ulijaza taarifa zako / Msimbo. b) Pili kwa kutumia Namba (ID) ya lalamiko kupitia tovuti ya eMalalamiko, Mobile App au Msimbo.
e9acf4b65f4f364b750a5581e8c002b8e186f7b4146ae20e2b56befea6b1921b
216
5.685185
12
1,228
1
0
0
0.462963
2.78
33
https://kongoo.bakita.go.tz/?search=advanced
Kiswahili KONGOO YA KISWAHILI YA TAIFA - BAKITA Tafuta Idadi ya utokeaji Jisajili Ingia Kiswahili | Kiingereza | Kifaransa | Kiarabu Advanced Burudani Muziki Uchawi Mapenzi Uganga Michezo Vichekesho Simulizi Sheria Hotuba Magazeti Habarileo Machapisho Chekasana Fasihi Riwaya Shaban Robert Siasa Wizara Ya Maliasili Na Utalii Hansard Shughuli Za Bunge Bajeti Hadithi Uchumi Afya Mabadiliko Ya Tabia Ya Nchi Ripoti Za Kamati Kamati Za Bunge Taarifa Kilimo Sayansi Tehama Wizara Ya Kilimo Na Chakula Mazingira Atomiyme.com Teknolojia LWAGA MWAMBANDE Mato Eric ABDALLAH SEIF DHUNGU afgreenwireless blogspot Alfred Mtewele Ally Mkoreha Amani Mtinangi Anna Testen Anne LaGrange Loving, MS., M(ASCP) Lisa F. Wolf, Ed.D ANNUUR Ansbert Ngurumo Aritamba Malagira Assenga Blogu atomiyme.com Bakari Ubena BAKARI KIANGO Baraza la wawakilishi Zanzibar BBC BBC News BBC Swahili Beatrice Kimaro Bertram B. B Mapunda BLOGGER Bongo5 Bongo5.com Bunge la Tanzania Bunge Polis BUNGE TAARIFA Burhani Yakub capt. Ibrahim Bendera Chachage S. L. Chachage CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA CHARO JOSEPHAT Chuo cha bahari Dar es salaam Chuo Kikuu cha Dar es Salaam CNC DAMAS LUCAS Daniel Samson DAR24 Daudi P. Shayo David Mselewa Dennis C. Rweyemamu Deus kibamba DW DW SWAHILI E. Kezilahabi ECONOMIC AND SOCIAL RESEARCH FOUNDATION (ESRF) Edward Lucas ELIAS MSUYA elimu blog Elizabeth Edward Emmanuel J. shilatu emmanuel mbatilo Emmanuel Mtengwa Ephrahim Bahemu Esau Ng'umbi Eunice Lugiana Evarist Chahali EZEKIEL KAMWAGA facebook Farm Radio Faustine Kapama FB ATTORNEY Flora Nzema Florah Temba FLORIAN KAIJAGE Francisca Swai Freddy Nice Fullhabari TV Gazeti la Raia Mwema Geofrey Nyang’oro George Mwakyembe GEORGE NJOGOPA globalpublishers H. Mwakiyembe habari leo Habel Chidawali Hadija Jumanne Hadija Maloya halmashauri ya jiji la dodoma Halmashauri ya jiji la Mwanza Halmashauri ya wilaya ya Masasi Halmashauri ya wilaya ya Muheza Happiness Tesha Human rights watch ICNL interbuns IOM UN MIGRATION IPP MEDIA Isaack Zake J.K. Nyerere Jacquiline Mrisho JAMES MGAI JAMHURI MEDIA JAMII FORUMS Janet Josiah Janeth Joseph Jeff Msangi Johannes Beck John J. Malata JohnSalim Jones S. Mapunda Joseph Mwendapole Josephat Nyiro Charo jw.org KABOGO GRACE PATRICIA KAKUTE Limited KELVIN MATANDIKO Kennedy Nkya Kizitto Noya Kornelio Maanga Krantz LAWS AFRICA Lubega Emmanuel LYDIA CHURI Magesa Melkory M Magesa Melkory M, Mama WItness M. Marwa Magreth Mwanjalila maishanivita blogspot MAJIRA Mambwana Jumbe MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA Mamlaka ya serikali Mtandao Manispaa ya Kinondoni MARCUS MPANGALA Maria Mtili Martha M. Mvungi Matern Kayera MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA MICHUZI BLOGU Millard Ayo MKUKUTA Mkulima mjasiriamali mogriculture MOHAMED ABDULRAHMAN Mohamed S. Mohamed Msajiri wa vyama vya siasa Msumba blogu Mtanzania Digital mtezamedia Muhammed khamis Muhammed S. Abdulla Muhibu Said MUHIDIN ISSA MICHUZI Muhoyi Dinya MUHUMA MUNIRA HUSSEIN MUSSA BILLEGEYA Mwajuma S. Masaiganah mwana wa makonda blogspot Mwananchi Mwananchi Digital MWANANCHI LIMITED Najjat Omar National AUdit Of Tanzania National bureau of statistics Ndesanjo Macha NEC Neville Meena NIPASHE NJOMBE DC NOOR SHIJA Ofisi ya Makamu wa Rais Ofisi ya Makamu wa raisi ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza Ofisi ya waziri mkuu open university Othman Michuzi Othuman Miraji OUMMIL KHEIR Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S. – Vatican. parentnetworkwny Patricia Kimelemeta Policy Forum Radio Tadio Radio5fm.co.tz Ramadhan Semtawa RASHID ABDALLAH Richard Madete Rose Haji Rose riwa Said A. Mohamed Salim Said SAMMY AWAMI Samwel S. Machang'u Semu Msongole Senkoro F.E.M.K. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar SERIKALI YA ZANZIBAR Shaaban Robert Shafi A. Shafi Shana Matthews Sharon Sauwa Sheria Kiganjani Shivyawata Simon Redslaus Stanley Adika Kevogo SUA Sunday Shomari Suzan Mshakangoto Sylvia Mwehozi TACRI TARI Tawala za mikoa na serikali za mitaa, mkoa wa Njombe Teddy Kilanga Theopista Nsanzungwanko tlsb tovuti kuu ya serikali Tovuti ya afyaleotz.blogspot.com Tovuti ya hazinayetu.blogspot.com Tovuti ya issamichuzi.blogspot.com Tovuti ya Kilimo.go.tz tovuti ya kiongozi tripod tovuti ya miradi na uwezeshaji Tovuti ya mitiki.blogspot.com Tovuti ya Pars Today tovuti ya tanzania online gateway Tovuti ya twaweza.org tovuti ya watchtower online library Tume ya kurekebisha sheria Tanzania Tunzo Mnzava tz-government-gazette U.S. Embassy in Tanzania UCHUMI MALIARDHI Udaku Special UN UN NEWS UNDP UNEP UNFPA UNFPA Tanzania UNIFEM usaid Ustawi wa jamii VATICAN ARCHIVES VATICAN NEWS Veronica Natalis VOA Swahili Walter Nguma Wazohurublog WILDAF TANZANIA Wilhelm Ostberg William Mabusi Wizara ya afya wizara ya ardhi Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali - Zanzibar. Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. wizara ya fedha Wizara ya fedha na mipango Wizara ya Habari ,Sanaa , Michezo na Utamaduni wizara ya habari na mawasiliano Wizara ya Katiba na sheria WIzara ya Kilimo Wizara ya Kilimo, Chakula, na Ushirika Idara ya Uendeshaji Mazao Wizara Ya Madini Wizara ya maendeleo ya jamii WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO Wizara Ya Maji wizara ya maliasili na utalii Wizara Ya Mambo Ya Ndani Wizara ya mambo ya nje WIZARA YA MAZINGIRA Wizara Ya Mifugo Wizara ya nishati wizara ya tamisemi Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi. Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. wizara ya utumishi wa umma wizara ya viwanda na biashara wizara ya viwanda na biashara zanzibar YUSUPH MAZIMU Zainab Deen Zainab Nyamka ZAKARIA MASEKE Zanzibaryetu ZANZINEWS zanzinews.com Zitto Kabwe Zitto Kabwe Ruyagwa Kilimo ni Biashara TWASHEREHEKA UHURU Na Ali Hassan Mwinyi,Tena akaona mbali, uchumi ukafunguliwa Utambuzi wa Anwani za makazi na postikadi katika mtindo wa kidijiti Mkono wa serikali ya Tanzania kuendelea kuwekeza kwa TTCL SABABU GANI ZINAWEZA MFANYA RAIS UHURU KENYATTA KUHUDUMU ZAIDI YA MUHULA WAKE Yaliyojiri mwaka 2014 katika teknolojia ya smartdevices Chadema wamshtaki Makinda Jaji mfawidhi Tabora ataka watumishi wapya kuzingatia weledi, uadilifu, uwajibikaji Utambuzi na udhibiti wa magonjwa ya nyanya Afya ya Mazingira TATIZO LA MWAKA 2000 Maswali 10 muhimu kuhusu “Tanzania na uchumi wa kati” MAENDELEO YA KISWAHILI KATIKA TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO TEHAMA Aliyegundua Pasifiki, na katika mwaka gani_ Anapa likizo na watoto _yote ya umoja_. Anapa hoteli na Resorts kwa familia na watoto Drilling Machine Bosch PBD 40_ maelezo ya jumla, specifikationer, maelezo na maoni ESOL Form B - Swahili Harusi ishara na ushirikina - nini nini_ Historia chronology Kislavoni Hotel Residence Familia na furaha 4 _ (Ugiriki, Rhodes)_ maoni, maelezo na maoni Idadi ya wakazi wa Ufa na historia ya maendeleo ya mji Irina Dacko_ heroine kuu ya mpango wa _Waache kusema_ ngumi mumewe_ Kodi wakazi wa Shirikisho la Urusi - ni ... Je, _kodi wakazi__ Kuanguka kwa Umoja wa Kisovyeti_ ushawishi nje au njama ya ndani_ Kuanguka kwa USSR na malezi ya CIS Kukomesha serfdom_ kwa kifupi kuhusu sababu na matokeo Kwa nini na kwa nini Hitler kuangamiza Wayahudi Limit swichi_ Usalama wa mchakato wowote Madhumuni ya sekta ya viwanda ya Umoja wa Kisovyeti. Miaka ya viwanda, maendeleo yake, matokeo Marais wa Ukraine katika mpangilio. Rais wa kwanza wa Ukraine. Ukraine wa rais mpya Mtangazaji dowels_ Aina, maombi, GOST Mwanasayansi Boyl Robert_ wasifu, shughuli za kisayansi Mwanzo wa vita. nafasi ya Russia Nini ilikuwa matukio kuu ya NEP_ Makala ya sera mpya ya kiuchumi ya Umoja wa Kisovyeti (tazama jedwali) Sahihi upandaji wa pilipili kutoa mavuno ya ukarimu Septemba 11 1991 horoscope na maana ya ishara ya zodiac. - Uchambuzi Wa Siku Ya Kuzaliwa Siri ajali ya vyombo katika bahari Taa mafuta_ Wageni kutumia. Mafuta ya taa taa, _Die Fledermaus_ Ukoloni wa nini_ Mkuu Kigiriki ukoloni Umiliki wa ardhi, mradi katika hali ya huduma_ ili na makala ya umiliki Unga wa nyumbani mashine mwongozo na Unyogovu Mkuu katika Marekani Vifaa vya ujenzi na Majengo, Viwango vya Majumba Vita Miaka Saba _1756-1763_ sababu za na matokeo Vita vya siku sita Viwanda dryer - sehemu ya umeme Wasifu Marco Polo hadithi ya mtu ya ajabu Wasifu wa Marie-Antoinette - Malkia wa Ufaransa TCRA inavyoibeba ‘Tanzania ya kidijitali’ Wataalamu wa Tehama watakiwa kujisajili ZANZIBAR NA UMOJA WA KIISLAMU Afrika Kusini yaidhinisha bima ya afya 12 Agosti 2011 Afya ya Mubarak si nzuri 11 Juni 2012 Bima ya afya kwa raia Marekani 28 Juni 2012 Meli yatoa huduma za afya Tanzania 9 Novemba 2011 Mgomo wa madaktari Tanzania wamalizika 9 Februari 2012 Mkenya atuzwa kwa kutetea mazingira 16 Aprili 2012 Serikali ya Tanzania yatoa ufafanuzi 28 Machi 2011 Muhogo tegemeo kwa mabadiliko ya tabia nchi 28 Februari 2012 Olimpiki ilizingatia mazingira 11 Agosti, 2012 - Saa 1426 GMT MAHAKAMA YA HAKI YA AFRIKA MASHARIKI YAITAKA SERIKALI YA TANZANIA KUREKEBISHA SHERIA YA VYAMA VYA SIASA MATOKEO YA UCHAGUZI KENYA MAHAKAMA YAULIZA MASWALI MAGUMU BUNGE LAPITISHA MUSWADA WA MAREKEBISHO YA SHERIA MBALIMBALI ZA FEDHA WA MWAKA 2022 RAIS SAMIA TAMAA ZA 2025 ZINAONDOKA FURSA NA VIKWAZO KATIKA MARIDHIANO YA KISIASA TANZANIA FREEMAN MBOYE BINGWA WA MIKAKATI YA SIASA ZA UPINZANI TANZANIA. Tanzania yaungana na jirani zake kuunda soko la pamoja la Afrika Mashariki MKUTANO WA RAIS SAMIA NA LISSU ULIVYOPOKELEWA KWANINI CCM IMEBADILI MSIMAMO JUU YA KATIBA MPYA Kampuni ya mifumo ya BAE yakiri makosa Wana Nyerere na Amin kukutana Butiama Samia Suluhu pendeni Sayansi Ni kwasababu gani baadhi ya nchi za Afrika hazitaki msaada wa nguo 27 Julai 2018 Sababu kuu zilizoifanya Tanzania kufikia uchumi wa kipato cha kati Tanzania yaitaka Mwananchi kuomba radhi kwa taarifa kuhusu deni la taifa 19 Mei 2018 Uchumi wa Tanzania unaimarika kwa kiasi gani? UCHUNGUZI HALI YA UCHUMI DUNIANI MPOROMOKO WA DEMOKRASIA AFRIKA WAPONZA UCHUMI DOLA YA MAREKANI YADIDIMIA KUNDI LA DOLA NANE TAJIRI DUNIANI BARAZA LA MAHAKAMA NCHINI LIBYA MFUMO WA KUSIMAMIA UMASIKINI Uzalishaji mazao ya chakula waongezeka 2012 Teknolojia kuwasaidia marefarii Brazil Mabadiliko ya tabianchi yaeneza magonjwa 2 Septemba 2013 Je wapinzani Tanzania wamejipanga kutatua changamoto zinazowakabili Jitihada za serikali kusaidia ugunduzi katika Tehama Jumanne, Machi 26, 2013 Teknolojia Yaiangusha Kenya katika Uchaguzi 7 Machi 2013 Katika teknolojia wiki hii Takwimu rasmi za serikali Tanzania itakuwa sawa na Ulaya ndani ya miaka sita Rais Samia asema Uchumi wa Tanzania umestahimili vipi athari za corona? Ufundi Chuma Asilia Afrika Mashariki KUPUNGUA KWA NGUVU ZA KIUME,HM Hospital - Bunju B Kwa nini afya siyo kipaumbele katika bajeti ya taifa 201112 .policyforum.or. Matokeo ya Uta? ti wa Viashiria vya VVUUKIMWI na Malaria Tanzania 2011-2012 Mpango wa afya ya jamii ya Safidy ripoti ya mwaka wa 5 Mtu 1 kati ya 4 atahitaji huduma ya afya ya akili duniani SAUTIZETU HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE,Septemba 2012, toleo la. 4 TANGAZO LA KAZI LA AFYA 2011 KILIMO BORA CHA MIHOGO _Makazi ya kijeshi_ Arakcheev_ mageuzi ya faida na hasara Kitabu Bila Haki Bilal UTANGULIZI Madhehebu Ithnaa Sayansi na Teknolojia _ kitoto TUME YA TAIFA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA YATOA TUZO LEO. - MTAA KWA MTAA BLOG Tehama Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Kimeanzishwa mwaka 2012 Ripoti ya Uchunguzi wa Madini yamfikia Rais Magufuli 2017 Uchumi wa Nchi Uko Imara MGOGORO WA KIFEDHA Kwa mujibu wa ripoti ya Global Peace Index Tanzania yaongoza kwa amani Afrika Mashariki, yashika nafsi hii kusini mwa Jangwa la Sa Vijana waaswa kushiriki mashindano ya teknolojia TAARIFA YA KAMATI KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA FEDHA WA MWAKA 2016 BUNGE LA TANZANIA KAMATI YA BAJETI TAARIFA YA KAMATI YA BAJETI JUU YA MAPENDEKEZO YA MPANGO WA TAIFA UNAOKUSUDIWA KUTEKELEZWA NA S Mpango wa Taifa Maadili na Madaraka ya Bunge Taarifa ya Kamati Ardhi, Maliasili na Utalii Huduma na Maendeleo ya Jamii Taarifa ya Kamati kuhusu uchunguzi wa tuhuma zinazowahusu Ndg. Paul Christian Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na Ndg. Alexa Mambo ya Nje Nishati na Madini Sheria ndogo Taarifa ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shauri la Mhe. Ester Amos Bulaya Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge - Shauri la Mh. Mbowe na Halima Mdee Bajeti Kilimo, Mifugo na Maji LAAC Masuala ya Ukimwi Miundombinu VBM Taarifa ya Mwaka ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii 2016-2017 Kilimo, Mifugo na Maji PAC MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nane 17 Aprili 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Saba – Tarehe 14 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Sita – Tarehe 13 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nne – Tarehe 11 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tatu – Tarehe 6 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Pili – Tarehe 5 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tano – Tarehe 12 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha kumi- Tarehe 19 Aprili 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha tisa - Tarehe 18 Aprili 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Moja – Tarehe 20 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Sita – Tarehe 2 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Saba – Tarehe 8 Februari 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Nne – Tarehe 27 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Nne – Tarehe 3 Februari, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao chs Sita- Tarehe 7 Februari 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na tatu- Tarehe 25 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nne- Tarehe 3 Februari 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nane- Tarehe 9 Februari 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha kumi na tano- Tarehe 28 Aprili 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tano- Tarehe 6 Februari 2023 MKUTANO WA TISA Kikao cha Tatu Tarehe 3 Novemba, 2022 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tatu – Tarehe 2 Februari, 2023 Mkutano wa ishirini Kikao cha Ishirini na Nne - Tarehe 5 Julai, 2010 Mkutano w Ishirini Kikao cha Ishirini na Nane - Tarehe 12 Julai, 2010 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tano Tarehe 5 Februari, 2018 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Tatu mwaka 2011 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Moja Tarehe 17 Aprili, 2018 HALI YA KILIMO HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO NA USHIRIKA MHESHIMIWA PAUL P. KIMITI (MBUNGE) WAKATI AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FE TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU MALALAMIKO YALIYOFIKISHWA KWENYE KAMATI DHIDI YA WAHESHIMIWA WABUNG TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU UCHUNGUZI WA VITENDO VYA BAADHI YA WABUNGE KUFANYA VURUGU BUNGENI N TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA (PIC) KWA KIPINDI CHA KUA MAONI NA MAPENDEKEZO KUHUSU TAARIFA YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KATIKA SERIKALI ZA MITAA KWA MWAKA WA FEDHA MAONI YA KAMATI KUHUSU AZIMIO LA BUNGE LA KUBADILISHA HADHI MAPORI YA AKIBA YA BIHARAMULO BURIGI, KIMISI, IBANDA NA RUMANYIKA - OR HOTUBA YA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU AZIMIO LA KURIDHIA UBADILISHAJI HADHI MAPORI YA AKIBA YA BIHARAMULO, BURIGI, KIMI TAARIFA YA SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JANUARI 2018 HADI JAN TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO KUHUSU SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JANUARI, 2018 HADI JA TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO KUHUSU SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JANUARI, 2018 HADI JA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA KWA KIPINDI CHA JANUARI, 2018 HADI JAN TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA KAMATI KWA MWAKA 2018/2019 TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JANUARI, 2018 HADI JANUAR TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA KWA KIPINDI CHA FEBRUARI 2018, HADI J TAARIFA YA MWAKA KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA KAMATI YA BUNGE YA BAJETI KATIKA KIPINDI CHA MWEZI JANUARI, 2019 HADI MWEZI JAN TAARIFA YA MWAKA KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA KAMATI YA BUNGE YA BAJETI KATIKA KIPINDI CHA MWEZI JANUARI, 2019 HADI MWEZI JAN TAARIFA YA MWAKA KUHUSU SHUGHULI ZA KAMATI KWA KIPINDI CHA FEBRUARI 2019 HADI JANUARI 2020 TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA KWA KIPINDI CHA KUANZI TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA KAMATI KWA KIPINDI CHA FEBRUARI, 2019 HADI JANUARI, 2020 TAARIFA YA SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI KWA KIPINDI CHA KUANZIA JANUARI, 2019 H TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA KWA KIPINDI CHA KUANZIA FEBRUARI, 2019 HADI JANUA TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA KWA KIPINDI CHA KUANZIA FEBRUARI, 2019 HADI JANUA TAARIFA YA SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA KWA KIPINDI CHA KUANZIA FEBRUARI 2019 HADI JA TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO KUHUSU SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA KWA KIPINDI CHA KUANZIA FEBRUARI, 2019 HADI J HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO NA CHAKULA HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WI TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU WIZARA YA MAJI KWA MWAKA WA FEDHA 20 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI TAARIFA YA SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA KWA KIPINDI CHA JANUARI, 2021 HADI JANUARI, 20 MAONI YA KAMATI KUHUSU UTEKELEZAJI WA BAJETI YA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO PAMOJA NA MAFUNGU YALIYO CHINI YAKE KWA MWAKA WA FEDHA MAONI YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA FEDHA WA MWAKA 2022 TAARIFA KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA WIZARA YA NISHATI (FUNGU 58) KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022 TAARIFA YA KAMATI KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022 TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU UCHUNGUZI WA TUHUMA KUVUNJA HAKI ZA BUNGE KWA KUSEMA UONGO TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU TUHUMA ZINAZOMKABILI MHE. JOSEPHAT MATHIAS GWAJIMA TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU NA BAJETI YA WIZARA YA UTAMADU TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA KUHUSU UTEKELEZAJI WA BAJETI YA OFISI YA WAZIRI MKUU KWA MWAKA WA FEDHA 2 TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA WIZARA YA KILIMO KWA MWAKA WA FED TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA WIZARA YA MAMBO YA NDAN TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU KUHUSU UTEKELEZAJI WA BAJETI YA WIZARA YA HABARI MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA MWAKA 2021/2022 TAARIFA YA MWAKA KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA KAMATI YA BUNGE YA BAJETI KATIKA KIPINDI CHA MWEZI JANUARI, 2021 HADI MWEZI JAN TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO KWA KIPINDI CHA JANUARI 2021 HADI FEBRUARI 2022 TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA KWA KIPINDI CHA FEBRUARI 2021 - FEBRUARI TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA KUANZIA JANUARI, 2021 HADI FEBRUARI, 2022 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI MAONI YA KAMATI KUHUSU MUSWADA WA MAREKEBISHO YA SHERIA MBALIMBALI ZA FEDHA NAMBA 13 WA MWAKA TAARIFA YA KAMATI KUHUSU RIPOTI ZA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA HESABU ZILIZOKAGULIWA ZA SERIKALI KUU, MASHI AARIFA KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU NA BAJETI YA WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU MAONI YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA ULINZI WA T MAPENDEKEZO YA MAAZIMIO YA BUNGE KUTOKANA NA TAARIFA YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU HESABU ZA SERIKALI Z KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA MAONI YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA M KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA MAONI YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA U MAONI YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA USIMAMIZI WA RASLIMALI ZA MAJI WA MWAKA 2 MAONI YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA KUHUSU AZIMIO LA BUNGE LA KURIDHIA ITIFAKI YA MKATABA WA UMO MAPENDEKEZO YA MAAZIMIO YA BUNGE KUTOKANA NA TAARIFA ZA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA UKAGUZI WA HESABU ZA SE MAPENDEKEZO YA MAAZIMIO YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA 2020/2021 KAMATI YA BUNGE YA BAJETI TAARIFA YA KAMATI YA BUNGE YA BAJETI KUHUSU MAPENDEKEZO YA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA WA MWAKA 2023/24 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA MAONI YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA KUHUSU AZIMIO LA BUNGE KURIDH TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO KUHUSU UCHAMBUZI WA SHERIA NDOGO TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI KUHUSU UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZAKE KATIKA KIPINDI CHA KUANZIA MWEZI JANUARI, 2016 TAARIFA YA KAMATI KUHUSU MUSWADA WA MAREKEBISHO YA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA WA MWAKA 2016 TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA KAMATI KWA KIPINDI CHA JANUARI 2016 HADI JANUARI 2017 TAARIFA YA KAMATI KUHUSU TAARIFA YA HESABU ZILIZOKAGULIWA ZA SERIKALI KUU NA MASHIRIKA YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA ULIOISHIA JUNI 3 TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI KWA MWAKA 2016/2017 TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI KWA KIPINDI CHA JANUARI, 2021 HADI FEBRUARI, 2022 TAARIFA YA KWANZA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO KUHUSU UCHAMBUZI WA SHERIA NDOGO TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU KWA KIPINDI CHA JANUARI 2021 HADI FEBRUARI 2022 TAARIFA YA KAMATI KUHUSU HESABU ZILIZOKAGULIWA ZA SERIKALI ZA MITAA KWA MWAKA WA FEDHA 2013/14 NA 2014/15 TAARIFA YA MWAKA KUHUSU TAARIFA YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA HESABU ZILIZOKAGULIWA ZA MAMLAKA ZA SERIKALI TAARIFA YA SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI KWA KIPINDI CHA KUANZIA JANUARI 2021 HA TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA KWA KIPINDI CHA JANUARI 2021 HADI FEBRUARI 2022 TAARIFA YA KAMATI YA BUNGE YA BAJETI KUHUSU MAPENDEKEZO YA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA PAMOJA NA MWONGOZO WA KUTAYARISHA MPANGO N TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU NA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII KWA MWAKA 2021/2022 TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI KUHUSU MAPENDEKEZO YA NYONGEZA YA BAJETI YA MWAKA 2021/22 TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA (PIC) KWAKIPINDI CHA KUAN TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA MHE. JOSEPH MBILINYI (MB) KUHUSIANA NA KUTOA ISHARA YA MA TAARIFA YA MWAKA YA KAMATI KUHUSU TAARIFA ZA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI KWA HESABU ZILIZOKAGULIWA ZA SERIKALI KUU NA MAS TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA KWA KIPINDI CHA JANUARI, 2021- FEBRUA TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII KWA KIPINDI C HA JANUARI, 2021 HADI FEBRUA TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO KUHUSU UCHAMBUZI WA SHERIA NDOGO ZILIZOWASILISHWA BUNGENI KWENYE MKUTANO WA T TAARIFA YA KWANZA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO KUHUSU UCHAMBUZI WA SHERIA NDOGO 2016 MAONI YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI KUHUSU MUSWADA WA MABADILIKO YA SHERIA MBALIMBALI NA 6 TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA (PIC) KWA KIPINDI CHA JANUARI , 2016 HADI TAARIFA KUHUSU UCHAMBUZI WA SHERIA NDOGO ZILIZOWASILISHWA KATIKA MKUTANO WA KUMI NA NANE NA MKUTANO WA KUMI NA TISA WA BUNGE JUNI TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII KUANZIA JANUARI, 2016 HADI JANUARI 2017 TAARIFA YA KAMATI KUHUSU TAARIFA YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA HESABU ZILIZOKAGULIWA ZA MAMLAKA ZA SERIKAL TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC) KUHUSU TAARIFA ZA UKAGUZI ZA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU Z TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA KWA KIPINDI CHA JANUARI 2016 HADI JANUARI 2017 TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU NA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII KWA MWAKA 2019/ 2020 BUNGE LA TANZANIA KAMATI YA BUNGE YA MASUALA YA UKIMWI TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA KAMATI KWA KIPINDI CHA FEBRUARI 2019 TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA KUANZIA JANUARI, 2016 HADI JANUARI, 2017 TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI ZILIZOTEKELEZWA KATIKA KIPINDI CHA KUANZIA JANUARI,2016 HADI TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA KWA MWAKA 2016/2017 MAONI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KATIKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KUHUSU MAPANDEKEZO YA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA 2017 HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KATIKA WIZARA YA HABARI KATIKA WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, WASANII NA M TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU NA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI KWA MWAKA 2019/2020 TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA KWA KIPINDI CHA FEBRUARI 2019, HADI J KAMATI YA BUNGE YA BAJETI,TAARIFA YA KAMATI KUHUSU MUSWADA WA MAREKEBISHO YA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA,28 JUNI 2016 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU NA SHUGHULI ZA KAMATI KWA MWAKA 2018/2019 TAARIFA YA MWAKA YA SHUGHULI ZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA KWA KIPINDI CHA FEBRUARI 2018, HADI J KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC) TAARIFA YA SHUGHULI ZA KAMATI KWA MWAKA 2019 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA TATU Kikao cha Thelathini na Saba – Tarehe 26 Mei, 2021 kanuni ya adhabu MAREKEBISHO YA SHERIA MBALIMBALI ZA FEDHA 2022 BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) BUNGE TANZANIA MAJADILIANO BUNGE MKUTANO(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI (BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA TANZANIA MAHAKAMA KUU DIVISHENI ES SALAAM MAOMBI MAREJEO NA BAINA MAOMBI NA MJIBU MAOMBI(BATCH) MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU MAHAKAMA KUU Mkutano wa kumi na moja Kikao cha thelathini na nne 26 Mei 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Nane Tarehe 1 Juni, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Tano Tarehe 29 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Sita Tarehe 30 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Saba Tarehe 31 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 2 Juni, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini Ð Tarehe 5 Juni, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Moja Tarehe 6 Juni, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Mbili Tarehe 7 Juni, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Tatu Tarehe 8 Juni, 2023 Mkutano wa Pili, Kikao cha Kwanza Febuari 8 2011 Mkutano wa Kumi na Tisa, Kikao cha Tisa - Tarehe 29 Aprili, 2005 Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Kwanza Tarehe 7 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Pili - Tarehe 8 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Tatu Tarehe 9 Juni, 2005. Mkutano wa sita kikao cha kwanza mwaka 2012 Mkutano wa sita kikao cha pili mwaka 2012 Mkutano wa sita kikao cha tatu mwaka 2012 Mkutano wa sita kikao cha nne mwaka 2012 Mkutano wa sita kikao cha tano mwaka 2012 Mkutano wa sita kikao cha sita mwaka 2012 Mkutano wa sita kikao cha saba cha mwaka 2012 Mkutano wa sita kikao cha nane mwaka 2012 Mkutano wa sita kikao cha nane cha mwaka 2012 Mkutano wa Pili, Kikao cha Tatu mkutano wa sita, kikao cha kwanza 31 januari 2017 Mkutano wa Pili, Kikao cha Pili 9 Februari, 2011 Mkutano wa siba kikao cha kwanza mwaka 2012 Mkutano wa nne kikao cha kumi na tatu mwaka 2011 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Ishirini na Mbili - Tarehe 2 Julai, 2010 Mkutano wa nne kikao cha kumi na nne mwaka 2011 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Ishirini na Tatu - Tarehe 3 Julai, 2010 Mkutano wa nne kikao cha kumi na tano mwaka 2011 Mkutano wa nne kikao cha kumi na sita mwaka 2011 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Ishirini na Tano - Tarehe 6 Julai, 2010 MKUTANO WA NNE Kikao cha Kumi na Saba mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Kumi na Tisa mwaka 2011 Mkutano wa ishirini Kikao cha Ishirini na Sita - Tarehe 8 Julai, 2010 MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Moja mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Mbili mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Tatu mwaka 2011 MKUTANO WA SABA Kikao cha Arobaini na Mbili Tarehe 6 Juni, 2017 MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne cha mwaka 2011 MKUTANO WA SABA Kikao cha Arobaini na Nne – Tarehe 8 Juni, 2017 MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Tano cha mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Sita 2011 MKUTANO WA SABA Kikao cha Arobaini na Tatu – Tarehe 7 Juni, 2017 MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Saba cha mwaka 2011 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Ishirini na Saba - Tarehe 9 Julai, 2010 MKUTANO WA SABA Kikao cha Hamsini na Moja – Tarehe 20 Juni, 2017 MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nane cha mwaka 2011 MKUTANO WA SABA Kikao cha Hamsini na Nane – Tarehe 3 Julai, 2017 MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Tisa cha mwaka 2011 MKUTANO WA SABA Kikao cha Hamsini na Tano – Tarehe 28 Juni, 2017 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Ishirini na Tisa - Tarehe 13 Julai, 2010 MKUTANO WA SABA Kikao cha Hamsini na Tatu – Tarehe 22 Juni, 2017 MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini cha mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Moja cha mwaka 2011 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini – Tarehe 2 Mei, 2018 MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Ishirini na Mbili 2015 MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Mbili cha mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Tatu cha mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Nne cha mwaka 2011 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Sita– Tarehe 24 Aprili, 2018 MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Tano mwaka 2011 MKUTANO WA NANE Kikao cha Kwanza – Tarehe 5 Septemba, 2017 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Nane – Tarehe 8 Februari, 2018 MKUTANO WA NNE Kikao cha Thealathini na Sita mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Saba mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Nane mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Thelathini na Tisa mwaka 2011 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nane – Tarehe 12 Aprili, 2018 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Ishirini na Tisa - Tarehe 13 Julai, 2010 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini mwaka 2011 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Nne – Tarehe 2 Februari, 2018 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Thelathini - Tarehe 14 Julai, 2010 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini mwaka 2011 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Thelathini na Moja - Tarehe 15 Julai, 2010 MKUTANO WA NANE Kikao cha Pili – Tarehe 6 Septemba, 2017 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Mbili mwaka 2011  MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Moja mwaka 2011 bunge la Tanzania kikao cha 36 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Saba – Tarehe 7 Februari, 2018 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Tatu mwaka 2011 bunge la Tanzania kikao cha 1 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Sita – Tarehe 6 Februari, 2018 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Nne mwaka 2011 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Kumi na Mbili - Tarehe 21 Juni, 2010 mkutano wa 7 kikao cha 14 MKUTANO WA SABA Kikao cha Sitini – Tarehe 5 Julai, 2017  MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Tano Tarehe mwaka2011 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Kumi na Tatu - Tarehe 22 Juni, 2010 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Kumi na Nne - Tarehe 23 Juni, 2010 mkutano 7 kikao cha 13 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Sita mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Saba mwaka 2011 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tatu – Tarehe 1 Februari, 2018 MKUTANO WA NANE Kikao cha Tatu – Tarehe 7 Septemba, 2017 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Kumi na Tano – Tarehe 24 Juni 2010 MKUTANO WA SABA Kikao cha Thelathini na Tisa – Tarehe 1 Juni, 2017 mkutano wa 6 kikao cha 2 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Kumi na Sita - Tarehe 25 Juni, 2010 mkutano wa 6 kikao cha 3 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tisa – Tarehe 9 Februari, 2018 mkutano wa 7 kikao cha 15 mkutano wa 6 kikao cha 4 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Saba mwaka 2011 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Kumi na Saba – Tarehe 26 Juni, 2010 mkutano wa 7 kikao cha 16 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Nane mwaka 2011 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Kumi na Nane - Tarehe 28 Juni, 2010 mkutano wa 7 kikao cha 1 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Tisa mwaka 2011 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Kumi na Tisa - Tarehe 29 Juni, 2010 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Moja mwaka 2011 MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Arobaini na Saba – Tarehe 16 Juni, 2020 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Ishirini - Tarehe 30 Juni, 2010 mkutano wa 6 kikao cha 5 MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Arobaini na Moja - Tarehe 9 Juni, 2020 Mkutano wa Ishirini Kikao cha Ishirini na Moja – Tarehe 1 Julai, 2010 MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Arobaini na Nne- Tarehe 12 Juni, 2020 mkutano wa 7 kikao cha 17  MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Tano mwaka2011 MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Moja - Tarehe 1 Juni, 2021 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Sita mwaka 2011 Mkutano wa Pili Kikao cha Kwanza – Tarehe 08 Februari, 2011 MKUTANO WA TANO Kikao cha Kwanza 2011 MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Saba - Tarehe 8 Juni, 2021 Mkutano wa Pili Kikao cha Pili – Tarehe 9 Februari, 2011 MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Nane - Tarehe 9 Juni, 2021 MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Mbili - Tarehe 2 Juni, 2021 Mkutano wa Pili Kikao cha Tatu – Tarehe 10 Februari, 2011 mkutano wa 7 kikao cha 2 MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Nne – Tarehe 4 Juni, 2021 Mkutano wa Pili Kikao cha Nne – Tarehe 11 Februari, 2011 MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini - Tarehe 31 Mei, 2021 Mkutano wa Nne Kikao cha Tatu –Tarehe 13 Juni, 2011 MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Arobaini - Tarehe 8 Juni, 2020 Mkutano wa Pili Kikao cha Tano – Tarehe 14 Februari, 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Pili – Tarehe 1 Septemba, 2021 Mkutano wa Pili Kikao cha Sita–Tarehe 15 Februari, 2011 MKUTANO WA SITA Kikao cha Pili – Tarehe 2 Februari, 2022 Mkutano wa Pili Kikao cha Saba – Tarehe 17 Februari, 2011 Mkutano wa Pili Kikao cha Nane – Tarehe 18 Februari, 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Nane mwaka2011 MKUTANO WA SITA Kikao cha Pili – Tarehe2Februari, 2022 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Moja mwaka2011 MKUTANO WA PILI Kikao cha Pili – Tarehe 3 Februari, 2021 MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Thelathini na Mbili - Tarehe 16 Julai, 2010 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Mbili mwaka 2011 MKUTANO WA TANO Kikao cha Pili – Tarehe 3 Novemba, 2021 MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Kwanza – Tarehe 27 Januari, 2009 MKUTANO WA SABA Kikao cha Pili – Tarehe 6 Aprili, 2022 MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao cha Pili – Tarehe 6 Novemba, 2019 MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KWANZA Kikao cha Pili – Tarehe 11 Novemba, 2020 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Nne 2011 MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Pili - Tarehe 29 Januari, 2020 MKUTANO WA TATU Kikao cha Pili – Tarehe 31 Machi, 2021 MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Saba - Tarehe 5 Februari, 2020 MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Pili – Tarehe 28 Januari, 2009 MKUTANO WA NNE Kikao cha Saba – Tarehe 8 Septemba, 2021 MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Tatu – Tarehe 29 Januari, 2009 MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Saba – Tarehe 9 Aprili, 2020 MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Nne – Tarehe 30 Januari, 2009 MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Tano - Tarehe 2 Februari, 2009 MKUTANO WA SITA Kikao cha Saba – Tarehe 9 Februari, 2022 MKUTANO WA PILI Kikao cha Saba – Tarehe 10 Februari, 2021 MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Sita - Tarehe 3 Februari, 2009 MKUTANO WA TATU Kikao cha Saba – Tarehe 12 Aprili, 2021 MKUTANO WA KUMI NNE Kikao cha Saba – Tarehe 4 Februari, 2008 MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao cha Saba - Tarehe 13 Novemba, 2019 MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Sita – Tarehe 4 Februari, 2020 MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Nane – Tarehe 5 Februari, 2009 MKUTANO WA KUMI NA NNE Kikao cha Tisa – Tarehe 6 Februari, 2009 MKUTANO WA NNE Kikao cha Sita – Tarehe 7 Septemba, 2021 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Sita – Tarehe 8 Aprili, 2020 MKUTANO WA KUMI NA TATU Kikao cha Tisa – Tarehe 7 Novemba, 2008 MKUTANO WA SITA Kikao cha Sita – Tarehe 8 Februari, 2022 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Nne mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Tano mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Sita mwaka2011 MKUTANO WA TANO Kikao cha Kwanza mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Nane mwaka 2011 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Moja mwaka 2011 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Arobaini na Mbili – Tarehe 11 Agosti, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Arobaini na Tatu – Tarehe 12 Agosti, 2008 MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Tano – Tarehe 25 Agosti, 2011 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Arobaini na Nne – Tarehe 13 Agosti, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Arobaini na Tano – Tarehe 14 Agosti, 2008 Kikao cha Hamsini na Sita 2011 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Arobaini na Sita – Tarehe 15 Agosti, 2008 MKUTANO WA TANO Kikao cha Kwanza 2011 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Arobaini na Saba – Tarehe 18 Agosti, 2008 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Pili 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Arobaini na Tisa – Tarehe 20 Agosti, 2008 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tatu 2013 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Nne 2013 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tano 2013 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Sita 2013 MKUTANO WA KUMI Kikao cha saba mwaka 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Hamsini na Moja – Tarehe 22 Agosti, 2008 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Nane2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Hamsini na Mbili – Tarehe 25 Agosti, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Mbili – Tarehe 11 Julai, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao Cha Ishirini na Tatu – Tarehe 14 Julai, 2008 MKUTANO WA KUMI Kikao cha Tisa 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 15 Julai, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 16 Julai, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Sita – Tarehe 17 Julai, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Saba – Tarehe 18 Julai, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tatu mwaka 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Nane – Tarehe 21 Julai, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Tisa – Tarehe 22 Julai, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nne 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tano mwaka 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Thelathini – Tarehe 23 Julai, 2008 MKUTANO WA TATU Kikao cha Sita – Tarehe 9 Aprili, 2021 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Thelathini na Moja – Tarehe 24 Julai, 2008 MKUTANO WA PILI Kikao cha Sita – Tarehe 9 Februari, 2021 MKUTANO WA TANO Kikao cha Sita – Tarehe 9 Novemba, 2021 MKUTANO WA SABA Kikao cha Sita – Tarehe 13 Aprili, 2022 MKUTANO WA TATU Kikao cha Sitini – Tarehe 28 Juni, 2021 MKUTANO WA TATU Kikao cha Sitini na Mbili – Tarehe 30 Juni, 2021 MKUTANO WA TATU Kikao cha Sitini na Moja – Tarehe 29 Juni, 2021 MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Tano – Tarehe 3 Februari, 2020 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 27 Juni, 2008 MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Tano – Tarehe 6 Aprili, 2020 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kumi na Nne – Tarehe 30 June, 2008 MKUTANO WA TATU Kikao cha Tano – Tarehe 8 Aprili, 2021 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tatu mwaka 2013 MKUTANO WA PILI Kikao cha Tano – Tarehe 8 Februari, 2021 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Pili mwaka 2013 MKUTANO WA TANO Kikao cha Tano – Tarehe 8 Novemba, 2021 MKUTANO WA KUMI NA SABA Kikao cha Tano - Tarehe 11 Novemba, 2019 MKUTANO WA TATU Kikao cha Tatu – Tarehe 1 Aprili, 2021 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Mbili – Tarehe 18 Aprili, 2018 MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Tatu – Tarehe 2 Aprili, 2020 MKUTANO WA NNE Kikao cha Tatu – Tarehe 2 Septemba, 2021 MKUTANO WA SITA Kikao cha Tatu – Tarehe 3 Februari, 2022 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kumi na Tano – Tarehe 1 Julai, 2008 MKUTANO WA NANE Kikao cha Sita – Tarehe 12 Septemba, 2017 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Pili 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kumi na Sita – Tarehe 2 Julai, 2008 MKUTANO WA NANE Kikao cha Tisa – Tarehe 15 Septemba, 2017 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kumi na Saba – Tarehe 3 Julai, 2008 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tatu mwaka 2013 Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Nne – Tarehe 10 Juni, 2005. Mkutano wa Pili, Kikao cha Tisa - Tarehe 17 Februari, 2006. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Ishirini na Moja – Tarehe 5 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Kumi na Sita - Tarehe 28 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Kumi na Tano – Tarehe 27 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao Cha Kumi na Tatu - Tarehe 23 Juni, 2005. mkutano 7 wa kikao cha 17 mkutano wa 7 kikao cha 2 mkutano wa 7 kikao cha 18 mkutano wa 7 kikao cha 3 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kumi na Nane – Tarehe 4 Julai, 2008 mkutano wa 6 kikao cha 6 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kumi na Tisa – Tarehe 8 Julai, 2008 mkutano wa 6 kikao cha 8 MKUTANO WA KUMI NA MBILI KIKAO CHA ISHIRINI – TAREHE 9 JULAI, 2008 mkutano wa 7 kikao cha 19 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Moja – Tarehe 10 Julai, 2008 MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Thelathini - Tarehe 16 Julai, 2009 mkutano wa 6 kikao cha 9 MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Moja - Tarehe 17 July, 2009 MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Thelathini na Mbili - Tarehe 18 Julai, 2009 mkutano wa 6 kikao cha 9 MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Thelathini na Nne - Tarehe 21 Julai, 2009 mkutano wa 7 kikao cha 20 mkutano wa 7 kikao cha 4 mkutano wa 7 kikao cha 4 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tatu – Tarehe 5 Aprili, 2018 mkutano wa 6 kikao cha 10 MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Thelathini na Tano - Tarehe 22 Julai, 2009 mkutano wa 7 kikao cha 21 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tano – Tarehe 9 Aprili, 2018 MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Thelathini Na Sita - Tarehe 23 Julai, 2009 Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Tano - Tarehe 13 Juni, 2005. MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Thelathini na Saba - Tarehe 24 Julai, 2009 Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Sita - Tarehe 14 Juni, 2005. MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nne - Tarehe 6 Aprili, 2018 MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Thelathini na Nane - Tarehe 25 Julai, 2009) Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Saba - Tarehe 15 Juni, 2005. mkutano wa 7 kikao cha 5 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Sita – Tarehe 10 Aprili, 2018 MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Thelathini na Tisa - Tarehe 27 Julai, 2009) MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Ishirini - Tarehe 3 Julai, 2009 MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Arobaini - Tarehe 28 Julai, 2009 mkutano wa 7 kikao cha 20 mkutano wa 6 kikao cha 10 mkutano wa 7 kikao cha 5 mkutano wa 7 kikao cha 22 mkutano wa 7 kikao cha 6 mkutano wa 7 kikao cha 23 mkutano wa 7 kikao cha 7 mkutano wa 7 kikao cha 24 mkutano wa 7 kikao cha 25 mkutano wa 7 kikao cha 26 mkutano wa 7 kikao cha 27 mkutano wa 7 kikao cha 8 mkutano wa 7 kikao cha 28 mkutano wa 7 kikao cha 9 mkutano wa 7 kikao cha 29 kikao cha 10 kikao cha 30 kikao cha 31 kikao cha 32 kikao cha 11 kikao cha 33 kikao cha 12 kikao cha 34 kikao cha 35 kikao cha 13 kikao cha 14 mkutano wa 2 kikao cha 4 mkutano wa 3 kikao cha 53 kikao cha 9 mkutano wa 3 kikao cha 54 mkutano wa 3 kikao cha 32 mkutano wa 3 kikao cha 33 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Mbili 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Tatu 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Nne 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Tano 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Sita 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Saba 2013 mkutano wa 2 kikao cha 5 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Nane 2013 mkutano wa 3 kikao cha40 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Tisa 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini 2013 mkutano wa 5 kikao cha 2 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Pili - Tarehe 10 Aprili, 2013 mkutano wa 2 kikao cha 6 mkutano wa 3 kikao cha 35 mkutano wa 3 kikao cha 10 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tatu 2013 mkutano wa 5 kikao cha 3 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nne - Tarehe 12 Aprili, 2013 mkutano wa 2 kikao cha 7 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tano – Tarehe 15 Aprili, 2013 mkutano wa 3 kikao cha 36 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Sita 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Saba - Tarehe 17 Aprili, 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nane 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Tisa 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Moja 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Moja 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Mbili 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Tatu 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Tano 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Sita 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Sita - Tarehe 15 Mei, 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Saba 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na Tisa 2013 ? MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Moja -2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Mbili – Tarehe 23 Mei, 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Tatu 2012 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Nne - Tarehe 25 Mei, 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Saba 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Nane 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Tisa 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Moja 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Mbili 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Nne 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Tano 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Sita 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Saba – 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Nane – 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini - 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Moja-Tarehe 18 Juni, 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Mbili – 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tatu – 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Nne - Tarehe 21 Juni, 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tano - 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Sita - 2013 ?MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Saba - 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Nane - 2013 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tisa – 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Kwanza - 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Pili – 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Tatu – 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao Cha Nne 2013 MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Tano – 2013 MKUTANO WA SABA Kikao cha Nane Tarehe 2012 MKUTANO WA SABA Kikao cha Tisa – 2012 MKUTANO WA SABA Kikao cha Kumi 2012 MKUTANO WA SABA Kikao cha Kumi na Moja 2012 MKUTANO WA NANE Kikao cha Pili – 2012 MKUTANO WA NANE Kikao cha Tatu 2012 ?MKUTANO WA NANE Kikao cha Nne – 2012 ?MKUTANO WA NANE Kikao cha Tano – 2012 MKUTANO WA NANE Kikao cha Sita – 2012 ?MKUTANO WA NANE Kikao cha Saba – 2012 Kikao cha Nane 2012 MKUTANO WA NANE Kikao cha Tisa 2012 ?MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi 2012 ?MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Moja 2012 MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Mbili 2012 ? MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – 2012 Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Nane - Tarehe 16 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Tisa - Tarehe 17 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Kumi - Tarehe 20 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Kumi na Moja - Tarehe 21 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini. Kikao cha Kumi na Mbili - Tarehe 22 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Kumi na Nne - Tarehe 24 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Kumi na Saba - Tarehe 29 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Kumi na Nane - Tarehe 30 Juni, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Kumi na Tisa - Tarehe 1 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Ishirini - Tarehe 4 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Ishirini na Mbili - Tarehe 6 Julai, 2005. Mkutano wa Pili, Kikao cha Nane - Tarehe 16 Februari, 2006. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Ishirini na Tatu - Tarehe 8 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Ishirini na Nne - Tarehe 11 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Ishirini na Tano - Tarehe 12 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao Cha Ishirini na Sita - Tarehe 13 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Ishirini na Saba - Tarehe 14 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Ishirini na Nane - Tarehe 15 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Ishirini na Tisa - Tarehe 18 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Thelathini - Tarehe 19 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Thelathini na Moja - Tarehe 20 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Thelathini na Mbili - Tarehe 21 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Thelathini na Tatu – Tarehe 22 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Thelathini na Nne – Tarehe 25 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Thelathini na Tano – Tarehe 26 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Thelathini na Sita – Tarehe 27 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Thelathini na Saba - Tarehe 28 Julai, 2005. Mkutano wa Ishirini, Kikao cha Thelathini na Nane - Terehe 29 Julai, 2005. Mkutano wa Kwanza, Kikao Cha Kwanza - Tarehe 28 Desemba, 2005. Mkutano wa Kwanza, Kikao cha Pili – Tarehe 29 Desemba, 2005. Mkutano wa Kwanza, Kikao cha Tatu - Tarehe 30 Desemba, 2005. Mkutano wa Pili, Kikao cha Kwanza - Tarehe 7 Februari, 2006. Mkutano wa Pili, Kikao cha Pili - Tarehe 8 Februari, 2006. Mkutano wa Pili, Kikao cha Tatu – Tarehe 9 Februari, 2006. Mkutano wa Pili, Kikao cha Nne - Tarehe 10 Februari, 2006. Mkutano wa Pili, Kikao cha Tano - Tarehe 13 Februari, 2006. Mkutano wa Pili, Kikao cha Sita - Tarehe 14 Februari, 2006. Mkutano wa Pili, Kikao cha Saba – Tarehe 15 Februari, 2006. MKUTANO WA TISA Kikao cha Kwanza Tarehe 1 Novemba, 2022 MKUTANO WA TISA Kikao cha Pili Tarehe 2 Novemba, 2022 MKUTANO WA TISA Kikao cha Nne Tarehe 4 Novemba, 2022 MKUTANO WA TISA Kikao cha Tano Tarehe 5 Novemba, 2022 MKUTANO WA TISA Kikao cha Sita Tarehe 7 Novemba, 2022 MKUTANO WA TISA Kikao cha Saba Tarehe 8 Novemba, 2022 MKUTANO WA TISA Kikao cha Nane Tarehe 9 Novemba, 2022 MKUTANO WA TISA Kikao cha Tisa Tarehe 10 Novemba, 2022 MKUTANO WA TISA Kikao cha Kumi Tarehe 11 Novemba, 2022 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Mbili - Tarehe 24 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na tatu - Tarehe 25 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na nne - Tarehe 27 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na tano - Tarehe 28 Aprili, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Sita - Tarehe 2 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Saba - Tarehe 3 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Nane - Tarehe 4 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Kumi na Tisa - Tarehe 5 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha ishirini - Tarehe 8 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na moja - Tarehe 9 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na mbili - Tarehe 10 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na tatu - Tarehe 11 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na nne - Tarehe 12 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na tano - Tarehe 15 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na sita - Tarehe 16 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na saba - Tarehe 17 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Ishirini na nane - Tarehe 18 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini - Tarehe 22 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na moja - Tarehe 23 Mei, 2023 MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na mbili - Tarehe 24 Mei, 2023 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA KIKAO CHA AROBAINI NA TANO BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA KIKAO CHA HAMSINI NA SABA BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA KIKAO CHA HAMSINI BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA KIKAO CHA AROBAINI NA NNE BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA KIKAO CHA AROBAINI NA SITA BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA KIKAO CHA AROBAINI NA SABA BUNGE LA TANZANIAMAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA KIKAO CHA AROBAINI NA NANE BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA KIKAO CHA AROBAINI NA TISA BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA KIKAO CHA AROBAINI NA TISA Tarehe 15 Juni, 2023 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Moja – Tarehe 20 Juni, 2023 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Mbili – Tarehe 21 Juni, 2023 TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU NA SHUGHULI ZA KAMATI KWA MWAKA 2018/2019 Kanuni na hotuba Kanuni na hotuba Kanuni na hotuba Kanuni na hotuba Kanuni na hotuba Kanuni na hotuba Kanuni na hotuba Kanuni na hotuba Kanuni na hotuba MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Tano MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Nane MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Tisa MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Moja MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Mbili MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Tatu MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Nne MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Tano MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Sita MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Saba MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Nane MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Arobaini na Tisa MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Moja MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Mbili MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Nne MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Saba MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Sita MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Thelathini na Saba Sayansi na Teknolojia Tanzania HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO SAYANSI NA TEKNOLOJIA Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 mpango wa maendeleo tanzania wa mwaka 2017.18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO BAJETI YA SERIKALI YA MWAKA WA FEDHA 2019/20 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 Mwongozo wa Matumizi Bora, Sahihi na Salama ya Vifaa na Mifumo ya TEHAMA Serikalini wa mwaka 2012 utekelezaji wa Bajeti ya Mfuko wa Bunge Taarifa ya Mwaka ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Utekelezaji wa Majukumu na shughuli za Kamati Jamii kuhusu Utekelezaji wa Majukumu na shughuli za Kamati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI Tathmini ya Utekelezaji wa Bajeti ya Serikali katika kipindi cha nusu Mwaka Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Bunge katika kushugulikia maeneo yenye matumizi mabaya ya fedha za umma katika wizara za Serikali na mashirika ya umma ni Kamati y Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Umma (PIC) Taarifa ya Mwaka ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria utekelezaji ikiwa ni pamoja na mafanikio na changamoto zilizojitokeza kuliwezesha Bunge kuijadili na hatimaye kuamua kutokana na mapendekezo yanayotolewa Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii KAULI YA WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA KUHUSIANA NA KUIBUKA KWA MAGONJWA YA MAZAO MBALIMBALI NA HASA UGONJWA MPYA WA MAHIND Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, zimeundwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Iba Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria 1518096950-Taarifa ya Kamati-Sheria Ndogo 1518176020-Taarifa ya Kamati- Mambo ya Nje 1537420922-Taarifa ya Kamati - Sheria Ndogo 1541658781-Maoni ya KRUB-Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2019-2020 1541774982-Taarifa na Maoni ya Kamati ya Bajeti kuhusu Mpango 2019-20 1542378315-Maoni ya KRUB-Azimio la Takwimu wa Afrika 1542378951-Maoni na Ushauri wa Kamati ya Bajeti-Takwimu Afrika 1549190296-Taarifa ya Kamati ya Mwaka -PAC (Swahili Version) 1549190505-Taarifa ya Mwaka ya Kamati -LAAC (Swahili Version) 1549191126-TAARIFA YA MWAKA - KAMATI YA BAJETI-Swahili Bajeti 1549191206-TAARIFA MWAKA -PIC (Swahili Version) 1549297460-Taarifa ya Mwaka 2018-19 Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira 1549383788-Taarifa ya Mwaka 2018- 2019 Kamati ya Kilimo , Mifugo na Maji 1549383871-Taarifa ya mwaka 2019 - Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii 1518176195-Taarifa ya Kamati-Maadili 1549297244-TAARIFA YA MWAKA 2018 HADI JANUARI 2019-Kamati ya Miundombinu 1518097176-Taarifa ya Kamati-Katiba na Sheria 1542377797-Maoni ya Kamati Mambo ya Nje-Uzuiaji Silaha na Sumu 1542377946-Maoni ya KRUB- Uzuiaji Silaha na Sumu BAJETI YA WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA KWA MWAKA 2012 - 2013... HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOL UTARATIBU WA UTEKELEZAJI WA MIFUMO MBALIMBALI YA TEHAMA KATIKA UTUMISHI WA UMMA Lipumba JK atamaliza urais vibaya Utenzi wa siku ya sheria, kanda ya Dar es salaam TAARIFA KUHUSU UTEKELEZAJI WA BAJETI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022 TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO KUHUSU UCHAMBUZI WA SHERIA NDOGO ZILIZOWASILISHWA BUNGENI KWENYE MKUTANO WA T Makuadi wa Soko Huria Almasi za Bandia IJUE SHERIA YA ARDHI NA TARATIBU ZINAZOHUSIKA KUPATA, KUMILIKI NA KUUZA ARDHI VIJIJINI NA MJIN SHIRIKA LA AFYA DUNIANI LAADHIMISHA MIAKA 60 TANGU KUANZISHWA KWAKE UCHUMI WA BLUU KATIKA KUKUZA PATO LA TAIFA CNC teknolojia_ 2010 Mkono Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Publishing House Kitabu - Kurasa [1] - Dunia maarifa encyclopedic ATHARI ZA SIASA KWENYE SEKTA YA UMEME Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kukabidhi bil. 568 kwa vijana wabunifu – Dar24 Adha ya Heri Mageuzi ya Uchumi Mambo muhimu ya kufahamu kuhusu muswada mpya wa sheria ya huduma za habari Tanzania Mzozo wa matumizi ya maji ya Mto Nile Katibu Mkuu Ban kuzuru Bara la Afrika UKOSEFU FEDHA ZA KUTOSHA KUGHARAMIA MIRADI YA MAENDELEO Ushiriki wa Kisiasa HAMAD ASHUTUMU UCHAGUZI KUWA SIO HURU NA WA HAKI VYAMA VIKUU VIGAWANE MADARAKA ZOEZI LA KUANDIKISHA WAPIGA KURA RAIS BENJAMIN MKAPA WA TANZANIA AMETOA ... CCM YAIBUKA NA USHINDI ZANZIBAR. UCHAGUZI TANZANIA WAREJESHWA NYUMA NI NANI ATAKAYESHIKILIA BENDERA YA CCM KATIKA UCHAGUZI MKUU WAPINZANI HAWATOMTAMBUA KIONGOZI MPYA RAIS KARUME ATAKA UTULIVU KATIKA MWEZI WA RAMADHAN CCM KUSHINDA UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA JOTO LA KISIASA VISIWANI ZANZIBAR WATANZANIA WASHEREHEKEA UHURU ZIARA YA RAIS MKAPA WA TANZANIA NCHINI UJERUMANI GHASIA ZAZUKA KATIKA KAMPENI ZANZIBAR WAPINZANI WASUSIA KIKAO CHA WAWAKILISHI CHAMA CHA UPINZANI CHALAUMU TUME KWA KUTOTOA MAAMUZI. MGOMBEA URAIS WA NCCR-MAGEUZI, TANZANIA DIRA YAIFIKISHA SERIKALI MAHKAMANI RAIS WA ZANZIBAR ATETEA MARUFUKU YA KUFANYIKA MIKUTANO YA KISIASA KWENYE VIWANJA VYA MICHEZO VIWANJA VYA MICHEZO MARUFUKU KUFANYIWA MIKUTANO MKAPA WA TANZANIA ZIARANI AFRIKA KUSINI RAU AZURU MAHAKAMA YA UM TANZANIA KIKWETE AONGOZA MAONI TANZANIA MUSTAKABALI WA UCHAGUZI WA TANZANIA MASHAKANI UCHAGUZI KUFANYIKA ZANZIBAR, BARA WAAHIRISHWA. WAKAZI WA ZANZIBAR WAPIGA KURA HII LEO POLISI WAFYATUWA MABOMU YA KUTOWA MACHOZI KAZI YA KUHESABU KURA INAENDELEA Rafiki na Adui wa Afrika – Utandawazi – DW – 08.01.2010 HALI YA UCHUMI DUNIANI MAKADIRIO YA KIUCHUMI UJERUMANI PAUL KRUGMAN APEWA TUZO LA NOBEL LA UCHUMI 2008 UCHUMI WA ANGOLA WATIA FORA BARANI AFRICA UCHUMI WA UJARUMANI NA UFARANSA WAIMARIKA UCHUMI WA UJERUMANI WAENDELEA KUKUA 2010 ulikuwa na mafanikio kwenye uhai-anuai Admin.WagnerD 4 Januari 2011 AFRIKA KATIKA MAGAZETI YA UJERUMANI,1 Agosti 2011 Afya na jamii 10 Mei 2012 June 15, 2011,WAZIRI DUNI AIELEZA UN MAFANIKIO YA AFYA TANZANIA Kisukari Ugonjwa hatari unaodharauliwa,10 Juni 2011 Kuathirika kwa Ukimwi si mwisho wa Maisha,30 Novemba 2011 Kutumia sheria kuhifadhi mazingira 24 Aprili 2012 MAITI AAMKA AFRIKA KUSINI NA KUANZA KUPIGA KELELE MONCHWARI!, AUGUST 2, 2011 Meli yatoa huduma za afya Tanzania,9 Novemba 2011 Njia za kupunguza uzito 25 Julai 2012 Siku ya kimataifa ya kupambana na ugonjwa wa kisukari,14 Novemba 2011 Ugonjwa wa kubambuka midomo 21 Desemba 2012 Ujuwe ugonjwa wa tete-kuwanga, 14 Septemba 2011 Ukimwi wasahaulika DRC 10 Februari 2012 Ukunga wa jadi waruhusiwa tena Malawi,16 Machi 2011 Unaijua idadi ya watu duniani hadi mwaka 2100,15 Mei 2011 Wageni wasioalikwa – Ugonjwa wa Malaria,Juni 2011 Uzalishaji wa mazao ya nafaka ni wa kuridhisha kwa kipindi cha 2013-2014 220711 Äthiopien Hunger,25 Julai 2011 Maisha ya mapambano katika viwanda vya chuma Tanzania 31 Mei 2012 Majadiliano ya mabadiliko ya tabia nchi , wajumbe washindwa kuafikiana 11 Desemba 2011 Tumejitayarisha kwa mvua za masika Matumaini yakoje katika kutano wa tabia nchi mjini Doha 26 Novemba 2012 Merkel ataka hatua kali zaidi kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi Halima Nyanza(ZPR) 4 Julai 2011 Mkutano wa mabadiliko ya tabia-nchi wamalizika Bonn 17 Juni 2011 Mto Ruaha hatarini kukauka,14 Septemba 2011 Äthiopien Hunger,25 Julai 2011 Majivu ya volkano yavuruga safari za ndege,25 Mei 2011 Mazingira Afrika – Kipindi 7 - 16 Machi 2011 Mazingira Afrika 16 Machi 2011,DW Mazungumzo kuhusiana na mazingira hayafiki popote 16 Juni 2011 Mkutano kati ya viongozi wa Umoja wa Ulaya na Afrika Kusini mjini Brussels 18 Septemba 2012 Sasa baiolojia-anwai ndiyo njia ya mazingira 16 Machi 2012 Uchafu bado kikwazo miji ya Afrika Mashariki 1 Aprili 2012 Uchumi na mazingira 10 Mei 2012 Uwindaji haramu tishio kwa wanyamapori, 10 Juni 2011 Vijana, mazingira na dunia ya kesho 10 Februari 2012 Afisa wa UN aonyesha shaka kuhusu Syria,14 Oktoba 2011.Imeboreshwa 17 Oktoba 2011 Nagona Gamba la Nyoka Kichwa Maji Dunia Uwanja wa Fujo Mzingile Rosa Misitika MAGEUZI YA KIUCHUMI TANZANIA VYAMA VYA SIASA VYAWEKA WAZI SURA MPYA YA SIASA MWAKA 2021 Waziri muu kukagua mradi wa sayansi, teknolojia na elimu ya juu Waziri mkuu akagua utekelezaji wa mradi wa sayansi, teknolojia na elimu ya juu SUA Kongamano la wanawake na teknolojia kufanyika nchini Alhamisi MIAKA 53 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR 2017 Waziri mkuu: Sheria za Tanzania zinakataa vitendo vya ulawiti PROF.MWANDOSYA AIPONGEZA DIT KUKUZA TEKNOLOJIA NCHINI Tanzania na Rwanda zakubaliana kukuza TEHAMA Matumizi ya Teknlojia 2020 na kuongezeka kwa mapato ya Serikali JMAT Pwani wapiga ndege watatu kwa jiwe moja DR SLAA ADAI KUWEKEWA BUGGING DEVICE CHUMBANI JE SIASA ZA TANZANIA ZITABADILIKA KUFUATIA KURUHUSIWA MIKUTANO YA HADHARA YA KISIASA JE ACT-WAZALENDO KINAWEZA KUA CHAMA KIKUU CHA UPINZANI TANZANIA KUREJEA KWA WANASIASA WA UPINZANI NI MWANZO WA SIASA MPYA TANZANIA MFAHAMU SPIKA MPYA WA BUNGE LA TANZANIA TULIA ACKSON RIPOTI YA CAG INAELEZA NINI KUHUSU UTAWALA WA SAMIA SULUHU FREEMAN MBOYE NINI MAANA YA KUACHIWA UONGOZI WA KAMBI YA UPINZANI Ijue Sheria Na Haki Zako May 10,2020 Kudhibiti magonjwa na wadudu wa maharage Mahakama ya Tanzania kuendelea kukaza uzi matumizi ya Tehama Mafanikio makubwa yapatikana mahakama ya Rufani ikitekeleza wajibu wa kikatiba Mahakama mkoani Pwani kuanza wiki ya sheria kiaina Wanachi wajitokeza kwa wingi uzinduzi wa wiki ya sheria nchini Majaji mahakama ya Rufani wanachapa kazi Mtazamo hasi rushwa mahakamani waporomoka SHERIA ZA TANZANIA Kuhamia teknolojia ya digitali Kenya bado Changamoto Majaliwa 'awabana' mawaziri kuhusu kilimo MFAHAMU AUGUSTINE MREMA MWAMBA WA SIASA ZA TANZANIA NANI KUCHEKA KULIA UPEPO MKALI WA RAIS SAMIA SULUHU Mahakama kanda ya Musoma yafanya kikao cha menejimenti KATIBA MPYA Maamuzi ya KAMATI KUU YA CHADEMA TAMISEMI yatoa taarifa nzito kuhusu wanafunzi waliofaulu masomo ya sayansi Utawala Unaanguka Slaa: Chenge hatoki ufisadi wa rada Elimu tulioipata itaondoa migogoro ya mirathi Juhudi za Tanzania kupunguza vifo vya watoto zakabiliwa na changamoto Lengo la milenia la kutokomeza maradhi bado ni changamoto nchini Tanzania HISIA ZA VYAMA VYA SIASA KUHUSU DEMOKRASIA YA NCHI Teknolojia Mpya Ya Kununua Gesi Ya Kupikia Kwa Kutumia Simu Ya Mkononi OCT 20, 2022 Pepo ya Mabwege Tanzania yang’ara ubunifu wa kiuchumi duniani Serikali imetaja sababu kukwama kwa kilimo Bunge lataka Watanzania kunufaika na azimio la kilimo Chadema yaibwaga CCM kuhusu posho JK aunga mkono Dowans isilipwe Uviko ulivyoathiri kilimo cha umwagiliaji Ziwa Victoria KESI YA ALIYETOROKA NCHINI KWENDA KUISHI DUBAI YAKWAMA TENA Wizara ya Kilimo yaanza kutekeleza agizo la Majaliwa TANZANIA KUINGIA KWENYE UCHUMI WA KATI NI MATOKEO YA USIMAMIZI MZURI WA SERA ZA UCHUMI-KASSIM MAJALIWA UONGOZI WA MKOA WA DODOMA NA BENKI YA MAENDELEO YA KILIMO WAKUBALIANA KUBORESHA UWANJA WA NANE NANE NZUGUNI NA KUWEZESHA SHUGHULI Kilimo Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika Idara ya Kilimo Uwekezaji wa kilimo kilimo cha chikichi Kigoma Tanzania: Hali ya Uoga, Udhibiti kadri ukandamizaji unavyoongezeka SHERIA ZA HABARI ZA NCHINI TANZANIA HUDUMA YA KWANZA KATIKA KUTIBU JERAHA ZA KUUNGUA KUTATHMINI USHAHIDI: MABADILIKO YA TABIA YA NCHI NA UHAMIAJI KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Wanafunzi Wa Tanzania Wingia Kwenye Mashindano Ya TEHAMA Yaliyoandaliwa Na Huawei Haki ya Kupata Ujira wa Haki Ujamaa Binadamu na Maendeleo Tanu na Raia Azimio la Arusha Baada ya Miaka Kumi MBOWE NA WENZAKE WANA KESI YA KUJIBU Uchumi unakua kwa kasi – Benki Kuu CHANGAMOTO KWA VYUO VIKUU KUTOA KIPAUMBELE MAFUNZO YA MAZINGIRA,KUTUMIA MTAALA ENDELEVU Taarifa kwa Vyombo vya Habari Kuhusu ya Hali ya Uchumi wa Taifa Katika Mwaka 2019 na Tathimini ya Awali ya Utekelezaji wa Bajeti k SOMO LA UCHUMI Bajeti ya serikali 2017/2018 kuwa Trillion 31.6 Mar 28, 2017 Kikwete ajiuzulu Serikali kutenga bajeti ya Kilimo HOTUBA YA LOWASSA Monduli! CHADEMA YATOA SALAAM ZA RAMBIRAMBI KWENYE JANGA LA MAFURIKO RIPOTI YA MAZINGIRA 2003 JINSI YA KU-BLOCK EMAIL USIZOZITAKA Sayansi na Teknolojia ya Kesho duniani Kawunju Mkunaardhi Mawaziri wa JK tumbo moto Chama cha CCJ kumshitaki msajili wa vyama Tanzania El Niño Ni Nini MWAKA 2008 ULIKUA NI MWAKA WENYE JOTO ZAIDI TANGU 1850 KILIMO CHA MMEA WA MBONO KUHIFADHI ARDHI NA KAMA ZAO LA BIASHARA Imetayarishwa December 2000 Waziri wa Tehama atoa maagizo matatu TTCL Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia kwa Tanzania Posho kumfukuza Shibuda Chadema Athari au Madhara ya Intaneti Unayopaswa Kuyafahamu SHERIA ZA SERIKALI ZA MTAA 11 Februari, 2019 JAJI MKUU AZINDUA MAJUZUU YA TAARIFA ZA SHERIA TANZANIA Ufugaji bora wa kuku wa kienyeji SUA yawa ya Kwanza kugundua chanjo ya ugonjwa wa ndui duniani Jinsi ya kulima uyoga na kuongeza kipato cha ziada Faida za Sayansi na Teknolojia ni zipi? MIAKA SABA YA UTEKELEZAJI WA SERIKALI MTANDAO TAASISI YENYE VIWANGO VYA UBORA VYA ISO 9001:2008 Jarida la kila robo mwaka la Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ISSN: 0856 - 803 TO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA IMETHIBITISHWA NA ISO 9001:2015 UAMUZI NA.6 WA GHARAMA ZA MWINGILI GILLY BONNY ONLINE TV UAMUZI WA KAMATI YA MAUDHUI KUHUSU TUHUMA YA UKIUKAJI WA KANUNI ZA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA (MA UAMUZI UAMUZI WA KAMATI YA MAUDHUI KUHUSU TUHUMA YA UKIUKAJI WA KANUN? ZA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA (MAUDHUI YA MITAND IKISIRI YA SHERIA SHERIA NDOGO ZA (KILIMO CHA KOROSHO) ZA TUME YA MANISPAA YA KINONDONI SHERIA NDOGO ZA ELIMU (MAHUDHURIO YA LAZIMA) ZA TUME YA MANISPAA YA KINONDONI 2000 JE TANZANIA KUTEGUA KITENDAWILI CHA TUME HURU YA UCHAGUZI MIAKA 60 YA UHURU MCHANGO WA VYAMA VYA UPINZANI KATIKA SIASA TANZANIA JE MATAMSHI YA WAZIRI SIMBACHAWENE KUDHIBITI MATUMIZI YA MITANDAO HUENDA YAKADUMAZA UHURU WA MAONI MAJIBIZANO YA SPIKA NDUGAI NA RAIS SAMIA NA FUKUTO LA SIASA 2022 NA 2025 UPI MUSTAKABALI WA UHUSIANO WA MASHAKA KATI YA MSAJILI , VYAMA VYA SIASA NA POLISI Wabunifu wa sayansi, teknolojia watamaliza tatizo la ajira nchini Lwidiko MWONGOZO WA UENDESHAJI WA TOVUTI ZA SERIKALI WAZIRI UMMY:HAKUNA MGONJWA ALIYETHIBITISHWA KUWA NA EBOLA NCHINI CHADEMA YAMTANGAZA RASMI DK. SLAA MGOMBEA WAKE WA URAIS ATHARI YA UTANDAWAZI NA SIASA YA TANZANIA NA MAENDELEO YAKE (SEHEMU YA KWANZA) Kuelekea Katiba Mpya Spika Makinda akutana na BAKWATA Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imemaliza kikao chake Airtel na DTBi Watoa mafunzo ya Tehama kwa walimu wa shule za Msingi na Sekondari Teknolojia ilivyomuumbua huyu mwizi MAZINGIRA NI KITOVU CHA MAENDELEO TANZANIA Kilimo bora cha mtama Fahamu Kilimo Cha Matango Mboga mboga na matunda Wadudu na Magonjwa ya Mihogo Mazao ya Mizizi Mwongozo kwa wakulima kwa wadudu waharibifu na magonjwa ya zao la viazi vitamu CHINA ILIVOSHAWISHI SIASA ZA TANZANIA JINA LA NYERERE LILIVYOJENGEKA NA SIASA ZA TANZANIA Nyota ya Rehema IJUE SHERIA YA VYAMA VYA SIASA NA KANUNI ZAKE Shule 10 sekondari halmashauri ya Arusha zinafundisha somo la TEHAMA MTANZANIA MVUA ZA EL NINO 2023 JE, TUDAI KATIBA MPYA AU TUJIANDAE NA UCHAGUZI WA MWAKA 2020?- 2 Maalim Seif kuvuka au kukwama 2020? Maridhiano Serikali, Chadema ni mwanzo mzuri wa siasa safi Misimamo ya baadhi ya wasomi wetu tahayuri kwa Taifa Prof. Nombo: Wabunifu 283 kuendelezwa na serikali kupitia COSTECH TAMWA-ZNZ yataka mabadiliko ya haraka sheria ya habari Kosa la Bwana Msa Siri ya Sifuri Ufisadi wafumuliwa upya tume ya taifa a taifa ya sayansi na teknolojia yatoa tuzo za ugunduzi na ubunifu na kutoa Mwega kwa ajili ya utafiti mwaka 2010, l TAKRIBANI WANAWAKE MILIONI 650 WALIO HAI WALIOLEWA KABLA YA MIAKA 18 UGAIDI Tanzania Hatuna Serikali! UBIA wa CCM NA BAKWATA Utawaumiza Waislam! KIKWETE Kupingwa kwa MAANDAMANO MAREKANI Sherehe Za UHURU Miaka 50 Zitagharim Shilingi Ngapi UDA KUCHUNGUZWA NA BUNGE Tanzania Inahitaji MAPINDUZI pia CCM Inaibomoa Tanzania MAUAJI IGUNGA: Taarifa ya CHADEMA UDHAIFU WA CHADEMA BUNGENI: Tamko la MNYIKA dhidi NAIBU SPIKA KATIBA MPYA Tamko la TUNDU LISSU 'KATIBA MPYA' Tamko la TUNDU LISSU BUNGE Hotuba ya Halima MDEE Wizara ya ARDHI KIKWETE Ang'olewe Uenyekiti CCM! TANESCO Walimuhujumu Lowassa? JAIRO Apokelewa kwa Shangwe Wizarani MAANDAMANO Kupinga Serikali/DOWANS DOWANS: Kamanda KOVA Anasikitisha na Anashangaza KIKWETE IKULU INAPWAYA! Polisi Inatumiwa Kisiasa LEMA (Mb) Aenda Jela MKUTANO WA AFYA YA JAMII Teknolojia ya kisasa AFYA YA BINADAMU Ahadi ya Serikali kwa wakulima wa ndizi MWAKA WA KILIO CHA MASOKO KWA WAKULIMA IPTL YAGONGA MWAMBA KESI KUPINGA MAAZIMIO YA BUNGE MATUMAINI KATIBA MPYA ARIJOJO IPTL YAZUA KIZAAZAA MAHAKAMANI RAIA WA CHINA WAKANA KUHONGA POLISI MAMILIONI SERIKALI YAPINGA KORTINI BUNGE LA KATIBA KUSIMAMISHWA SHERIA KUBADILISHA MFUMO WA ELIMU YA MSINGI MASAJU AAPISHWA KUWA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI (AG) HATIMA YA BUNGE LA KATIBA KUJULIKANA SEPT 15 ZITTO AIBUKA KIDEDEA MAHAKAMANI SHERIA YA MTANDAO IMEPUNGUZA UHALIFU MGOGORO BUNGE MAALUMU LA KATIBA PINDA TUMERUDISHA MAHAKAMA YA KADHI ILI IJADILIWE ZAIDI WASHTAKIWA WA UGAIDI WAPANGIWA HAKIMU MWINGINE KATIBA NA SUALA LA ARDHI, MALIASILI, GESI NA MAFUTA KASORO TISA ZILIZOTIBUA KUUNDA KATIBA MPYA MAHAKAMANI KWA KUGHUSHI TOVUTI FEKI NA KUTUMIA MAJINA YA TAASISI NA WANASIASA MCHAKATO WA KATIBA MPYA: MDEE NA WENZAKE HURU, POLISI WAWAKAMATA TENA TISA KIZIMBANI KWA UWINDAJI HARAMU BUNGE LA KATIBA NI SUKARI, SHUBIRI KESI YAFUNGULIWA BUNGE LA KATIBA, KESI YA KUHOJI UHALALI WAKE YAFUNGULIWA VIGOGO 11 WA TRL KORTINI KWA UBADHIRIFU MCHINA WA MENO YA TEMBO AKOSA DHAMANA SAKATA LA ESCROW: VIGOGO WA BOT, TRA, TANESCO WAPANDISHWA KIZIMBANI SHAHIDI AELEZA ALIVYOSAFIRISHA VIELELEZO KUTOKA ENEO LA TUKIO TUKITAKA KATIBA MPYA NZURI, TUFANYE MAMBO KWA MUWALA TUKITAKA KATIBA MPYA NZURI, TUFANYE MAMBO KWA MUWALA , Februari 18, 2015 WASHTAKIWA HAO KUTOKA TRA, TANESCO NA BOT WALISOMEWA MAHAKAMA YAFUTA KESI YA DC DHIDI YA KAFULILA MABADILIKO YA KATIBA MUSWADA KUPINGA USHOGA WANAIMBA AMANI, UHURU NA HAKI LAKINI EMMANUEL MBASHA AACHIWA HURU KESI YA HALIMA MDEE YAPIGWA KALENDA SERIKALI YAHOFIA KUPOTEZA SH5.1 BILIONI KWA USIMAMIZI MBOVU WA SHERIA, KANUNI WAFANYABIASHARA MAZAO YA MISITU LINDI WALALAMA HOJA YA KUIKATAA KATIBA INAYOPENDEKEZWA HAINA MASHIKO UCHAMBUZI WA BAJETI MISWADA MIWILI YA HABARI KUWASILISHWA ‘KIMAFIA’ BUNGENI KESI MAUAJI YA BARLOW SABABU ZA KUSEMA HAPANA KWA KATIBA INAYOPENDEKEZWA MAHAKAMA YAJIVUA MIPAKA YA BUNGE BUNGE LAPITISHA MUSWADA, SASA WAANDISHI KUFUNGWA JELA IKIWA KESI YA KUPINGA BUNGE LA KATIBA YAPANGIWA MAJAJI WATATU SERIKALI YAICHOMOA MISWADA YA HABARI MATUKIO YA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI YAZIDI KUKITHIRI NCHINI MUSWADA WA VAT WAONGEZA MUDA WA BUNGE JK, UKAWA LEO, MAKANISA YAONYA HAKIMU AJITOA KESI YA JUMUIYA YA UAMSHO SERIKALI YAIKABA KOO IPTL MAHAKAMANI BUNGE LA KATIBA LAPINGWA MWALIMU ATOZWA SH800,000 KWA UTUMISHI HEWA IKULU YAMJIBU WARIOBA, WAJUMBE WALALAMIKA SHAHIDI WA TATU KESI YA PONDA ATOA USHAHIDI MAHAKAMA YA KADHI BADO ‘PASUA KICHWA’ KORTI YAIZUIA CHADEMA KUMJADILI ZITTO RAIS KIKWETE ATEUA WAKUU WA MIKOA WAPYA Magufuli amechora mstari sahihi wa kumpima 2020 Majibu ya Serikali ya Tanzania kuhusu wanafunzi na siasa vyuoni Miaka 50 ya Uhuru Majaliwa awataka MaDC kuwaeleza wakulima kilimo kitakavyowanufaisha SHERIA IWASHUGHULIKIE WALIOTAJWA NA CAG NDAMA MTOTO WA NG’OMBE’ KORTINI KIKWETE NA KAGAME WAPUMUA KIDOGO Wadau waelezwa jinsi Tehama inavyoweza kukuza uchumi Tanzania Waziri Mkuu Majaliwa asisitiza umuhimu wa mifumo ya usalama kwenye miji kupitia TEHAMA Sheria na kanuni za sekta mawasiliano kupitiwa MAREKEBISHO YA SHERIA YA NDOA MAHAKAMA YAKUBALI PINGAMIZI UTETEZI KESI YA SABAYA Zanzibar mbioni kuzifanyia marekebisho sheria zinazolalamikiwa na wadau wa habari ripoti zamdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za fedha 2019.2020. UKAGUZI WA MIFUMO YA TEHAMA Kitabu cha Uchumi 2017 Kitabu cha Uchumi 2018 Filamu ya Malawi yawasaidia wakulima kujikinga na mabadiliko ya tabia nchi Jinsi NEC ilivyoanzishwa Historia ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi KUASISIWA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI Mwaka 1991 EU, Marekani wajitosa mgogoro wa Katiba Chadema, NCCR Mageuzi wachafua hali hewa bungeni Zitto avuliwa madaraka Bosi COSTECH: Miaka miwili kiserikali, tunaneemeka kwa teknolojia 31 Mar 2023 Kujiunga na mfuko wa afya ya Jamii (CHF) Halmashauri ya Wilaya ya Njombe RAIS SAMIA KUFANYA MABADILOKO KWENYE ELIMU POLISI Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais Mwaka 2016/2017 Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais mwak 2018/2019 Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais Mwaka 2019/2020 Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais ZIARA YA KATIBU MKUU MBARALI YATOA SURA MPYA KWA SEKTA YA MAZINGIRA. Uchumi wa Bahari kuzingatia hifadhi ya mazingira Serikali yawasilisha muswada wa marekebisho ya sheria mbalimbali OMMS yasaini makubalian na taasisi ya LAWS.AFRICA Uchumi na Uzalishaji Baraza la Madiwani la pitisha Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 Wamiliki wa biashara za vileo watakiwa kuzingatia sheria na kanuni za uendeshaji biashara MPANGO WA KUDHIBITI UKIMWI WA MWAKA (2008-2012) Bajeti ya ofisi ya waziri mkuu 2022/23 Bajeti ya ofisi ya waziri mkuu mwaka 2017/18 Bajeti ya ofisi ya waziri mkuu mwaka 2019/20 Bajeti ya ofisi ya waziri mkuu 2020/21 Bajeti ya ofisi ya waziri mkuu 2016/17 Nyenzo 6: Barafu ya mlima Kilimanjaro TUME YA TAIFA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA YATOA TUZO LEO. Tanzania Maandamano ya chama cha Chadema mjini Arusha JUHUDI ZA KUHIFADHI MAZINGIRA Rais Mstaafu Ben William Mkapa: 1938-2020: Ukweli na Uwazi!Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamini William Mkapa alizaliwa tarehe Maonesho ya 3 ya mwaka ya AT EXPO yaahirishwa Kikwete abariki nyongeza ya mishahara MAPENDEKEZO KWA AJILI YA KATIBA MPYA YALIYOTOLEWA NA WANACHAMA WA POLICY FORUM UTANGULIZI MISINGI YA KATIBA Uwepo wa sheria ya uteketaji itamaliza ukatili huo nchini Benki ya Dunia yajipanga kukuza uchumi wa Tanzania na kupunguza umasikini 04 Desemba, 2017 Moto wawaka Chadema CAG ampa Tendwa miezi sita ruzuku vyama vya siasa Je, muswada wa mabadiliko ya sheria ya habari umeondoa kero zote Tanzania? KUREJEA KWA TUNDU LISSU NA USHAWISHI WAKE KUTASAIDIA VIPI CHADEMA MABADILIKO YA BARAZA LA MAWAZIRI YANA MAANA GANI KWA UONGOZI WA RAISI SAMIA MASUALA GANI YATAJADILIWA BAINA YA RAIS SAMIA NA WAPINZANI TANZANIA DR ALI MWINYI YAPI MAFANIKIO NA CHANGAMOTO ZA MWAKA MMOJA WA UTAWALA WA ZANZIBAR SIASA ZA TANZANIA KWANINI UHUSIANO WA SERIKALI NA UPINZANI UNAZOROTA JE WANAOMPINGA RAIS SAMIA KUJITOKEZA KUGOMBEA MWAKA 2025 TEKNOLOJIA MPYA NA UWAKILISHI WA AFRIKA KWENYE CEBIT 2005 Biashara, Maji na Krismasi UTUNZAJI BORA WA TAKA NGUMU MAJUMBANI UNA FAIDA ZAKE Asali Chungu Dunia Mti Mkavu Kiza katika Nuru Nyuso za Mwanamke Babu Alipofufuka CUF kukabidhi rasimu ya katiba kwa maandamano KUONDOA MARUFUKU YA UPINZANI KULIVYOMNUFAISHA SAMIA Asali Yenye Shubiri Fahamu kuhusu Baraza la Ushauri la watumiaji wa Huduma za Mawasiliano (TCRA-CCC) Mzalendo HOTUBA YA RAIS WA ZANZIBAR DR HUSSEIN MWINYI KWENYE WIKI YA SHERIA Kufikirika Kusadikika Siku ya Watenzi Wote Wasifu wa Siti Binti Saad Adili na Nduguze Utubora Mkulima Masomo Yenye Adili Mbali na Nyumbani Kuli Vuta ni Kuvute Kasri ya Mwinyi Fuadi Haini Mtoto wa Mama Tunza Jamii Yako, Tunza Mazingira Yako kwa Maisha Bora Kilimo cha alizeti sasa kwa mkataba Wizara kilimo, JKT kushirikiana kwenye kilimo Vyuo vya ualimu vyaagizwa kutumia Tehama kufundisha Sheria kiganjani Ujumbe wa mgeni rasmi, Mh. William Lukuvi katika maadhimisho ya watu wenye ukemavu Uchumi wa Tanzania kukua kwa asilimia 5.5 mwaka 2020 Kiswahili katika Kufundishia TEHAMA katika Shule za Msingi nchini Tanzania: Umuhimu na Changamoto zake Kiswahili katika Kufundishia TEHAMA katika Shule za Msingi nchini Tanzania Muhogo zao linaoongoza kulimwa ukanda wa jangwa la Sahara Dk Slaa, Lissu mbaroni UTEKELEZAJI WA SERIKALI MTANDAO NCHINI Serikali za Tanzania, Kenya na Uganda zawasilisha bajeti kuu MAFUNZO YA MFUMO WA MASOKO KILIMO BIASHARA NA KANUNI ZA KILIMO BORA CHA MSETO WA MBAAZI Sekta ya kilimo Dk Mahera awafunda watendaji sekta ya afya Tanga SURA YA 16 KANUNI YA ADHABU SHERIA KUU Mr. ALI HASSAN MWINYI Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mheshimiwa Alhaj Ali Hassan Mwinyi aliyeongoza Serekali ya Awamu ya Pili alii Tanzania ni miongoni mwa nchi 10 za Afrika zinazokua kwa kasi kiuchumi MAZINGIRA MAZOEZI NA AFYA ZETU IJUE NAFASI YA MAJI KATIKA MWILI WAKO TAMBUA MADHARA YA MALARIA CHUMVI FAIDA NA MADHARA YAKE VITU VYA KUZINGATIA ILI KUWA NA AFYA NJEMA USAFI WA MAZINGIRA KATIKA SEKTA YA CHAKULA USAFI WA MAZINGIRA KATIKA AFYA USAFI WA MAZINGIRA UKUSANYAJI WA MAJI MACHAFU KATIKA MAZINGIRA TEKNOHAMA KICHOCHEO CHA MAENDELEO NCHINI KILIMO BORA CHA MBONO IJUE AFYA YAKO Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Nyerere Katika Mto Rufiji (Stiegler’s Gorge) MBEGU BORA ZA MAHARAGE MAJI MOTO-RAFIKI WA MKULIMA MIHOGO NJIA BORA ZA UKAUSHAJI NA USINDIKAJI TANGAWIZI UTANGULIZI MIGOMBA KANUNI ZA KILIMO BORA ALOE VERA - KINGA YA MALARIA KILIMO KWANZA AZIMIO LA KILIMO KWANZA KWA KUWA VITUNGUU NAZI MNAZI SAYANSI NA TEKNOLOJIA MPYA (25) SHIRIKA LA AFYA MUHIMBILI Mambo Muhimu katika Mabadiliko ya Shirika la Afya Muhimbili UHABA WA MADAWA TANZANIA Kuishi Muda Mrefu Ukiwa na Afya Bora Tume ya kurekebisha sheria Tanzania yafanya kongamano la Tathmini ya utekelezaji wa sheria za makosa dhidi ya maadili Tanzania Tume imeanza kufanya utafiti na tathmini ya sheria za makosa dhidi ya maadili Tathmini ifanyike kwa sheria zinazosimamia makosa ya maadili NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA AFANYA ZIARA KATIKA OFISI ZA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA Makamu wa Rais aitaka tume yakurekebisha sheria nchini kufikisha elimu ya sheria vijijini ili kupunguza migogoro ya ardhi Ukusanyaji maoni kwa ajili ya maandalizi ya mpango wa mapitio ya sheria mbalimbali Tume za kurekebisha sheria Tanzania na Zanzibar zimesaini mkataba wa ushirikiano Uinjilisti kwa kusaidiwa na TEHAMA Faida na Hasara zake tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 tz-government-gazette-dated-2021 Dhamira ya dhati ya Marekani na ubia wake usioyumba na Tanzania UMUHIMU WA KUANDAA MPANGO WA BIASHARA KATIKA KUJENGA BIASHARA IMARA UTUNZAJI NA UDHIBITI WA FEDHA KATIKA BIASHARA 09/08/2017 DR Slaa Aibuka...Afikiria Kurudi Tanzania...Adai Watanzania Wamvumilie Rais Magufuli MAKALA: Kinachompa Membe Ujasiri, ‘JEURI’ Mbele ya Wembe Unaokata, ‘Siri ni Silaha?’ Wakati Tanzania Bara Wakisoma Bajeti ya Trilioni 31 13 juni 2017 Wakati Tanzania Bara Wakisoma Bajeti ya Trilioni 31,Zanzibara Wasoma Bajeti Yao ya Trilioni 1.8..!!! June 13, 2017 BOT Yaeleza Kuwa Tanzania Miongoni mwa Nchi za Afrika Ambazo Uchumi Wake Unaokua kwa Kasi November 21, 2017 Halipendwi Shirika Hapa Pesa Kwanza- Rais JPM July 23, 2018 Bajeti Kuu ya Serikali 2017/18 June 09, 2017 Tanzania Kinara wa Utawala Bora Afrika Mashariki February 07, 2018 Usawa katika elimu, sayansi na teknolojia ni daraja la ajira bora kwa wanawake _ Habari za UN Nchi za Afrika zapokea mitaji mingi isiyo rasmi kuliko ilivyodhaniwa- IMF Sera makini kunusuru biashara duniani mwaka 2017/2018 Mwaka 2014 umewezesha kutambuliwa kwa umuhimu wa kilimo cha kaya Pambaneni na magonjwa ya kilimo na mifugo Miaka 100 ya kristalografia imeleta maendeleo ya sayansi Mahakama kuu Tanzania katika kuimarisha haki sasa 'kuziba nyufa, badala ya kujenga ukuta' TUKISHIRIKIANA BEGA KWA BEGA TUTAFIKIA MALENGO YA MILENIA TANZANIA: PINDA Wanawake Tanzania wainua vipato vyao kwa kutumia teknolojia Teknolojia ya kisasa kurahisisha ukusanyaji wa takwimu: Tanzania Teknolojia duni yadhoofisha uwezo wa ukuaji Afrika Vichocheo vya uchumi vyahitajika kukwamua maskini Tanzania 11 Aprili 2017 Vichocheo vya uchumi vyahitajika kukwamua maskini Tanzan MIRADI YA UNDP EQUATOR Kilimo bora ni mustakhabali wa kilimo barani Afrika NI NAMNA GANI WANAWAKE NA VIJANA WENYE ULEMAVU WANAWEZA KUFIKIA HAKI ZA KIJINSIA NA AFYA YA UZAZI NA HAKI ZAO ZA KUISHI MAISHA YAL NI NAMNA GANI WANAWAKE NA VIJANA WENYE ULEMAVU WANAWEZA KUFIKIA HAKI ZA KIJINSIA NA AFYA YA UZAZI NA HAKI ZAO ZA KUISHI MAISHA YAL UNIFEM kuwatayarisha wagombea wanawake kuelekea uchaguzi mkuu wa Tanzania MKAKATI WA NCHI WA USHIRIKIANO WA KIMAENDELEO 2020 – 2025 Utandawazi na maendeleo ya sayansi na teknolojia ni changamoto ya kuwasaidia maskini kupambana na mazingira yao HALI YA UZALISHAJI WA MAZAO YA CHAKULA Mahakama Tanzania yataka marekebisho ya sheria ya ndoa CHADEMA kuanza tena maandamano Chama kipya cha kisiasa chaundwa Tanzania. Athari tano za kiuchumi zinazoweza kutokea baada ya kuongezeka kwa tozo za miamala ya simu Tanzania Njama za Vigogo MABADILIKO YA SHERIA YA NDOA SURA YA 29 BInadamu na mazingira Elimu ya sheria itumike kupunguza ukatili kwenye ndoa SERA YA AFYA YA MWAKA 2007 Afya Ukamilifu wa binadamu kimwili bunge mazingira Ebola Halmashauri Wilaya Ya Kakonko Halmashauri ya Mji wa Mafinga Hati Rasmi (Uanzishaji wa Bodi ya Huduma za Afya) za Halmashauri Wilaya Ya Kakonko huduma za afya na ustawi wa jamii Madaktari wa Tanzania mwenendo wa matokeo mazuri ya afya Sheria Ndogo za (Afya Na Usafi wa Mazingira) wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida Sheria Ndogo Za (Afya Na Usafi wa Mazingira) Za Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Sheria Ndogo za (Uanzishaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii ) za Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Sheria Ndogo za (Uanzishaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii wa Tiba kwa Kadi) za Halmashauri ya Mji wa Mafinga Sheria Ndogo Za (Uanzishaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii ya) Za Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI nchini Tanzania Uzazi wa mpango TANZANIA NA UKIMWI Kijitabu hiki, kinachotoa muhtasari wa matokeo muhimu ya Ukimwi HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA , KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA AFYA KWA MWAKA 2022/2 BAJETI YA WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, MWAKA 2020/21 HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA, USTAWI WA JAMII, WAZEE, JINSIA NA WATOTO MHESHIMIWA KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA BAJETI YA WAZIRI WA AFYA MWAKA 2018/19 Hotuba ya bajeti ya wizra ya afya kwa mwaka 2016/17 Hotuba ya bajeti ya wizara ya afya kwa mwaka 2017/187 Hotuba ya bajeti ya wizara ya afya kwa mwaka 2018/19 Hotuba ya bajeti ya wizara ya afya kwa mwaka 2022/23 Hotuba ya bajeti ya wizara ya afya kwa mwaka 2020/21 Hotuba ya bajeti ya wizara ya afya kwa mwaka 2021/22 Zanzibar Hotuba ya bajeti ya wizara ya afya kwa mwaka 2018/19 Zanzibar hotuba ya wizara ya ardhi ya mwaka 2022/2023 hotuba ya wizara ya ardhi ya mwaka 2020/2021 hotuba ya wizara ya ardhi ya mwaka 2018/2019 hotuba ya wizara ya ardhi ya mwaka 2016/2017 hotuba ya wizara ya ardhi ya mwaka 2015/2016 hotuba ya wizara ya ardhi ya mwaka 2017/2018 SHERIA ZINAZOHUSU MASUALA YA ARDHI NA JINSIA TANZANIA SHERIA ZA ARDHI NA JINSIA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO KWA MWAKA WA FEDHA 2018/19. HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO KWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020. HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2020/2021. HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022. HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023. HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI MHESHIMIWA DKT. SHUKURU JUMANNE KAWAMBWA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZ HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI MHESHIMIWA PROF. JOYCE LAZARO NDALICHAKO (MB.) AKIWASILISHA BUNGENI MAKAD HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA MHESHIMIWA PROF. JOYCE LAZARO NDALICHAKO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA MHESHIMIWA PROF. JOYCE LAZARO NDALICHAKO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA MHESHIMIWA PROF. JOYCE LAZARO NDALICHAKO (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA M HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA MHESHIMIWA PROF. JOYCE LAZARO NDALICHAKO (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA M HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA MHESHIMIWA PROF. JOYCE LAZARO NDALICHAKO (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA M HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA PROF. ADOLF FAUSTINE MKENDA (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MAT Matumizi ya teknolojia teknolojia sayansi na teknolojia Kiswahili katika Kufundishia TEHAMA uelekeo wa dunia Matumizi ya Lughatandawazi Vijana kujiandikisha masomo ya Tehama yanayotolewa na Airtel COSTECH kukabidhi bil. 568 kwa vijana wabunifu Habari Mawasiliano na Tehama Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Bunge lapitisha muswada wa marekebisho sheria ya PPP Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango ya Mwaka 2022/2023 Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango Mwaka 2020/2021 Hotuba ya Bajeti ya wizara ya Fedha na Mipango Mwaka 2021/2022 Hotuba ya Bajeti ya wizara ya Fedha na Uchumi mwaka 2010/2011 BENKI YA DUNIA YAIMWAGIA SIFA TANZANIA KWA UCHUMI IMARA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO BAJETI YA SERIKALI YA MWAKA WA FEDHA 2019/20 Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuh MATUKIO MUHIMU YA KIUCHUMI KWA MWAKA 2020 Serikali ya Tanzania yatamba ukuaji wa uchumi na pato la taifa Uchumi wa Tanzania kukua kwa asilimia 4 mwaka 2020 TAARIFA YA HALI YA UCHUMI WA TAIFA KWA MWAKA 2020 NA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA WA MWAKA 2021/22 Taarifa Ya Hali Ya Uchumi Wa Taifa Kwa Mwaka 2019 Na Mpango Wa Maendeleo Wa Taifa Wa Mwaka 2020/21 Wawasilishwa Bungeni Taarifa Ya Hali Ya Uchumi Wa Taifa Kwa Mwaka 2019 Na Mpango Wa Maendeleo Wa Taifa Wa Mwaka 2020/21 Wawasilishwa Bungeni. Hotuba ya bajeti ya Wizara ya Habara, Sanaa, Michezo na Utamaduni Mwaka 2016/2017 Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Habara, Sanaa, Michezo na Utamaduni Mwaka 2017/2018 Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Habara, Sanaa, Michezo na Utamaduni Mwaka 2019/2020 Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Habara, Sanaa, Michezo na Utamaduni Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Habara, Sanaa, Michezo na Utamaduni Mwaka 2022/2023 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu hotuba ya wizara ya habari na mawasiliano ya mwaka 2022/2023 hotuba ya wizara ya habari na mawasiliano mwaka 2021/2022 TEHAMA Kitengo Cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Uchumi wa Tanzania Kuendelea Kupaa katika kipindi kifupi kijacho- IMF Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria Mwaka 2017/2018 Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria Mwaka 2014/2015 Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria Mwaka 2018/2019 Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria Mwaka 2021/2022 Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria adhabu ya kifo ARDHI na umuhimu wake katika maisha ya binadamu haki sawa katika mambo ambayo mila na desturi haki za mtoto kosa dhidi ya Sheria kuharibu na kuchafua mahali popote pa kuabudia ruhusa ya Rais sheria ya ndoa Sheria ya Tawala za Mikoa ya Mwaka 1997 talaka tatu za Sheria za Mirathi kama zinavyotumika hapa Tanzania TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA utumishi wa umma KANUNI ZA MSAADA WA KISHERIA WA MWAKA 2020 Muhtasari Wizara ya Katiba na Sheria ndiyo mhimili mkuu wa masuala yote ya kisheria nchini. Tangazo kwa umma Historia ya Wizara Wizara ya Katiba na Sheria ndiyo mhimili mkuu wa masuala yote ya kisheria nchini HAKI ZA BINADAMU HAKI ZA WAFANYAKAZI KANUNI ZAMAADILI YAUTENDAJI KATIKAUTUMISHI WA UMMA KANUNI YA ADHABU SHERIA KUU MABADILIKO YA SHERIA MCHAKATO WA KUDAI HAKI KISHERIA UTEKELEZAJI WA SHERIA YA UTUMISHI WA UMMA SURA YA 298 KATIKA USIMAMIZI WA MASUALA YA AJIRA NIDHAMU NA RUFAA Hotuba ya Wizara ya Fedha na Mipango ya Makadirio ya Mapato na matumizi 2006 - 2007 (1) Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na Ushirika Mwaka 1997/98 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na ushirika mwaka 1998/99 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na Ushirika Mwaka 2000/01 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na Chakula Mwaka 2001/02 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na Chakula Mwaka 2002/03 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na Chakula Mwaka 2003/2004 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na Chakula Mwaka 2004/2005 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na Chakula Mwaka 2005/2006 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na Chakula Mwaka 2006/2007 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na Chakula Mwaka 2007/2008 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo na Chakula Mwaka 2008/2009 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Mwaka 2009/2010 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Mwaka 2010,/2011 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Mwaka 2011/2012 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Mwaka 2012/2013 HOTUBA YA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2008/09 ILIYOTOLEWA KATIKA BARAZA LA WAWAKILISHI NA WAZIRI WA KILIMO, Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Mwaka 2013/2014 HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA MAZINGIRA,YA MHE. BURHAN SAADAT HAJI (MBM) KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI NA MAPATO YA FEDHA Y Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Mwaka 2014/2015 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Mwaka 2015/2016 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Mwaka 2016/2017 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo Mwaka 2018/2019 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo Mwaka 2019/2020 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo Mwaka 2020/2021 Hotuba ya Bajeti Wizara ya Kilimo Mwaka 2022/2023 HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA MAZINGIRA,YA MHE. BURHAN SAADAT HAJI (MBM) KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI NA MAPATO YA FEDHA Y HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO NA MALIASILI MHE. MANSOOR YUSSUF HIMID (MBM) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO NA MALIASILI MHE. SULEIMAN OTHMAN NYANGA (MBM) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZAR HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO NA MALIASILI MHE. SULEIMAN OTHMAN NYANGA (MBM) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZAR HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO NA MALIASILI MHE. DKT. SIRA UBWA MAMBOYA (MBM) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZAR HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI MHE. HAMAD RASHID MOHAMED (MBM) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FE Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Kilimo 1995/1996 mazao ya kibayoteki kiutandawazi HISTORIA FUPI YA MKOA WA MTWARA TEKNOLOJIA YA USINDIKAJI NA UHIFADHI WA MAZAO YA NAFAKA HISTORIA YA BODI YA MAZIWA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO NA CHAKULA, MHESHIMIWA CHARLES N. KEENJA (MB.), KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILI TANZANIA INA ZAIDI YA TANI 3,013,515 YA MAZAO YA CHAKULA Uandaaji wa Miradi ya Kilimo cha Umwagiliaji Maji Mashambani Kuzuia Mchwa bila Kemikali Mbegu Mpya za Mazao Mbalimbali Zaidhinishwa Sheria Ndogo za Kilimo Kwanza na Usalama wa Chakula SHERIA YA UVUVIYA MWAKA 2003 SHERIA YA UWAJIBIKAJI WIZARA YA KILIMO NA CHAKULA Taarifa_ya_Mwaka_2007 TAARIFA FUPI YA MATOKEO YA MRADI WA UTAFITI WA PIMA Kilimo cha Basil Kilimo cha Binzari Kilimo cha Dill Kilimo cha Fennel Kilimo cha Pilipilimtama Kilimo cha Rosemary Kilimo cha Soya Kilimo cha Tangawizi Kilimo cha Vanilla Kilimo cha Viazi vitamu Hotuba ya bajeti ya wizara ya madini mwaka 2019/2020 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu utekelezaji wa Majukumu na shughuli za Kamati Taarifa ya utekelezaji wa majukumu na bajeti ya Wizara na Taasisi zake kwa mwaka wa Fedha 2019/2020 Bunge Maalum la Katiba historia ya kisiasa ya Tanzania hotuba ya Kikwete kikao hiki maalum cha Baraza kumkaribisha Tanzania Mheshimiwa Pierre Nkurunziza mafunzo ya uofisa miaka 31 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi migogoro ya kisiasa Siasa za Tanzania vyama vya Tanzania SERA YA TAIFA YA MIFUGO BAJETI YA WIZARA YA MAJI MWAKA 2014/2015 BAJETI YA WIZARA YA MAJI MWAKA 2016/2017 BAJETI YA WIZARA YA MAJI MWAKA 2017/2018 BAJETI YA WIZARA YA MAJI MWAKA 2018/2019 BAJETI YA WIZARA YA MAJI MWAKA 2019/2020 BAJETI YA WIZARA YA MAJI MWAKA 2020/2021 BAJETI YA WIZARA YA MAJI MWAKA 2021/2022 BAJETI YA WIZARA YA MAJI MWAKA 2022/2023 hotuba ya wizara ya maliasili na utalii ya mwaka 2022/2023 hotuba ya wizara ya maliasili na utalii ya mwaka 2021/2022 hotuba ya wizara ya maliasili na utalii ya mwaka 2020/2021 hotuba ya wizara ya maliasili na utalii ya mwaka 2015/2016 hotuba ya wizara ya maliasili na utalii ya mwaka 2014/2015 hotuba ya wizara ya maliasili na utalii ya mwaka 2013/2014 hotuba ya wizara ya maliasili na utalii ya mwaka 2009/2010 hotuba ya wizara ya maliasili na utalii ya mwaka 2008/2009 BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI MWAKA 2017/2018 BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI MWAKA 2018/2019 BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI MWAKA 2020/2021 BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI MWAKA 2022/2023 Bajeti ya wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Africa mashariki kwa mwaka 2020 Bajeti ya wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Africa mashariki kwa mwaka 2022 Bajeti ya wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika kwa mwaka 2022 MIKATABA YA KIMATAIFA TAMKO LA KIMATAIFA LA HAKI ZA BINADAMU UMOJA WA NCHI HURU ZA AFRIKA MAELEZO YA MAFUNZO Hifadhi ya Kasa na Nguva BAJETI YA WIZARA YA MIFUGO MWAKA 2016/2017 BAJETI YA WIZARA YA MIFUGO MWAKA 2019/2020 BAJETI YA WIZARA YA MIFUGO MWAKA 2020/2021 BAJETI YA WIZARA YA MIFUGO MWAKA 2021/2022 BAJETI YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI MWAKA 2022/2023 BAJETI YA KIKAO CHA TATHMINI YA UTENDAJI KAZI WA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI MWAKA 2018/2019 HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI MHE. PROF. SOSPETER MWIJARUBI MUHONGO (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MAT HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE (MB.),AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA M HOTUBA YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2017/2018 HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI MHE. DKT. MEDARD MATOGOLO CHANANJA KALEMANI (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZ HOTUBA YA BAJETI WIZARA YA NISHATI HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI MHE. DKT. MEDARD MATOGOLO CHANANJA KALEMANI (MB.), AKIWASILISHA BUN HOTUBA YA BAJETI WIZARA YA NISHATI HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI MHE. DKT. MEDARD MATOGOLO CHANANJA KALEMANI (MB.), AKIWASILISHA BUN HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI MHESHIMIWA JANUARY YUSUF MAKAMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA utekelezaji wa majukumu na bajeti ya Wizara ya Nishati HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23 HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA KWA MWAKA WA FEDHA 2017/18 HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA KWA MWAKA WA FEDHA 2018/19 BAJETI YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, MWAKA 2021 HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA KUHUSU MAPITIO, MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FE HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA KWA MWAKA WA FEDHA 2016/17 BAJETI YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA, SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ MWAKA 2020/21 BAJETI YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA, SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ MWAKA 2019/20 MISINGI YA SHERIA KATIKA KUSIMAMIA HAKI NA WAJIBU KWA WATUMISHI WA UMMA MWONGOZO WA FEDHA ZA SERIKALI ZA MITAA SHERIA YA AJIRA NA MAHUSIANO KAZINI Jarida la mifumo yetu novemba 2017 januari 2018 HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI, MHESHIMIWA MHANDISI DKT. LEONARD MADARAKA CHAMURIHO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO NA M HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI, MHESHIMIWA PROF. MAKAME MNYAA MBARAWA (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO NA MAKADIRIO YA MA HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO MHESHIMIWA PROF. MAKAME M. MBARAWA (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO NA MAKADI HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO MHESHIMIWA PROF. MAKAME M. MBARAWA (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO NA MAKADI HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO MHESHIMIWA PROF. MAKAME MNYAA MBARAWA (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO NA MAK HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO MHESHIMIWA MHANDISI ISACK ALOYCE KAMWELWE (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO NA HOTUBA YA WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO, MHESHIMIWA ENG. ISACK ALOYCE KAMWELWE (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MPANGO NA MA HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT. HUSSEIN ALI MWINYI (MB.), KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUM HOTUBA YA MHESHIMIWA DKT. STERGOMENA LAWRENCE TAX (MB.), WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO BAJETI YA WAZIRI WA NCHI – OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA MWAKA 2020/21 Bajeti ya wizara ya utumishi wa umma kwa mwaka wa fedha 2018/19 Bajeti ya wizara ya utumishi wa umma kwa mwaka wa fedha 2019/20 Hotuba ya bajeti ya utumishi wa umma na utawala bora kwa mwaka 2022/23 MWONGOZO WA VYAMA VYA WAFANYAKAZI hotuba ya wizara ya viwanda na biashara hotuba ya wizara ya viwanda na biashara ya mwaka 2021/2022 hotuba ya wizara ya viwanda na biashara ya mwaka 2019/2020 hotuba ya wizara ya viwanda na biashara ya mwaka 2017/2018 hotuba ya wizara ya viwanda na biashara ya mwaka 2020/2021 hotuba ya wizara ya viwanda na biashara ya zanzibar ya mwaka 2022/2023 Katiba mpya Tanzania : Maswali 4 mepesi yenye majibu magumu MATOKEO YA UCHAGUZI WA RAIS KUHOJIWA MAHAKAMANI KUNAVYOWEZA KUBADILI SIASA ZA TANZANIA MATUKIO MUHIMU KWENYE KESI YA FREEMAN MBOYE IGP WAMBURA NA MFUPA MGUMU WA KUUTAFUNA KUHUSU POLISI TANZANIA KATIBA MPYA TANZANIA MASWALI MANNE MEPESI YENYE MAJIBU MAGUMU RAIS SAMIA AMALIZ A MARUFUKU YA MIAKA SITA YA MIKUTANO YA VYAMA VYA KISIASA Vijana wakumbatia kilimo Kenya KITABU CHA MABADILIKO YA TABIA NCHI CHAZINDULIWA, SIMBACHAWENE AWAASA WANANCHI KUTUNZA MAZINGIRA Japan kuisaidia Tanzania teknolojia katika ulinzi MATOKEO YA SENSA HALI YA KISIASA YA MUUNGANO Tamko la CHADEMA Juu ya Mauaji ya Wananchi wakati wa Maandamano Arusha Hali ya Uchumi ni Mbaya, Watanzania Wamepoteza Matumaini Tafuta neno Rekebisha .
892d6acb4dad50a924105c86adf809afbde87f973651d89e8a615efedbb213eb
18,140
5.022822
143
91,114
1
0
0
0.027563
8.85
1,196
https://www.nishati.go.tz/news/watu-milioni-300-afrika-kutumia-nishati-safi-ya-kupikia-ifikapo-2030-dkt-biteko
##### WATU MILIONI 300 AFRIKA KUTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA IFIKAPO 2030- DKT. BITEKO **Benki ya Dunia na AfDB zaunga mkono Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia** **Mkutano wa Marais Afrika kufanyika Tanzania; Ajenda ya Nishati Safi kupewa kipaumbele** **Tanzania yawa mfano Afrika mapinduzi Sekta ya Nishati** Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.Dkt. Doto Biteko amesema ifikapo mwaka 2030 watu milioni 300 katika Bara la Afrika watakuwa wanatumia Nishati Safi ya kupikia huku Tanzania ikiwa ni kinara katika kuhamasisha Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia. Amesemajuhudi zinazofanyika katika kufikia lengo hilo zimepelekeaBenki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Benki ya Dunia ( WB) kuunga mkono Ajenda ya Nishati Safi ya kupikia katika bara la Afrika. Biteko amesema hayo wakati akizungumza katika Mkutano wa Jukwaa la Majadiliano kuhusu Masuala ya Nishatikwa Bara la Afrika kwa ngazi ya Mawaziri unaofanyika Jijini Dar es salaam kwa siku mbili ulioandaliwana Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na AfDB. Amesema AfDB imeichangua Tanzania kufanya mkutano huo wa majadiliano kwa kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa kimaendeleo na mafanikio katika Sekta ya Nishati ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika zinazoshirikiana na benki hiyo na imekuwa mfano wa kuigwa na nchi hizo.. Ameeleza kuwa,katika mkutano huo masuala mbalimbali yanajadiliwa huku lengo kubwalikiwa ni kuweka mipango thabiti ya kuhakikisha kuwa watu Milioni 300 katika Bara la Afrika wanatumia nishati safi ya kupikiaifikapo 2030 ikiwa ni miaka 6 kutoka sasa. " Mkutano huu pia ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa Maraiswa nchi za Afrika unaotarajiwa kufanyika mwaka 2025 ikiwa ni mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ndiye kinara wa ajenda ya Nishati safi ya kupikia Afrika." Amesema Dkt. Biteko Amesema Marais hao watakuja nchini kujadili masuala ya nishati katika Bara la Afrika ikiwemo suala lawatu milioni 300 Afrika kutumia nishati safi ya kupikia. Ameongeza kuwa, mkutano huo utafanya tafakuri na utaweka mikakati ya kuhakikisha kuwa nishati safi ya kupikia inapatikana kwa uhakika na gharama nafuu ili kila mwananchi anaweza kuimudu. Amesema mkutano huo ni muhimu kwa Tanzaniahasa kwenye sekta ya nishati kwakuwa imefanya mapinduzi makubwa kwenye nishatina upatikanaji wa umeme nchini ni wa uhakika na miradi mikubwa inayotekelezwa ipo mwishoni na kwamba kazi kubwa iliyopo ni kuhakikisha watu wanapata umeme kila sehemu. “Furaha yetu ni kwamba tumepata heshima kubwa ambayo haikuja hivihivi bali ni kutokana na mahusiano mazuri ya kidiplomasia kati nchi yetu, Benki ya Maendeleo ya Afrika ( AfDB) na Benki ya Dunia na kutokana pia na kupiga hatua katika masuala ya usimamizi mzuri wa kisera, uzalishaji, usafirishaji, usambazaji na upelekaji wa umeme vijijini."Amesema Dkt. Biteko. Amesema Tanzania imepiga hatua katika kupeleka umeme vijijini na ifikapo Desemba tutakuwa tumepeleka umeme katika vijiji vyote zaidi ya 12,000 na kuhamia katika vitongoji vyote. Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Kelvin Kairuki amesema Benki hiyo kwa kushirikiana na Benki ya Dunia itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kufanya kazi pamoja kwa sababu Tanzania iko katika mstari wa mbele katika kutekeleza Ajenda ya Nishati safi ya Kupikia ikilinganishwa na nchi nyingine zinazofanya kazi na benki hizo. Amesemauamuzi wa kuamuamkutano mkubwa wa Marais ufanyike Tanzania ni pamoja nakumuunga mkonoRais Samia katika juhudi za utekelezaji wa Ajenda ya Nishati safi ya kupikia na kuwa kinara wa ajenda hiyo kwa nchi za Afrika. Mkutano huoumehudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba, Kamishna wa Umeme na Nishari Jadidifu Mhandisi Inocent Luoga, Wakuu wa Taasisi zilizochini wa Wizara ya Nishati na wadau wa nishati kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania.
ae6af8afd15db3ab1e87aba1c5d84daf7774d58b06ca8b0de78c1cf93eabbd0e
582
5.589347
21
3,253
1
0
0
0.171821
2.41
79
https://www.nishati.go.tz/news/serikali-yaweka-mkazo-kukuza-tasnia-ya-ufugaji-wa-kuku
##### SERIKALI YAWEKA MKAZO KUKUZA TASNIA YA UFUGAJI WA KUKU **Vijana Wahimizwa Kujiajiri Kupitia Ufugaji Kuku** **Dkt. Biteko Atoa Maagizo kwa Wizara ya Mifugo Kukuza Tasnia ya ufugaji wa Kuku** **Watanzania Wahimizwa Kufuga Kibiashara sio Kitamaduni** ** Mkutano wa Kwanza wa Tasnia ya Kuku na ndege wafugwao Kusini mwa Afrika Wafanyika Tanzania** Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa ujio wa Mkutano wa Jukwaa la Tasnia ya Kuku na ndege wafugwao kwa Nchi za Kusini mwa Afrika unadhihirisha namna Tanzania chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt.Samia ilivyokuwa na mahusiano mazuri ambayo yamefungua milango katika sekta mbalimbali ikiwemo ya tasnia ya kuku na ndege wafugwao. Amesema hayo leo Oktoba 16, 2024 jijini Dar es salaam wakati akimwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdory Mpango katika ufunguzi wa mkutano huo. Ametaja faida za ufugaji kuku na ndege wafugwao kuwa ni pamoja na kuchangia usalama wa chakula na kuongeza pato la Taifa kikanda na kimataifa. Amesema kuwa asilimia 55 ya kaya nchini na katika nchi mbalimbali ni ufugaji unaofanywa zaidi na wanawake na vijana na kuwa Tanzania ina kuku milioni 103.1 wakiwemo kuku wa asili na kisasa. Kupitia Jukwaa hilo, Dkt. Biteko ameiagiza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuanzisha mashamba ya kuku wazazi kwa ajili ya kuzalisha vifaranga, kuanzisha vituo vya kisasa, maabara pamoja na kuwekeza katika machinjio ya kisasa ya kuku. Dkt. Biteko ametoa maagizo mengine ikiwemo “ Wizara iweke pia mfumo wa mnyororo baridi wa usambazaji wa kuku, iwekeze pia katika vizimba, chakula cha kuku na ianzishe viwanda vya kusindika vyakula vya kuku ili vipatikane ndani ya nchi na sio kutumia fedha za kigeni kuagiza nje,” Ametoa wito kwa wadau wote wa ufugaji wa kuku kuendeleakushirikiana na Serikali kutekeleza majukumu yao kwa kuwa Serikaliimetoa fursa kwa kila mmoja kuweza kujishughukisha na kujiongezea kipato. Fauka ya hayo, Dkt. Biteko ameikaribisha sekta binafsi kushiriki katika tasnia hiyo ili kusaidia kukuza uchumi wa nchi huku akiwataka watafiti kushirikiana na Serikali. Kwa upande wake, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema kuwa kufanyika kwa mkutano huo ni matokeo ya mkutano wa AGRA uliofanyika Dar es alaam na kuongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia ambapo AGRA walielezwa juu ya kuipa kipaumbele sekta ya ufugaji wa kuku kwa kuwa nchini Tanzania familia nyingi zinafuga kuku “Tunawashukuru AGRA na Food Alliance kwa kutukubalia na ndio maana leo jukwaa la kwanza limefanyika hapa Tanzania na kutoa fursa kwa wafugaji wetu kujifunza na kujenga mahusiano,” amesema Mhe. Ulega. Amebainisha kuwa takwimu zinaonesha kuwa ifikapo 2030 kuku watachangia asalimia 41 ya protini na kuwa watafiti nchini washirikiane na Serikali wanapotoa matokeo ili kutoleta taharuki kwa jamii kupitia matokeo ya tafiti zao. “ Hivikaribuni watafiti walifanya utafiti kwa kutumia sampuli chache juu ya ulishaji wa kuku wanaofugwa na akina mama na vijana tafiti ile ilileta taharuki, kupitia Jukwaa hili nitumie fursa hii kuwaambia watafiti washirikiane na Wizara ili kutotoa taarifa za taharuki kwa jamii na kuwa Serikali inaweza kudhibiti wafugaji wasiofuata taratibu hivyo tusiharibu jitihada zinazofanywa na kukuza tasnia hii,” amesema Mhe. Ulega. “Tunawaheshimu na kuthamini kazi zao ila tuone wanapofanya tafiti na kupeleka kwa jamii tuwe na mkakati wa pamoja wa kufikisha tafiti hizo kwa jamii,” amesisitiza Mhe. Ulega. Naye, Waziri Mkuu wa zamani wa Ethiopia na Mwenyekiti wa Bodi ya Muungano wa Mapinduzi ya Kijani barani Afrika (AGRA), Mhe. Dkt. Hailemariam Dessalegn, amesema kuwa fursa muhimu zilizopo kupitia ufugaji wa kuku ni chanzo cha protini, soko la uhakika na ajira kwa vijana na ka kushiriki katika mnyororo wa thamani. “Jukwaa hili linatoa fursa ya kujifunza faida na changamoto katika tasnia hii na kuongeza ushirikiano. Kukuza tasnia hii katika nchi yetu inahitaji majukwaa kama haya na inahitaji utayari wa wadau mbalimbali kwa kuwa wana uwezo wa kuwekeza ili kukuza tasnia hii,” amesema Mhe. Dessalegn. Ameongeza “Tanzania ni kinara wa kuwa na njia shirikishi na ni imani yangu itaendelea hivi chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia ili kufikia ajenda ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), haswa dhamira ya kumaliza njaa na umasikini ifikapo 2030. Hakuna nchi inayoweza kufikia mafanikio haya peke yake hivyo sera ya ukanda, mafunzo na majadiliano na mawasiliano ni muhimu kufikia malengo.” Mfugaji kutoka nchini Malawi, Grace Gondwe amesema kuwa baada ya kumaliza Chuo Kikuu nchini humo alianzisha biashara ya ufugaji wa kuku wa kisasa licha ya kukutana na changamoto mbalimbali amemudu kufanya kazi hiyo kwa miaka mitano sasa na kuwa tafiti mbalimbali zinaonesha mahitaji yake yaongezeka siku hadi siku. “Kupitia ufugaji nimekuwa mshauri pia kupitia Kampuni yangu tumeanza kutumia teknolojia katika uzalishaji wa kuku ambapo uzalishaii umekuwa mkubwa kwa gharama nafuu. Vijana wenzangu napenda kuwaambia tuendelee kufuga kuku kuna fursa nyingi pamoja zinazoendana na ufugaji wa kuku,” amesema Grace. Mfugaji wa kuku kutoka mkoani Tanga, Bw. Omary Mussa amesema kuwa ameanza ufugaji kupitia miradi mbalimbali na baada ya mafunzo amekuwa mfugaji tangu mwaka 2023 akianza na kuku 500 na sasa anafuga kuku 4,000 aina ya chotara na kuku wa kisasa. “Tanzania kufuga kuku ni utamaduni wetu tuna kazi ya kubadilisha kutoka kuwa tamaduni kuwa kibiashara nimeanzisha Kampuni ya Kuku Pesa Investment Group ili watu wafuge kuku kupata pesa,” amesema Mussa. Ameongeza “Changamoto ni kuwa watu wanafuga bila faida, Kampuni yetu inatoa mafunzo kwa mtu anaye fuga ikiwa ni pamoja na kubadilisha mitazamo kuwa sio lazima uajiriwe unaweza kujiajiri mwenyewe. Hadi sasa vijana 108 wamepata mafunzo na ufugaji na tuna wafugaji 98 tunaowasimamia mkoani Tanga.”
2377d2a595b1e432d7b5bed358f410e16f62ce204e041781aa7b110cf4a150d7
893
5.486002
42
4,899
1
0
0
0.111982
1.79
129
https://www.tia.ac.tz/waziri-mwigulu-nchemba-aingarisha-tia-kampasi-ya-mwanza/
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), ametembelea na kukagua ujenzi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania, Kampasi ya Mwanza, inayojengwa na Serikali kupitia Wizara ya Fedha, kwa gharama ya shilingi bilioni 7.8, kitakachokuwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi zaidi ya 5,000 kwa wakati mmoja, “Afisa Mtendaji Mkuu umefanya kazi nzuri sana, majengo ya Kampasi ya TIA Mwanza yamejengwa katika viwango ambavyo Serikali ya awamu ya sita inataka, sikutegemea kufanyika kwa kazi nzuri namna hii, hapa Mtendaji Mkuu na menejimenti mnastahili pongezi,”. Alisema Dkt. Mwigulu Naye, Afisa Mtendaji Mkuu Profesa William Pallangyo, amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitatu, Serikali kupitia Wizara ya Fedha, imeipatia TIA shilingi za kitanzania bilioni 58.1 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu ya kujifunzia na kufundishia katika Kampasi za Mtwara bilioni 6.1, Mbeya bilioni 3.2, Mwanza bilioni 7.8, Kigoma bilioni 11 na Zanzibar bilioni 30, “Kwa sasa, mradi wa Kampasi ya Mwanza umekamilika kwa asilimia 99 na unatarajia kuzinduliwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mnamo tarehe 12 Oktoba, 2024,”. Alisema Profesa Pallangyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mhe. Machibya Kashinje amesema wananchi wa Misungwi wamepokea mradi wa TIA kwa furaha kubwa ya wanafunzi kupata elimu ya juu katika mazingira mazuri na ya kisasa. “Ujenzi wa TIA Kampasi ya Mwanza Mhe. Waziri umefungua fursa nyingi sana hususani za elimu na uchumi kwa wakazi wa Misungwi, na kanda ya ziwa kwa ujumla,”. Alisema Mwenyekiti Machibya Mwananchi Joseph Majula, amesema ujio wa Kampasi ya TIA binafsi umempa fursa ya kupeleka vijana wake wawili kuanza cheti cha awali, na mmoja amechaguliwa kujiunga TIA kozi ya Ugavi na Ununuzi. Halikadhalika, Waziri Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba alipanda miti ikiwa ni kiashiri ya utunzaji mazingira.
212bae097b837723d3eea645705ba3a37271d09ba00469c4612fb070d6d1929c
290
5.562069
15
1,613
1
0
0
0
3.79
32
https://www.vpo.go.tz/news/makamu-wa-rais-awataka-vijana-kuacha-tabia-zisizo-za-kimaadili
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema zinahitajika tafiti za kina pamoja mikakati katika kufanya mapinduzi ya kitamaduni kubadili tabia na mazoea yasioyafaa yanayojitokeza katika jamii hivi sasa ambayo ni kikwazo kwa maendeleo. Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifungua Mkutano wa Kusherehekea Miaka 30 ya Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) uliyofanyika katika Ukumbi wa Johari Rotana Jijini Dar es Salaam. Ametaja baadhi ya mazoea na tabia hizo ni pamoja na kutojali muda, kutokuwa na uaminifu mahali pa kazi pamoja na kutumia njia zisizofaa katika kupata kipato. Makamu wa Rais ameitaka ESRF pamoja na Watalaam wa Fikra Tunduizi (Think Tank) kuangazia pia tabia za hivi karibuni za vijana kushiriki katika mahusiano na wanawake waliyowazidi umri maarufu (mashangazi) kama njia rahisi ya kujikimu, kutumia muda mwingi bila kufanya kazi kwa kushinda vijiweni, uchezaji kamari, utupaji taka ovyo, uchomaji moto ovyo wa nyasi na misitu pamoja na ubinafsi. Pia Makamu wa Rais amesema ni muhimu kuangazia tabia zingine kama vile matumizi makubwa ya fedha katika anasa kuliko kuweka akiba ikiwemo uchangiaji zaidi katika matukio ya sherehe na tafrija kuliko kusaidia gharama za elimu na matibabu kwa familia za kipato cha chini. Mengine ni kuongezeka kwa tabia ya utegemezi pamoja na kukithiri kwa vitendo vya ukatili kwa wanawake, watoto pamoja na vitendo vya ushirikina ikiwemo mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino). Halikadhalika Makamu wa Rais ametoa rai kwa ESRF kufanya tafiti katika maeneo mengine muhimu ikiwemo hatari za kimataifa kama vile mabadiliko ya haraka ya Teknolojia, kutokuwa na uchumi stamihilivu, mizozo mikali inayopelekea mivutano ya kisiasa pamoja na kufanya tafiti kufahamu mienendo ya soko la ajira na namna vijana watakavyoweza kuendana nayo. Amesema ili kutumia vema idadi kubwa ya vijana iliyopo barani Afrika ikiwemo Tanzania, Taasisi za Tafiti zinapaswa kuanisha ufadhili endelevu wa miradi na programu zinazopendelewa na vijana kulingana na vipaumbele vya Taifa. Aidha amesisitiza umuhimu wa tafiti katika sekta ya madini ikiwemo madini adimu ya kimkakati ambayo ni msingi wa viwanda vya teknolojia ya juu, tafiti juu ya utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi kwa njia endelevu pamoja na tafiti zitakazolenga kufanya mageuzi ya maeneo yanayotambulika kama nusu jangwa kuwa fursa mpya ya uzalishaji nchini. Amesema zinahitajika tafiti za maendeleo ya kilimo kwa kutumia maji yaliyopo chini ya ardhi pamoja na uvunaji maji ili kuleta mabadiliko katika maeneo hayo. Makamu wa Rais amesema Serikali ya Awamu ya Sita imedhamiria kuendelea kufanya kazi na kusaidia utafiti wa kiuchumi na uchambuzi wa sera unaofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) pamoja na taasisi nyingine za ndani ikiwa lengo ni kuongeza ufadhili wa utafiti na uwekezaji katika miundombinu inayounga mkono tafiti hizo. Amesema Serikali itaendelea kusisitiza Wizara, Idara na Wakala mbalimbali kutumia huduma zinazotolewa na ESRF ili kuhabarisha maendeleo ya sera na mikakati ya kisekta. Pia ameongeza kwamba Serikali itaendelea kuhimiza sekta binafsi, Azaki, Wadau wa Maendeleo na wadau wengine kuendelea kushirikiana na ESRF. Mkutano huo, umehudhuriwa na watafiti, wasomi, watunga sera, wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na watumishi wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) wa sasa na zamani.
8a5d8857c4a6f26fdbd868b63491eb992e7f766aa0f4eb954157c745819e833e
514
5.577821
16
2,867
1
0
0
0
0.19
80
https://www.pmo.go.tz/news/dkt-biteko-akaribisha-wawekezaji-sekta-ya-nishati
#### Habari ## Dkt. Biteko akaribisha wawekezaji sekta ya nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa Serikali inawakaribisha wawekezaji katika sekta ya nishati ili kuongeza kasi ya usambazaji, uzalishaji na unganishwaji wa nishati nchini Tanzania. Dkt. Biteko amesema hayo leo Oktoba 21, 2023 nchini Singapore wakati akishiriki mjadala kuhusu nishati akiwa pamoja na Waziri wa Madini na Nishati kutoka nchini Cambodia, Mhe. Keo Rottanak na Waziri wa Maliasili kutoka nchini New Zeland Mhe. Shane Jones wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Kimataifa ya Nishati ya nchini Singapore. “ Serikali haziwezi kufanya kila kitu zenyewe hivyo ni muhimu kushirikiana na sekta binafsi. Sisi Tanzania tunawaalika sekta binafsi ije kuwekeza katika sekta ya nishati kwa ajili ya kuimarisha uzalishaji, upatikanaji na usambazaji nishati na kuboresha maisha ya watu kwa ujumla,” amesema Dkt. Biteko. Akizungunzia, ajenda ya nishati safi ya kupikia nchini amesema kuwa ni matokeo ya utafiti uliofanywa na kubaini kuwa idadi kubwa ya Watanzania wanatumia kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia hali inayosababisha magonjwa ya mfumo wa upumuaji na uharibifu wa mazingira. Ili kupunguza athari hizo, Dkt. Biteko amesema kuwa Serikali imeandaa mkakati unaolenga kuhakikisha Watanzania asilimia 80 wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034. “ Serikali imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na kuhakikisha nishati safi inapatikana kwa urahisi na bei nafuu na hivyo tunawakaribisha wawekezaji kuja kuwekeza katika hili kwa sababu soko lipo,” amesema Dkt. Biteko. Kuhusu jitihada za Serikali za kuimarisha sekta ya nishati nchini, Dkt. Biteko ametaja miradi mbalimbali inayofanywa na Serikali ikiwemo mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP) wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2115. “ Serikali inaendeleza vyanzo vipya vya nishati mfano umeme wa jua, upepo na gesi, aidha kwa sasa asilimia 51 ya umeme unazalishwa kwa maji. Tanzania tumeendelea na maandalizi ya kuziuzia umeme nchi za Kenya, Rwanda, Burundi na sasa tunaendelea na mradi kwa ajili ya kuunganisha na nchi ya Zambia, kupitia Umoja wa Mauzio ya Umeme wa pamoja katika nchi za Afrika Mashiriki na Jumuiya za Kusini mwa Afrika (SADC) tuna soko la uhakika na hivyo tunawakaribisha wawekezaji kuja kushirikiana nasi,” amesisitiza Dkt. Biteko. Naye, Waziri wa Madini na Nishati kutoka nchini Cambodia, Mhe. Keo Rottanak amesema kuwa mwaka 1998 nchi yake ilifanya mageuzi makubwa katika sekta ya nishati na kuwa sasa asilimia 99 ya vijiji ina umeme. “ Tutahakikisha tunafikisha umeme katika nyumba za watu na malengo yetu ni ifikapo mwaka 2030 umeme unaozalishwa kwa jua kuwa mbadala wa umeme unaozalishwa na maji, amesema Mhe. Rottanak. Kwa upande wake, Waziri wa Maliasili na kutoka nchini New Zeland, Mhe. Shane Jones amesema kuwa nchi yake imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya kusambaza umeme na kuwa inajikita katika kuwekeza katika vyanzo mbadala vya kuzalisha nishati. Awali akifungua mkutano huo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Viwanda na Biashara wa Singapore Mhe. Gan Kim Yong amesema kuwa mahitaji ya nishati duniani yanazidi kuongezeka siku hadi siku hivyo nchi zinapaswa kubuni vyanzo mbadala na kupunguza madhara yatokanayo na gesi ya ukaa ifikapo mwaka 2050. Akitoa uzoefu wa nchi yake kwenye kuongeza vyanzo mbadala vya nishati amesema “ Kwa sasa tuko kwenye mkakati wa kuzalisha umeme kwa kutumia haidrojeni na nyuklia ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na kuongezeka kwa ushiriki wa Kampuni za Google na Amazon ambazo zimeonesha nia ya kuwekeza kwenye miradi ya nishati jadidifu.” Amesema Mhe. Kim Yong. Aidha,katika mkutano huo pia umefanyika uzinduzi wa tawi la ofisi ya kanda ya Shirika la Kimataifa la Nishati (IEA) nchini Singapore. =MWISHO=
34c24659a19bc208d209b390c8f5cecd16c353bcf8e359412f3140710c174f29
587
5.488927
33
3,222
1
0
0
0.340716
2.9
68
https://muhas.ac.tz/
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknoloji Prof. Adold Mkenda akisalimiana na Prof. Karim Manji mara ya kuwasili chuoni kwa ajili ya Hafla fupi ya Kumpongeza Prof. Manji Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Appolinary Kamuhabwa akitoa salamu za ukaribisho katika hafla fupi ya kumpongeza Prof. Karim Manji Mwenyekiti wa Baraza la Chuo, Dkt. Harrison Mwakyembe akitoa salamu za pongezi katika hafla fupi ya kumpongeza Prof. Karim Manji iliyofanyika chuoni MUHAS Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda akiangalia baadhi za tuzo ambazo Prof. Manji aliwahi kupata kabla ya kuanza rasmi hafla fupi ya kumpongeza Prof. Karim Manji akielezea mafanikio yake kwa ufupi katika sherehe ya kumpongeza iliyofanyika chuoni MUHAS Wageni waalikwa katika hafla fupi ya kumpongeza Prof. Karim Manjil iliyofanyika chuoni MUHAS Wageni waalikwa wakifatilia hotuba fupi ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda katika hafla fupi ya kumpongeza Prof. Karim Manji Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda akimkabidhi tuzo ya kumpongeza Prof. Karim Manji katika halfa fupi iliyofanyika chuoni MUHAS. Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda akimpongeza Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Appolinary Kamuhabwa kwa kuandaa halfa fupi ya kumpongeza Prof. Karim Manji Hafla ya Kumpongeza Prof. Karim Manji iliyofanyika chuoni MUHAS Participants during Startup School Workshop held at MUHAS Participants following up discussion during Startup School workshop held at MUHAS MUHAS Coordinator Innovation Unit Dr. Nelson Masota in a group photo with CEO Sahara Ventures Mr. Jumanne Mtambalike during Startup School Workshop held at MUHAS Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo MUHAS, Prof. Emmanuel Balandya (Kulia) na Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Akili Mirembe, Dkt. Paul Lawala (kushoto) wakisaini mkataba wa ushirikiano katika kufundisha, kufanya tafiti na Huduma za Ushauri wa kiutaalamu kati ya MUHAS na Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo MUHAS , Prof. Emmanuel Balandya ( Kulia) na Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe( kushoto), Dkt. Paul Lawala wakionyesha mikataba baada ya hafla fupi ya utiaji saini iliyofanyika chuoni MUHAS Previous slide Next slide ## STUDY AT MUHAS - Announcements - Registration for Semester one of the Academic Year 2024/2025 - action medeor foundation scholarship to support training program at the Pharm R&D Lab, School of Pharmacy - Innovation and Entrepreneurship in Health Care Innovation - Call For Applications into Funded Postdoctoral Fellowship - Diploma Selections for Academic Year 2024/2025- Round 11 - Revised University Supplementary Examinations Timetable - Invitation to the College for Medicine White Coat Ceremony for the Year 2024 - Important Notice on Orientation and Registration for Academic Year 2024/2025 - DHS Data and Complex Survey Analysis - Selection for Bachelor Programs Academic Year 2024/2025 - Selected Candidates for Diploma Programmes Academic Year 2024/2025 - Short Course on Hepatitis B and C Prevention, Control and Screening of People in High Risk Areas - The Health Data Analytics Training Focuses on Machine Learning Algorithms - A call for Training Workshop on Systematic Review and Meta-Analysis - PRESS RELEASE: MUHAS Emerges as 2024 Carnegie Host Institution for the Carnegie African Diaspora Fellowship Program - ESIA REPORT- Cardiac Teaching Hospital - Selected Applicants for Postgraduate Programmes for Academic Year 2024/2025 - Short Course on Quality Assurance and Quality Control of Herbal Products Level III - Short Course Training in Traditional Medicine Development Level II - Mafunzo ya Muda Mfupi ya Uendelezaji wa Dawa za Asili ( Ngazi ya I) - Almanac For SIDA- Supported Short Course - News - # Upcoming Conferences - Upcoming ShortCourse ### MUHAS YAPOKEA GARI LA PILI KUWEZESHA SHUGHULI ZA UTEKELEZAJI WA MRADI WA HEET Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) katika utekelezaji wa maeneo saba ya Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mabadiliko ### MUHAS YAPOKEA GARI KURAHISISHA SHUGHULI ZA UTEKELEZAJI WA MRADI WA HEET Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) katika utekelezaji wa maeneo saba ya Mradi wa Elimu ya Juu kwa ### VICE PRESIDENT IMPRESSED BY MUHAS KIGOMA CAMPUS DESIGNS The Vice President of the United Republic of Tanzania, Dr. Philip Isdor Mpango, commended the Muhimbili University of Health - Frequently Downloads - SSL VPN Request Form - East Africa’s Centres of Excellence in Skills and Tertiary Education in Biomedical Sciences Project Phase II Project ESMP mandatorily annexed to the Financing Agreement FA. - ESIA REPORT- CARDIAC TEACHING HOSPITAL Environmental and Social Impact Assessment Report For Kigoma Campus(ESIA Report) - Environmental and Social Impact Assessment Report For Mloganzila Campus(ESIA Report) - Trip Authority Form - The Amne Salim Covid-19 Research Fund Dissemination Symposium - MUHAS Research Excellence Award Guidelines - Payee Registration - Imprest Form - Petty Cash Form - Procurement Form - Kanuni Za Bunge - Annual Report - Prospectus, ByLaws & Guidelines - Policies & Plan Documents - MUHAS News Letter - Local Travel Form - Research Integrity&Conflict Of Interest Guidelines - Student Assessment Book
845bdeeb453982c52f59d26c171c2dd763e4ca766baa520896f6212838b2ba7d
805
5.522981
6
4,446
1
0
0
0.621118
7.95
30
https://www.maadili.go.tz/pages/faqs-2
##### Maswali **1. Kuhusu utoaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni, kuna changamoto ya Wenza kusaidia kupatikana kwa Taarifa za Tamko. Je, Mwenza asipowezesha kutoa taarifa sahihi itakuwaje?** **Jibu:** Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, jukumu ama wajibu wa kutoa tamko la rasilimali na madeni ni kwa kiongozi wa umma, ambaye anatakiwa kutoa tamko hilo juu ya rasilimali na madeni yake, ya mwenza/wenza wake, na watoto wake wenye umri chini ya miaka 18 ambao hawajaoa ama kuolewa. Mali zinazotakiwa kutolewa tamko ni pamoja na fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, viwanja, mitambo, na shughuli nyinginezo halali anazojishughuisha nazo. Endapo kiongozi atatumia majina ya mwenza, watoto au ndugu kuficha mali zake na akabainika kiongozi huyo atawajibishwa kwa mujibu wa sheria. Ni jukumu la kiongozi husika kumwelimisha mwenza wake kuhusu matakwa ya sheria ya maadili ili kumpatia ushirikiano katika kutekeleza sheria hiyo, endapo mwenza huyo hataelewa, kiongozi anashauriwa kuwasiliana na Ofisi ya Kamishna wa Maadili ili kupata ushauri zaidi. Endapo kiongozi wa Umma atashindwa kutoa taarifa zinazomilikiwa na mwenza/wenza kwa sababu mwenza huyo ameficha taarifa hizo/ ama hajawezesha kupatikana kwa taarifa husika, hatua za kisheria zitachukuliwa kwa atakayekuwa amehusika kuzuia utekelezaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. **2. Katika kipindi cha miezi sita ya kusubiria (Cooling off Period). Je, hairuhusiwi kiongozi kufanya shughuli nyingine yoyote?** **Jibu:** Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Kanuni ya 3(2)(g) ya Kanuni za Udhibiti wa Mgongano wa Maslahi 2020, kiongozi wa umma anapokuwa amestaafu au ameacha utumishi wa umma, ndani ya kipindi cha miezi sita tangu ameacha utumishi huo, (cooling off period), hataruhusiwa kuajiriwa, kujitolea, ama kujishughulisha na ajira kwa namna nyingine yoyote katika kampuni, watu ama ofisi yoyote inayofanya kazi na ofisi ya umma ambayo kiongozi huyo alikuwa akifanyia kazi alipokuwa madarakani. **3. Kuhusu malipo ambayo kiongozi hajalipwa na mwajiri wake wa zamani, je ayatamke kama madeni ya namna gani?** **Jibu:** Sheria inamtaka kiongozi wa umma kutamka rasilimali, maslahi na madeni yake anayodai ama anayodaiwa. Kama kuna malipo ambayo kiongozi hajalipwa, na anamdai mwajiri wake wa zamani ama wa sasa, ama anamdai mtu mwingine yeyote, kiongozi ataelezea deni hilo limetokana na nini pamoja na kiasi cha deni/madeni husika anachodai kwa mwajiri huyo. Vivyo hivyo endapo kiongozi anadaiwa na mwajiri, ama mtu mwingine yeyote atatamka deni hilo na kiasi anachodaiwa. **4. Kuhusu Tamko la Rasilimali na Madeni kwa Viongozi wapya, siku thelathini zinaanzia kuhesabika siku ya kuteuliwa au baada ya kuapishwa?** **Jibu:** Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma inamtaka kiongozi wa umma kutoa Tamko la rasilimali, masilahi na madeni ndani ya kipindi cha siku thelathini tangu kuteuliwa kwake katika nafasi aliyopewa. Kwa kawaida uapisho wa kiongozi aliyeteuliwa, hufuata mara baada ya uteuzi kufanyika, na uapisho unapofanyika ni ishara ya kiongozi anayoitoa kwa umma ya kuikubali dhamana pamoja na kuwajibika kwa nafasi aliopewa. **5. Ushauri kuhusu Tamko la Rasilimali na Madeni, Wenza wajaze matamko yao wenyewe. Je, inaruhusiwa?** **Jibu:** Viongozi wa Umma wanaowajibika na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, wametajwa katika Kifungu cha 4(1) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Aidha Gazeti la Serikali Na. 857 la tarehe 24 Novemba, 2023 limeorodhesha viongozi wanaowajibika na sheria hiyo, kwa kutaja vyeo vyote ambavyo viongozi wenye vyeo hiyvo wanapaswa kuwajibika na sheria ya maadili ikiwepo kutakiwa kutoa tamko la rasilimali, maslahi na madeni. Kwa mujibu wa sheria hiyo, Wenza wa Viongozi wa umma ambao hawana dhamana ya uongozi katika utumishi wa umma, hawapaswi na hawaruhusiwi kutamka rasilimali, maslahi na madeni yao binafsi kwa vile wao siyo viongozi wa umma kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Sheria inamtaka Kiongozi wa Umma kutamka rasilimali, maslahi na madeni yake, mweza/wenza wake na watoto wake walio chini ya umri wa miaka 18 ambao hawajaoa ama kuolewa. **6. Ni nini sababu ya kutoa tamko miezi mitatu kabla ya kustaafu?** **Jibu:** Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma inamtaka kiongozi wa umma kutoa tamko la rasilimali, maslahi na madeni katika vipindi vitatu: Kipindi cha siku thelathini tangu alipoteuliwa au kuchaguliwa; Kila ifikapo tarehe 31 Desemba ya kila mwaka, na kwa kipindi cha siku tisini kabla ya kustaafu utumishi wake kwa umma. Lengo la matamko haya yote kwa pamoja ni kumwezesha kiongozi kutekeleza matakwa ya sheria ya maadili ya viongozi wa umma ambayo imeainisha aina za matamko hayo na namna ya kuyatoa. **7. Je, kiongozi haruhusiwi kuwa na hisa?** **Jibu: **Sheria ya maadili ya Viongozi wa umma haijakataza viongozi kumiliki mali za aina yoyote zikiwemo hisa. Kiongozi wa umma anayo haki ya msingi na kikatiba kama raia mwingine yeyote kumiliki mali na kuhakikishiwa usalama wa mali zake. Kiongozi wa umma anachotakiwa kufanya ni kuwa muadilifu na kuhakikisha hisa ama mali nyingine zozote anazomiliki ni mali halali zinazotokana na kipato chake halali, na atoe tamko la hisa hizo, atamke idadi au kiasi cha hisa alizonazo, atamke kampuni yenye hizo hisa, pamoja na gawio ama faida anazozipata kutokana na hisa hizo. Kiongozi asitumie madaraka ama wadhifa wake kujipatia mali ama kujilimbikizia mali kinyume cha sheria. **8. Ukikuta fedha zimewekwa kwenye Akaunti yako bila ufahamu ukazitumia, inakuwaje?** **Jibu:** Uendeshaji wa akaunti binafsi katika taasisi za fedha ni jukumu la mmiliki binafsi wa akaunti hiyo. Endapo fedha zimewekwa ama kutolewa katika akaunti husika bila mmililki wa akaunti kufahamu, mmiliki wa akaunti hiyo anapaswa kutoa taarifa mara moja kwa uongozi wa benki husika. Ni kosa kwa kiongozi ama mtu yeyote kutumia fedha zilizoingizwa kwenye akaunti yake ya benki bila kujua fedha hizo zilikotoka. Kwa kutoa taarifa mapema kwa uongozi wa benki, kutamwondolea kiongozi ama mmililki wa akaunti husika kuhusishwa na matukio yasiyofaa ya wizi wa fedha, kusafirisha fedha haramu ama kujihusisha na matukio ya utakatishaji fedha, ambapo hatua za kisheria zinaweza kuchukuliwa dhidi yake. **9. Kama kuna taarifa ambazo bado kiongozi hajazipata ndani ya siku thelathini baada ya kupata wadhifa inakuwaje? ** **Jibu: **Endapo kiongozi wa umma atakuwa hajapata baadhi ya taarifa za umiliki wa rasilimali, maslahi au madeni yake anayotakiwa kuyatolea tamko ndani ya siku thelathini kwa mujibu wa sheria, ama endapo atapata changamoto zozote katika kutekeleza matakwa ya sheria ya maadili ya viongozi wa umma katika kutoa tamko hilo, kiongozi huyo anaweza kuwasiliana na ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa ushauri. **10. Kuhusu kudhibiti Mgongano wa maslahi, Je, viongozi wakatae kupokea michango ya harusi au wajiondoe kushughulikia masuala ya wale waliowachangia?** **Jibu:** Mgongano wa Maslahi ni tatizo la kimaadili. Hata hivyo, Viongozi wa umma, hawapaswi kujitenga ama kuishi kwa kukwepa kushiriki matukio ya kijamii yanayotokea ndani ya jamii kwa kisingizio cha kukwepa ama kudhibiti mgongano wa maslahi. Viongozi wanashauriwa kushiriki matukio ya harusi, misiba, nk katika jamii wanamoishi kwa uadilifu, pamoja na kushirikiana na wanajamii wengine bila kujihusisha na mgongano wa kimaslahi, na endapo kiongozi atakuwa na mashaka juu ya ushiriki huo anaweza kuwasiliana na Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa ushauri juu ya suala hilo. **11. Waheshimiwa Majaji wanaruhusiwa kufanya biashara?** **Jibu:** Viongozi wa Umma hawapaswi kuishi kama kisiwa. Wanayo fursa kisheria kufanya shughuli nyingine halali ili kuwaongezea kipato. Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma hajakataza kiongozi wa umma yeyote kujihusisha na biashara yoyote halali. Waheshimiwa Majaji na Viongozi wengine wanayo haki ya kufanya biashara. Wanaweza kufanya biashara, kununua hisa katika makampuni mbalimbali, kufanya shughuli za kilimo, ufugaji, nk. Ni jukumu la kiongozi husika kuona kwamba biashara ama shughuli nyingine anayoifanya ama anayotaka kuifanya ni halali na haitamzuia wala kuathiri kutekeleza ipasavyo majukumu na wajibu wake kwa umma. **12. Ni namna gani unaweza kushughulikia mgongano wa maslahi unaoweza kutokea kwa sababu ya biashara za familia au nafasi ya udhamini?** **Jibu:** Kiongozi wa Umma anatakiwa kujiepusha na Mgongano wa Maslahi katika maeneo yote ya biashara za familia ama nafasi za udhamini. Endapo familia inafanya biashara inayomsababishia kiongozi kuingia katika mgongano wa maslahi, kiongozi anapaswa kutamka maslahi hayo kwa mamlaka yake ya Nidhamu ama kwa Kamishna wa Maadili. Kwa mujibu wa Kanuni za Kudhibiti Mgongano wa Maslahi za mwaka 2020, masuala mbalimbali yameainishwa ya namna ya kiongozi kuepuka mgongano wa maslahi. Kanuni hizo zinampa kiongozi wa umma fursa ya kuwasiliana na Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ili kuomba ushauri kuhusu namna anavyoweza kufanya shughuli zake za biashara ama nyinginezo bila kujiingiza kwenye mgongano wa maslahi. **13. Ni hatua zipi zinachukuliwa kwa Viongozi wanaokiuka maadili? ** **Jibu:** Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, inafanya kazi ya kusimamia maadili kwa viongozi wa umma. Viongozi wanaothibitika kukiuka maadili wanachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria. Kila mara Kamishna wa Maadili anapokuwa na malalamiko yaliyochunguzwa na kujiridhisha kwamba kiongozi amekiuka maadili, kiongozi huyo huitwa kwenye Baraza la Maadili ambalo ndicho chombo cha kisheria kinachosikiliza na kufanya maamuzi ya mashauri ya viongozi waliokiuka maadili, na taarifa ya Baraza hilo huwasilishwa kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika. Hatua zinazoweza kuchukuliwa dhidi ya Kiongozi wa umma aliyekiuka maadili, zimeainishwa katika Kifungu (8)(a-g) cha Sheria ya Maadili, ikijumuisha kuonywa, kushushwa cheo, kusimamishwa kazi, kufukuzwa kazi, kufikishwa mahakamani, nk. **14. Hivi ni kweli mwenye pesa ndio mwenye haki na mnyonge hawezipata huduma kwa haki? Msemo huo una ukweli kiasi gani? ** **Jibu:** Wananchi wote wana haki sawa bila kujali hali yao ya kipato, katika kupata huduma za umma. Huduma nyingi za umma hutolewa bure, hata hivyo zipo baadhi ya huduma ambazo zinatakiwa kuchangiwa gharama kidogo kwa mujibu wa taratibu za taasisi husika zinazotoa huduma hizo. Ila kwa huduma ambazo ni za bure mwananchi hapaswi kudaiwa fedha, na endapo fedha zinadaiwa kwa huduma ambazo hotolewa bure, mwananchi watoe taarifa mara moja kwa mamlaka zinazohusika ikiwepo Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili inafanya kazi kwa kushirikiana na taasisi nyingine kama vile Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Jeshi la Polisi, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, nk., hivyo endapo mwananchi anaona kiongozi ama mtumishi wa umma anakiuka maadili kwa kuomba kupewa rushwa, ama kukataa kutoa huduma bila sababu za msingi, mwananchi atoe taarifa mara moja kwa Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi ama ofisi nyingine iliyotajwa hapo juu kwani Ofisi za Umma huwa zinafanya kazi kwa ushirikiano. Wananchi wanashauriwa kuwa tayari kutoa taarifa zinaweza kubaini watumishi na viongozi wanaokiuka maadili. Taarifa zinaweza kutufikia kwa mwananchi kufika moja kwa moja katika Ofisi zetu, kupiga simu, kuandika barua, ama kutuma taarifa kupitia *link* iliyopo kwenye tovuti ya Sekretarieti, www.maadili.go.tz
2a48e2554114cbe5cf135198c66955837156a1bf8f503717f5a2d74648dd2697
1,723
5.694719
83
9,812
1
0
0
0.058038
1.57
228
https://www.maadili.go.tz/complaints
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika." > Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara." > Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo." > Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa." >
f2f2d94263cec1b833408a2c1cb361463602bee90ed9ad393f5f2c72b19c9ebd
361
5.642659
15
2,037
1
0
0
0
1.66
58
https://www.maadili.go.tz/pages/history
##### Historia Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ni Idara ya Serikali inayojitegemea chini ya Ofisi ya Rais iliyopewa mamlaka ya kuchunguza tabia na mwenendo wa kiongozi wa umma yeyote kwa madhumuni ya kuhakikisha kuwa masharti ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma yanazingatiwa ipasavyo. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ilianzishwa chini ya Ibara ya 132 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Sekretarieti ya Maadili imepewa mamlaka ya kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya 1995 sura 398. Sheria hii ilianza kutumika tarehe 01 Julai 1995 na inatumika Tanzania Bara pamoja na Zanzibar kwa viongozi wenye madaraka katika Serikali ya Muungano. Sekretarieti ya Maadili inaongozwa na Kamishna wa Maadili ambaye huteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, Rais huwezesha kupatikana kwa watumishi wengine wa Sekretarieti ya Maadili ambao huwajibika kula kiapo cha kutunza siri zinazohusiana na majukumu ya taasisi. Taasisi ina ofisi ya Makao Makuu iliyopo Dodoma pamoja na ofisi nane za Kanda kama ifuatavyo; **Kanda ya Nyanda za Juu Kusini**yenye mikoa ya Mbeya, Iringa, Katavi, Songwe, Njombe na Rukwa. **Kanda ya Kusini**yenye mikoa ya **Kanda ya Kati**yenye mikoa ya **Kanda ya Kaskazini**yenye mikoa ya **Kanda ya Magharibi**yenye mikoa ya Tabora, Kigoma, Simiyu na Shinyanga. **Kanda ya Ziwa**yenye mikoa ya Mwanza, Mara, Geita na Kagera. **Kanda ya Mashariki**yenye mikoa ya **Kanda Maalum**yenye mikoa ya
612b62ad4e0c1c99efffd67756068d5ad87e89f473a3b9787f5adce0cc8ad471
232
5.491379
11
1,274
1
0
0
0.431034
3.45
20
https://www.maadili.go.tz/publications/bronchures
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika." > Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara." > Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo." > Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa." >
b1cb595baefd1ddd849151cd92f656675c6775c034282468ca77042d9cac11a2
374
5.644385
15
2,111
1
0
0
0
1.6
59
https://ods.maadili.go.tz
Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ni miongoni mwa Taasisi za usimamizi wa masuala ya Utawala Bora nchini Tanzania iliyoundwa kwa mujibu wa Ibara ya 132 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 (Sura ya Pili ya Sheria za nchi). Jukumu la msingi la Sekretarieti ni Kukuza na Kusimamia Maadili ya Viongozi wa Umma, kwa kuzingatia Dira ya Taasisi ambayo ni kuwa kitovu cha bora na ufanisi katika kukuza na kusimamia Maadili ya Viongozi wa Umma. Kupokea a kuhakiki taarifa za Rasilimali na madeni ya Viongozi wa Umma ni moja ya jukumu la Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma lililoainishwa katika Sheria ya Maadili Na. 13 ya Mwaka 1995. Sheria inamtaka Kiongozi wa Umma kuwasilisha Tamko la Rasilimali na Madeni kwa Kamishna wa Maadili kabla au ifikapo tarehe 31 Desemba kila Mwaka. Tangu kuanzishwa kwa Sekretarieti ya Maadili, Matamko ya Rasilimali na Madeni ya Viongozi yamekuwa yakipokelewa na kuwasilishwa Sekretarieti kwa nakala ngumu zoezi ambalo limekuwa na changamoto nyingi ikiwemo:- Gharama kubwa za uchapishaji wa fomu za Tamko na muda mwingi unaotumika kutuma fomu ili ziweze kuwafikia Viongozi. Ili kukabiliana na changamoto hizi Sekretarieti imeamua kuwekeza katika matumizi ya TEHAMA kwa kuanzisha Mfumo wa Ujazaji Matamko kwa njia ya Mandao (Online Declaration System -ODS). Kuhama kwenda katika matumizi ya TEHAMA kutaisaidia Sekretarieti kupunguza gharama hasa zile za uchapishaji wa fomu, usambazaji na wakati mwingine kuandika barua za kukiri kupokeaTamko. Mfumo wa ujazaji Matamko kwa njia ya Mandao (ODS) ni Mfumo mpya unaomuwezesha Kiongozi wa Umma kujaza Tamko la Rasilimali na Madeni na kuliwasilisha kwa Kamishna wa Maadili kwa nia ya Mandao. Mfumo huu utamuwezesha Kiongozi kutuma tamko lake akiwa sehemu yoyote na wakati wowote na zaidi utampunguzia gharama na muda aliokuwa akitumia kuwasilisha Tamko lake hapo awali. Ili kuweza kutumia mfumo huu Kiongozi atatakiwa kuwa na kompyuta na huduma ya intaneti. Ni matumaini yang kuwa kupitia mfumo huu hapatakuwa na Kiongozi atakaechelewa kuwasilisha Tamko au kushindwa kuwasilisha tamko. __Hotline Numbers__ + 255 26 2160 190 + 255 734 101040 __General Contact__ + 255 26 2160 192 [email protected] www.maadili.go.tz __Declaration Desk__ [email protected]
e0e0ba1e076f39eb5dbff6111c8c769bfea41812f17594152a5a995c0ddeb789
348
5.531609
13
1,925
1
0
0
0
5.46
53
https://www.maadili.go.tz/news/prof-sedoyeka-mkuu-wa-chuo-cha-iaa-afikishwa-mbele-ya-baraza-la-maadili
##### BARAZA LA MAADILI LAHITIMISHA KUSIKILIZA TUHUMA ZINAZOMKABILI PROF. SEDOYEKA Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma limehitimisha kikao chake cha siku mbili cha kusikiliza tuhuma za ukiukwaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma zilizokuwa zikimkabili Mkuu wa chuo cha Taasisi ya Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka. Kikao hicho kilichohitimishwa tarehe 17.10.2024 kiliongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Rose Teemba akisaidiana na wajumbe wa Baraza Bw. Peter Ilomo na Bi Suzan Mlawi. “Baraza litafanya hitimisho baada ya kusililiza pande zote mbili, ushauri utapelekwa kunako husika,” alisema Mhe. Teemba baada ya Prof. Sedoyeka kutoa utetezi wake. Prof. Sedoyeka alikuwa akikabiliwa na mashtaka manne anayodaiwa kutenda wakati akitimiza majukumu yake ya uongozi. Mashtaka hayo ni kumpandisha cheo Bw. Hakimu Ndatama kutoka Afisa Rasilimaliwatu daraja la II kuwa Mkuu wa sehemu ya Rasilimaliwatu bila kuwa na sifa, kuwa na mgongano wa maslahi kwa kufanya uamuzi wa kumnufaisha Bw. Ndatama, kuingilia mchakato wa zabuni ya ununuzi na ufungaji wa viti na meza katika kampasi ya Babati kwa kuifuta bila kufuata utaratibu na kufanya uhamisho wa ndani wa Afisa Ugavi kutoka kitengo cha Ununuzi na Ugavi kwenda Idara ya Maktaba tofauti na sifa za kitaaluma za mtumishi. Akiwasilisha mashtaka mbele ya Baraza tarehe 16 Oktoba, 2024 Wakili Mkuu wa Serikali Bi Emma Gelani alilieleza Baraza kuwa mlalamikiwa anakabiliwa na mashtaka manne na ameshindwa kutimiza matakwa ya kifungu cha 6(1)(a) 6(1)(c) na 12(1)(c) vya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. “Mlalamikiwa wakati akitekeleza majukumu yake ya uongozi pasipo kufuata sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma alimpandisha cheo Bw. Hakimu Ndatama kutoka Afisa Rasilimali II kuwa Mkuu wa sehemu ya Rasilimaliwatu kabla ya kukamilika kwa uhamisho wa mtumishi.” Hata hivyo, Prof. Sedoyeka alikana tuhuma zote zilizowasilishwa mbele ya Baraza. Bw. Ndatama ambaye ni mmoja kati ya mashahidi sita waliotoa ushaidi mbele ya Baraza alikiri kuwa tarehe 13.5.2023 alipandishwa cheo kutoka Afisa Rasilimaliwatu II kuwa Mkuu wa sehemu wa IAA kabla ya taratibu za uhamisho kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii hazijakamilika. Akitoa utetezi wake mbele ya Baraza kuhusu tuhuma hiyo, Prof. Sedoyeka alisema, “Sikuwa na mamlaka ya kumpandisha cheo Bw. Hakimu, isipokuwa nilimteua na kumpangia majukumu. Nilimteua kwa nia njema ya kuongeza ufanisi, kwa maelezo hayo, naomba Baraza lako lifute shtaka hili kwasababu nilitekeleza kwa nia njema.” Kuhusu lalamiko la kufanya uamuzi wa kumnufaisha Bw. Hakimu, Mkuu huyo wa chuo alilieleza Baraza kuwa hakuhusika na mchakato wa kumuombea uhamisho Afisa huyo kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii kwenda IAA. “Mimi sikuhusika kwa namna yoyote ile, kuomba Bw. Hakimu kuja IAA alipata barua tarehe 9.3.2023 wakati mimi nililipoti IAA tarehe 13.3.2023, hivyo, sikusaini barua yake ya kuomba ahamie wala kukumbushia,” alieleza. Kuhusu kuingilia zabuni ya ununuzi na ufungaji wa viti na meza na kuifuta kinyume kifungu cha 59(2) cha Sheriai ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, Mkuu huyo wa chuo alilieleza Baraza kuwa Taasisi yake ilipohitaji viti katika kampasi ya Babati, alielekeza iundwe kamati kutembelea maeneo tofauti nchini kuangalia mzabuni mwenye uwezo. “Nilielekeza Kitengo cha Manunuzi kumhusisha mzabuni Timber and Hardware Ltd na kamati ilikuwa na mapendekezo yake,” alisema na kuongeza kuwa, “Baada ya mchakato kufanyika, nilipitia nyaraka za mchakato .wa ununuzi na kugundua kuwa kuna wazabuni wawili walikuwa na bei ndogo hawakushinda kwa madai kuwa bidhaa zao hazikufikia viwango, watu hawa walishinda zabuni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, lakini kwetu hawakufikia viwango.” Kwa mujibu wa kiongozi huyo, taarifa ya ukaguzi ya vifaa husika haikuwa na maelezo ya kitaalam kukataa wazabuni waliokuwa na bei nafuu. “Kwangu mimi hii ni dosari, nilikuwa kwenye **mtanziko,** nikaamua kufanya kikao na mwenyekiti wa Bodi ya zabuni tukakubaliana kuwa hata tukitangaza zabuni upya kwa kuwa nyaraka ni zilezile, hakuna jinsi atashinda Jaffery ING Sign Ltd aliyekuwa na bei kubwa.” Katika mchakato huo wa ununuzi wa viti na meza, jumla ya kampuni nne zilijotokeza ikiwemo Jaffery ING Sain Ltd iliyopata zabuni kwa shilingi 1,144,057,200/, Timber and Hardware Ltd 1,013,974,000.03, Vadeck Investment Company Ltd iliyoomba zabuni kwa shilingi 762,625,003/= na kampuni ya Mult Cable Ltd kwa gharama ya shilingi 1,163,527,200.03. Prof. Sedoyeka alifuta zabuni kwa madai kuwa gharama ilikuwa kubwa kuliko bajeti ya taasisi ya shilingi bilioni 1.274 Mchakato huo uliositishwa Juni, 2023, hadi sasa hivi bado haujakamilika. Shahidi wa kwanza katika lalamiko hilo Bw. Ramadhani Mwanang’waka ambaye ni Afisa wa Sekretarieti ya Maadili alisema kuwa “baada ya kupitia nyaraka za zabuni tulibaini kuwa sababu za kusitisha zabuni hazikuwa miongoni mwa sababu zilizohainishwa kisheria.” Kuhusu uhamisho wa ndani wa Bw. Robert Mwitango Afisa Ugavi kutoka kitengo cha Ununuzi na Ugavi kwenda Idara ya Maktaba tofauti na sifa za kitaaluma za mtumishi, aliliambia Baraza kuwa, “Mimi ninayo mamlaka kumpangia shughuli nyingine mtumishi na uhamisho huu ulikuwa na nia njema kwa maslahi ya Taasisi.” “Kitengo cha Unununzi kilikuwa na watumishi 10, Idara ya Maktaba ilikuwa na upungufu wa watumishi na walitaka kufanya ununuzi mkubwa wa vitabu, kutokana na uhaba mkubwa wa rasilimaliwatu katika Maktaba, niliona kuhamisha mtumishi ni suala la kawaida katika taasisi,” alilieleza Baraza. Bw. Robert aliyefika mbele ya Baraza kutoa ushahidi, alikiri kuhamishiwa Idara ya Maktaba kwa barua ya tarehe 6.10.2023 ambayo haikubainisha majukumu ya kazi. “Nililipoti Maktaba nakupangiwa kukaa mapokezi kukagua wanafunzi wanaoingia na kutoka ndani ya Maktaba.” Bw. Robert ni Afisa ugavi daraja la I ambaye ni Certified Procurement and Supply Professional (CPSP). Wakili Gelani alilieleza Baraza kuwa .“uhamisho huu ulifanyika bila kuzingatia matakwa ya Kifungu cha 6(1)(c) cha Sheria ya Utumishi wa Umma kinachowataka wakuu wa Taasisi kusimamia na kuhakikisha watumishi wanakuwa katika taaluma zao.” “kitendo hiki ni kinyume na Kifungu cha 6(2) cha Sheria ya Maadili.”. Wakati akimsomea mashtaka mlalamikiwa, Bi. Gelani aliliambia Baraza kuwa, “Malalamiko dhidi ya Prof. Sedoyeka ni kinyume na kifungu cha 6(1)(c) cha Sheria ya Maadili kinachomtaka kiongozi wa umma kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Sheria za nchi,”alisema.
580d486d9d375e4a0b88efc8064081179f875b99c64f23cf263695de28957a92
953
5.737671
36
5,468
1
0
0
0.104932
1.89
118
https://www.maadili.go.tz/news/jaji-mst-mwangesi-hauwezi-kuwa-mwangalizi-wa-maadili-ya-watu-wengine-kama-wewe-huna-maadili
##### Jaji (Mst.) Mwangesi: Hauwezi kuwa mwangalizi wa maadili ya watu wengine kama wewe huna maadili. Rai imetolewa kwa Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na weledi wa hali ya juu wanapotekeleza majukumu yao. Rai hiyo imetolewa na Kamshina wa Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi wakati akiakifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi cha Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Cate mjini Morogoro Septemba 23, 2024. ‘’Hauwezi kuwa mwangalizi wa maadili ya wengine wakati wewe mwenyewe hauna maadili, hivyo kama mfanyakazi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma unatakiwa kuwa mfano wa kuigwa na watumishi wengine wa Umma katika nyanja ya uadilifu,’’alisema Mhe. Mwangesi. Jaji (Mst.) Mwangesi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo la Wafanyakazi wa ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, ameongeza kuwa uadilifu unajengwa kwa nguzo kuu tatu. Alizitaja nguzo hizo kuwa ni utaalamu, uaminifu na uwajibikaji na kuongeza kuwa ni wajibu kwa kila mtumishi wa Sekretarieti kuzingatia nguzo hizo. ‘’Ninawaasa kuzingatia nidhamu na kujituma katika kutekeleza majukumu yenu na yeyote atakayeenda kinyume na hayo, atakua si miongoni mwetu na hatutasita kumchukulia hatua kutokana na mwenendo wake,’’alisema. Katika hatua nyingine, Kamishna huyo wa Maadili, amezungumzia umuhimu wa watumishi kutunza na kulinda rasilimali za Taasisi na kuacha uzembe katika matumizi ya mali na vitendea kazi vya ofisi kutokana na upatikanaji wake kuwa wa gharama. ‘’Niwaombe kuacha uzembe na kuwa makini katika matumizi ya vitendea kazi na kuvitunza kwa hali na mali kwani vitendea kazi tulivyonavyo ni vichache na upatikanaji wake ni washida sana,’’amesisitiza. Kuhusu kuufanyaji kazi kwa ushirikaiano, Mwenyekiti huyo wa Baraza la Wafanya kazi, aliwapongeza watumishi wa Sekretarieti ya Maadili kwa kufanya kazi kwa ushirikiano na kuomba hali hiyo iwe endelevu na amesisitiza kuwa kwake milango ipo wazi kwa yeyote mwenye jambo kumuona na kujadili kwa pamoja. ‘’Niwapongeza kwa ushirikiano wenu katika utendaji kazi na ninawaomba ushirikiano huo mnaonionyesha mimi pia uwe endelevu miongoni mwenu ili tuweze kuifikisha mbali Taasisi yetu,’’ alisisitiza.
1653cc2059fdd0f99a93b1191177c6a41fd810919291398ab683ac89c63acf7d
343
5.740525
16
1,969
1
0
0
0.291545
0.87
61
https://www.maadili.go.tz/news/viongozi-wa-halmashauri-ya-mpwawa-waaswa-kufanya-kazi-kwa-kushirikiana
##### Viongozi wa Halmashauri ya Mpwawa waaswa kufanya kazi kwa kushirikiana Viongozi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa ambao ni madiwani pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wameaswa kuzingatia dhana nzima ya uwajibikaji wa pamoja wakati wanatekeleza majukumu yao ya kila siku ili kuweza kuwaletea wananchi maendeleo kuipatia serikali mafanikio. Wito huo umetolewa na Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili Kanda ya Kati – Dodoma Bi. Jasmin Awadh wakati akitoa mafunzo hayo kwa viongozi hao yaliyofanyika katika Halmashauri hiyo tarehe 05 Septemba, 2024 Aidha Bi. Jasmin alieleza kuwa suala la uwajibikaji wa pamoja kwa Viongozi lisipozingatiwa litasababisha ucheleweshwaji wa huduma za kijamii kwa wananchi kama vile hospitali, shule, barabara n.k na wananchi watapoteza imani yao kwa serikali. ”Kunapokua na mkinzano baina ya viongozi juu ya namna ya utekelezaji wa huduma mbalimbali za kijamii huyu anasema tufanye vile yule anasema tufanye vile lazima huduma hizo zikwame ama kutokufanyika kabisa” Bi.Jasmin aliwahimiza viongozi hao kushirikiana katika kupanga vipaumbele vya Taasisi ili kuhakikisha kwamba malengo yaliyopangwa na halmashauri yanatekelezwa ipasavyo ikiwemo kuwafikishia wananchi huduma wanazohitaji. “Nyinyi kama Viongozi mnapaswa kuwashirikisha watumishi walio chini yenu juu ya mikakati mliyonayo ili muweze kushirikiana kuitekeleza mnapaswa nyote muwe na uelekeo mmoja kila mtumishi aelewe jukumu lake katika kufanikisha malengo ya Taasisi” Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa Mhe. George Rume alisema kuwa mafunzo hayo kwa viongozi hao ni muhimu sana kwani yatawasaidia kuleta mabadiliko katika halmashauri yao kwani suala la maadili ni la muhimu sana hasa ushirikiano na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu yetu. Kwa mujibu wa Mhe Rume alieleza kuwa kiongozi yeyote ni lazima ajue dira ya Taasisi yake kwamba nini anatakiwa kufanya ili aweze kuwaongoza walio chini yake kuitekeleza na kuleta maendeleo kwa wananchi na serikali kwa ujumla. ”Tukianza kukinzana viongozi kwa viongozi hatufiki popote na tutazorotesha juhudi za serikali za kuwaletea wananchi maendeleo’’ alisema. Mafunzo hayo ni mkakati na kipaumbele cha Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuhakikisha kwamba Viongozi wote wanashirikiana katika Taasisi zao wanafanya kazi kwa pamoja kwa kuzingatia viwango vya juu vya maadili na kuleta matunda kwa wananchi
f228babc081dd97aea992c372b0610fb257e0d29af0fa82bc75232585182762a
340
6.002941
10
2,041
1
0
0
0.294118
1.18
53
https://www.maadili.go.tz/pages/disclaimer
##### Angalizo Angalizo Hakuna madai yatakayotolewa kuhusu usahihi au uhalali wa maudhui ya tovuti hii. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma haitakubali dhima yoyote kwa mtu yeyoye kwa taarifa au ushauri unaotolewa kwenye tovuti hii au kushirikishwa kwenye tovuti hii kwa marejeo. Taarifa iliyomo kwenye tovuti ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma haipaswi kuonyeshwa isipokuwa katika mfumo kamili wa sklini. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inaweza kuwaunganisha na wavuti za tovuti za nje zilizo za serikali au zisizo za serikali (Tovuti za mtumiaji watatu) isipokuwa pale itakapoelekezwa vinginevyo; - Haishirikishwi au kuhusishwa na mmiliki au mwendeshaji wa tovuti ya mtumiaji wa tatu; na - Kama una maswali yoyote kuhusu maudhui yaliyomo kwenye tovuti ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, tafadhali wasiliana nasi.
b647df4283dedb388e981f9884f52eda1cde8446b40e28aa8a3ed581d80bb921
129
5.666667
4
731
1
0
0
0.775194
2.33
16
https://www.uchukuzi.go.tz/pages/about-us
#### Kuhusu Sisi Kuhusu Sisi Wizara ya Uchukuzi iliundwa tarehe 30 Agosti, 2023 kwa kuzingatia Hati ya Mgawanyo wa Majukumu ya Serikali (Instrument) iliyotolewa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa mujibu wa hati ya mgawanyo wa majukumu, majukumu ya Wizara ya Uchukuzi ni kama ifuatavyo: - Kuandaa Sera za usafiri na kusimamia utekelezaji wake; - Kuandaa Sera ya Hali ya Hewa na kusimamia utekelezaji wake; - Kusimamia usafiri na usafirishaji kwa njia ya reli; - Kusimamia usafiri na usafirishaji kwa njia ya Anga; - Kusimamia usafiri na usafirishaji kwa njia ya maji; - Kusimamia utoaji wa leseni za usafirishaji; - Kusimamia utoaji wa taarifa za hali ya hewa kuimarisha usalama hususan katika usafiri kwa njia ya anga na maji; na - Kuongeza tija katika utendaji kazi, kuendeleza rasilimali watu na kusimamia Idara za Serikali, Taasisi, Mashirika ya Umma na miradi iliyo chini ya Wizara ya Uchukuzi. **DIRA** Kuwa nchi yenye huduma za uchukuzi na hali ya hewa zenye uhakika, usalama na nafuu. **DHIMA** Kusimamia na kuwezesha maendeleo ya miundombinu, huduma za uchukuzi na hali ya hewa kwa kutumia sera, sheria na miongozo iliyopo kwa maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi.
59b5c608c12873fdf12930120b608e0f5f782bbde6f42de8f365622c1316fc77
198
5.171717
6
1,024
1
0
0
0.505051
5.56
28
https://www.uchukuzi.go.tz/pages/organization-structure
#### Muundo **IDARA NA VITENGO** Wizara ya Uchukuzi inaundwa na Idara tano (5) ambazo ni Utawala na Menejimenti ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Sera na Mipango, Miundombinu ya Uchukuzi, Huduma za Uchukuzi na Usalama na Mazingira. Aidha, Wizara hii inaundwa na Vitengo saba (7) ambavyo ni Fedha na Uhasibu, Ufuatiliaji na Tathminini, Mawasiliano Serikalini, Ununuzi na Ugavi, Ukaguzi wa Ndani, Huduma za Sheria na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA). **TAASISI ZILIZOCHINI YA WIZARA YA UCHUKUZI** Wizara ya Uchukuzi inasimamia jumla ya Taasisi 15, kati ya hizo, Mamlaka za udhibiti ziko nne (4); Taasisi za Utendaji ziko nane (8); Vyuo vya Mafunzo ya kisekta viwili (2); na Mabaraza ya Walaji ni mawili (2). Aidha, kuna vyuo vya Mafunzo ya kisekta vinne (4) vinavyosimamiwa moja kwa moja na Taasisi za kiutendaji. Mchanganuo wa Taasisi hizo ni kama ifuatavyo: **MAMLAKA ZA UDHIBITI** Mamlaka za Udhibiti zilizo chini ya Wizara ya Uchukuzi ni: - Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA); - Mamlaka ya Usafiri Ardhini (LATRA); - Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC); na - Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). **TAASISI ZA UTENDAJI** Taasisi za kiutendaji zinajumuisha Wakala, Mamlaka, Mashirika na Makampuni. Taasisi hizo ni kama ifuatavyo: - Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA); - Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA); - Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA); - Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL); - Shirika la Reli Tanzania (TRC); - Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL); - Kampuni ya Meli ya Tanzania na China (SINOTASHIP). **VYUO VYA MAFUNZO** Wizara ya Uchukuzi inasimamia Vyuo viwili (2) vinavyotoa mafunzo ya usafiri na usafirishaji ikiwa ni pamoja na mafunzo ya matengenezo ya vyombo vya usafiri hususani katika usafiri kwa njia ya Anga. kama ifuatavyo: - Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT); - Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) ; **VYUO VYA MAFUNZO VILIVYOCHINI YA USIMAMIZI WA TAASISI** Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Uchukuzi zinasimamia vyuo vinne (4) vinavyotoa mafunzo ya uchukuzi na hali ya hewa ikiwa ni pamoja na mafunzo ya wataalam katika ngazi ya fundi mchundo kama ifuatavyo : - - Chuo cha Hali ya Hewa, Kigoma - Chuo cha Reli, Tabora - Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC), Dar es Salaam - Chuo cha Bandari Dar es Salaam. **MABARAZA YA WATUMIAJI WA HUDUMA ZA USAFIRI** Mabaraza ya Watumiaji wa Huduma za Usafiri yanayofanya kazi kwa kushirikiana na Mamlaka za Udhibiti ni:- - Baraza la Watumiaji wa Huduma za Usafiri wa Anga (TCAA-CCC); na - Baraza la Watumiaji wa Huduma za Usafiri Ardhini (LATRA - CCC).
48dbfd51d360ddb4a19a049942af7a0346f91ffcf178e320f594a2525358054c
420
5.090476
10
2,138
1
0
0
0.238095
8.1
55
https://www.uchukuzi.go.tz/news/makamu-wa-rais-dkt-mpango-aweka-jiwe-la-msingi-kiwanja-cha-ndege-tabora
#### MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AWEKA JIWE LA MSINGI KIWANJA CHA NDEGE TABORA Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Philip Mpango ameipongeza Wizara ya Uchukuzi na Wizara ya Ujenzi kwa kusimamia vema mradi wa ujenzi wa jengo la abiria katika kiwanja cha ndege Tabora. Dr. Mpango ametoa pongezi hizo leo wakati aliweka jiwe la msingi katika jengo la abiria linaloendelea kujengwa katika kiwanja cha ndege Tabora. "Macho yangu yananiambia kuwa hapa tutapata jengo zuri kabisa, hakika ni jambo la kutia moyo kwamba fedha za wananchi zinatumika sawasawa na ilivyopangwa," Amesema Dr.Mpango. Awali akizungumza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Mhandisi Mohamed Besta,amesema mradi huo wa ujenzi umefikia asilimia 72, huku akibainisha kuwa jengo hilo linatarajiwa kuwa na sakafu ya chini na ya juu. Besta amesema kuwa katika sakafu ya chini jengo hilo linatarajiwa kuwa na ofisi za kampuni mbalimbali za ndege kwa ajili ya tiketi pamoja na eneo maalum la kupumzikia abiria. Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania Abdul Mombokaleo ameishukuru serikali kwa jitihada zake katika kuboresha usafiri wa anga uku akiahidi kuwekwa kwa mikakati bora ya kibiashara ambayo itakifanya kiwanja hicho kuwa na matokeo yaliyokisudiwa.
413897db2f988310a0b81c531f89eda6222f1d89512671ac843d6a2cacd7f69f
199
5.457286
7
1,086
1
0
0
0.502513
1.01
25
https://www.uchukuzi.go.tz/news/bilioni-37-zatumika-kiwanja-cha-ndege-songea
#### Bilioni 37 zatumika Kiwanja cha Ndege Songea erikali imesema takriban sh. Bilioni 37 zimetumika kufanya ukarabati na upanuzi wa miundombinu ya Kiwanja cha ndege cha Songea hatua ambayo itachagiza kuongezeka kwa safari za ndege ambazo zitakidhi soko la wasafiri wa anga wa mkoa wa Ruvuma. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa wakati alipokagua kiwanja hicho na kusema maboresho hayo ni chachu itakayosaidia safari za ndege kufanyka kila siku za wiki. “Kukamilika kwa uwanja wa ndege huu kumesababisha shirika letu la ndege kuanza safari zake za kawaida Air Tanzania sasa inakuja mara 3 kwa wiki tulitamani ije mara nyingi baadaa ya mara tatu labda tufanye ianze kufanya mara tano kwa wiki lakini baadae ianze kuja kila siku” Alisema Mbarawa. Pamoja na hilo Waziri Mbarawa amesema kwa sasa wananchi wataendelea kutumia jengo dogo la abiria wakati Serikali inaendelea kufanya mchakato wa ujenzi wa jengo la kisasa la abiria ambalo litaweza kutoa huduma bora kwa wananchi ambazo zitaendana na hadhi ya kiwanja hiko. Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed ameishukuru Serikali kwa kuimarisha sekta ya uchukuzi mkoani humo na kuendelea kutoa kipaumbele kwenye utekelezaji wa miradi iliyochini ya wizara hiyo. Naye Meneja wa Kiwanja hicho Dustan Komba amesema maeneo yaliyoboresha ni pamoja na njia ya kutua na kurukia ndege na kutoka urefu wa mita 1600 kwenda mita 1860, usimikaji wa taa za kuongozea ndege kwa ajili ya kuwezesha Ndege kutua sa 24. Maboresho mengoine ni pamoja na kituo cha kupokea nishati kwa maana ya maji na umeme, katika line ya umeme yenye msongo wa kilowatt 33 na lami ambayo inakidhi viwango na vigezo na yenye miundombinu toshelevu kwa ajili ya utuaji wa ndege.
0c61eae220039d0b47cd91f76b24d9a62f66a075b17393afa97fc7d66e3b5d26
281
5.185053
8
1,457
1
0
0
0.355872
2.85
43
https://www.uchukuzi.go.tz/news/mradi-wa-matenki-kupunguza-changamoto-ya-mafuta-nchini-prof-mbarawa
#### MRADI WA MATENKI KUPUNGUZA CHANGAMOTO YA MAFUTA NCHINI-PROF. MBARAWA Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame mbarawa ametembelea ujenzi wa matenki ya mafuta unaondelea jijini Dar es salaam maeneo ya Tungi kigamboni ambapo amesema kuwa matenki hayo yatakuwa 14 huku matenki sita yatakuwa ya dizeli na 5 yakiwa ni ya petrol. Akizungumza Jijini Dar es salam Mara baada ya kutembelea ujenzi huo Prof Mbarawa amesema kuwa mradi huu utagarimu kiasi cha Fedha shilingi Bilioni 678 na utaenda kuleta manufaa makubwa kwenye nchi yetu kwani mara baada ya kumalizika mradi huo tutapunguza changamoto za Mafuta. "Tunafahamu kuwa kwa sasa meli za mafuta zinachukua muda mrefu. Katika kuleta mafuta hii inatokana. Na upungufu wa matenki yaliyopo nchini pia mafuta hayo yakitolewa yanapelekwa kwenye vituo husika na sisi kama serikali tumeamua kujenga mantenki ili yawekewe mafuta na kupelekea wateja wetu. Aidha ameongeza kuwa mradi huu unaenda kutekelezwa Kwa Miaka 2 Miwili kutokana na hali za Mvua pia Mamlaka ya usimamizi wa bandari (TPA) kwa kushirikiana na wakandarasi Watasimamia ujenzi huo mpaka kukamilika na kuweza kukabidhi Rasmi. Natoa wito kwa wasimamizi wote ambao wamepewa kusimamia ujenzi huo kufanya kazi vyema na uwe mradi bora zaidi kwani serikali kupitia Dkt samia suluhu hassani ametoa fedha za kutosha kwa ajili ya kutekeleza mradi huo wa mantenki. Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya usimamizi wa bandari (TPA) Juma Kijavala amesema kuwa Mradi huo unaenda kutekelezwa kwa wakati ili huduma za mafuta ziweze kuendelea nchini. Naye Meneja wa Mardi huo. Mhandisi Hamisi Hassani amesema kuwa manteki hayo ya mafuta yatakuwa na ujazo wa 27 kwa Tenki moja la dizeli huku oil ikiwa ni 27 hivyo jumla ya ujazo itakuwa ni 378 pia mradi huu unaenda kupunguza kero ya mafuta ikiwemo bandarini na nitahakikisha mradi huu unaenda kuisha kwa wakati ambapo umepangwa. Vilevile Mstahiki Meya kutoka kigamboni na diwani wa kata ya Tungi Ernest Mafimbo ametoa pongezi kwa Serikali kwa kuweza kupeleka mradi huo kigamboni kwani itaenda kupelekea Ajira hususani kwa Vijana, Mama lishe pia sisi kama manispaa ya kigamboni tunaenda kupata manufaa kupitia mradi huo.
a355f432b0a44b6d03c3b2394a68f26449f9b5f0f6291e0c700a939625fe87d9
338
5.399408
11
1,825
1
0
0
0.295858
2.37
48
https://www.uchukuzi.go.tz/news/serikali-kujenga-gati-5-bandari-ya-dar-es-salaam
#### Serikali kujenga gati 5 Bandari ya Dar es Salaam Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema inakusudia kuongeza ukubwa wa Bandari ya Dar es Salaam kwa kujenga gati mpya tano zenye urefu wa mita 300 Kauli hiyo ya Serikali imetolewa leo tarehe 3 June 2024 na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt.Ally Possi alipofanya ziara katika Bandari ya Dar-es-Salaam ili kujionea mwenendo wa kazi. Dkt.Possi amesema eneo la Bandari ni dogo na kwahivyo Serikali inaangalia uwezekano wa kuongeza eneo la bandari ili kupata gati za kuhudumia meli nyingi zaidi na lengo likiwa ni kuifanya iwe 'hub' ya shughuli za kibandari katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA,Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam Bwa.Mrisho S.Mrisho amesema mpaka kufikia Aprili mwaka huu,Bandari ya Dar es Salaam ilikuwa imehudumia tani milioni 19.6 kiasi ambacho kinakaribia kuvuka lengo la kuhudumia tani milioni 22.
f3b04ee226bb76245c1bbc8c54a86174b2819a89aa396c16facc66a27ea5cb25
152
5.236842
3
796
1
0
0
0.657895
4.61
15
https://www.psptb.go.tz/pages/what-we-do?mid=34
# Tunafanya Nini Bodi ina jukumu la kusimamia viwango vya kitaalamu na maadili ya wataalamu katika nyanja za manunuzi na vifaa. Ili kutekeleza na kukamilisha jukumu hili, Sheria ya kuwezesha uwepo wa PSPTB imeipa mamlaka PSPTB kufanya yafuatayo: - Kutayarisha na kuishauri serikali juu ya sera na yanayohusiana na taaluma ya manunuzi na vifaa; - Kupanga, moja kwa moja, kuratibu, kufuatilia na kudhibiti wafanyakazi mahitaji katika manunuzi na vifaa na usimamizi wa taaluma; - Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa kutambua nakutoa mafunzo kwa taasisi zote za ndani ya nchi sadaka kozi katika manunuzi na vifaa na huduma za ushauri katika manunuzi na usimamizi vifaa , vifaa vya utunzaji, usambazaji, ufungaji, usimamizi wa kitaalamu, menejimenti ya mikataba na udalali; - Kuunda, kuanzisha na kutekeleza matengenezo ya viwango vya maadili na kusimamia shughuli za wataalamu wa manunuzi, vifaa vya wataalamu, wakaguzi manunuzi, vifaa na wakaguzi hisa, mafundi manunuzi na vifaa mafundi na mazoezi ya taaluma ya manunuzi na usimamizi vifaa ; - Kutoa mafunzo au kutoa fursa kwa ajili ya mafunzo ya watu katika kanuni; taratibu na mbinu ya manunuzi na usimamizi vifaa; - Kuendesha mitihani ya kitaaluma na na tuzo nyingine ya bodi katika manunuzi na vifaa, ukaguzi wa manunuzi, vifaa na hisa ukaguzi na masomo mengine yanayohusiana na manunuzi na usimamizi vifaa; - Ili kufanya usajili wa wataalamu wa manunuzi na vifaa; - Kuweka na kudumisha madaftari ya usajili wa wataalamu wa manunuzi na vifaa kwa mujibu wa PSPTB ; - Kutathmini sifa za kitaaluma na vitendo kwa lengo la usajili wa watu chini ya PSPTB ; - Kudhamini, kupanga na kutoa vifaa kwa ajili ya mikutano, semina, mijadala na mashauriano juu ya masuala yanayohusiana na manunuzi na vifaa vya usimamizi. - Kuagiza ada inayolipwa kwa Bodi - Ili kusaidia wanachama wa umma katika suala hilo kugusa juu
1dbc83d97b057f328dd3d14047395fe6a12e9d137d367e60b60079fc18fb4b9a
298
5.208054
3
1,552
1
0
0
0.33557
5.7
55
https://www.psptb.go.tz/pages/registration?mid=35
# Usajili USAJILI WA WATAALAMU, MAFUNDI NA MAKAMPUNI YA USHAURI Chini ya utoaji wa sehemu ya III ya Sheria Namba 23 ya 2007, mtu utambuliwe na haki ya kufanya mazoezi kama mtaalamu wa Ununuzi na Ugavi au fundi ikiwa mtu huyo ni amesajiliwa kihalali chini ya Sheria. Kwa mujibu wa Sheria Namba 23 ya 2007, Bodi inalo daftari la usajili kama ifuatavyo: - - Kujiandikisha kwa ajili ya Ununuzi na Ugavi Wataalamu Watu wanaostahili kuandikishwa kama mtaalamu manunuzi na vifaa lazima mtu ambaye ni mmiliki wa CSP, CPSP, CIPS, shahada, stashahada ya juu au tuzo nyingine kuhusiana. - Kujiandikisha kwa mtaalamu wa ufundi wa Ununuzi na Ugavi Watu wanaostahili kuandikishwa katika ufundi wa manunuzi na vifaa lazima mtu ambaye ni mmiliki wa Professional I au II, diploma au cheti au tuzo nyingine kuhusiana. Utaratibu wa usajili mtu ambaye anataka kupata usajili chini ya Sheria ya PSPTB, atawasilisha maombi katika fomu kwa Mkurugenzi Mtendaji akiambatanisha na: - - nakala ya hati au nakala za vyeti kwa sifa za kitaaluma wa mwombaji. - ada ya maombi kama ilivyoelekezwa. - Nyaraka nyingine kama atakavyoelekezwa na Bodi. - Maendeleo ya Taaluma (CPD) Hii ni sehemu ya mahitaji ya uanachama. Shughuli hii lengo la kuweka wanachama uwezo wa kujiendeleza na maendeleo ya karibuni katika taaluma na mahitaji katika sekta hii. Maarifa na ujuzi ni muhimu kwa wataalamu yanapotolewa katika nyanja ambapo wataalamu kutoka sekta mbalimbali wanadilishana uzoefu. Kila mwanachama mtaalamu analazimika kuwa na angalau masaa 40 ya CPD kwa mwaka
46e92dc1bc546ecd30516b5b6f926599dc289badd7b7ba3d2006c318d7a4ce27
245
5.228571
10
1,281
1
0
0
0.408163
5.71
43
https://www.psptb.go.tz/pages/examination-centres?mid=58
# Vituo vya Kufanyia Mitihani Kuna vituo ambapo mafunzo ya muda mfupi na muda mrefu huendeshwa nchi nzima Matokeo ya Mitihani na utoaji wa vyeti Matokeo mitihani yatawasilishwa kwa maandishi baada ya Bodi kuyapitia na kutoa idhini. Kauli ya Matokeo kwa kila somo itapelekwa moja kwa moja na mtahiniwa.Mtahiniwa atapewa tuzo ya cheti cha awali cha Ununuzi na Ugavi baada ya kumaliza mitihani katika ngazi hii. Cheti cha Foundation juu ya mafanikio ya kumaliza ngazi ya Foundation na juu ya mafanikio ya kumaliza ngazi nne zaProfessional ikiwa ni pamoja na andiko la tafiti ambalo huwa ni tuzo kigezo cha ya Mtaalamu kuthibitishwa na kupewa CPSP
2af407b422ff6d8d00ff034f86fd07444ae04580f55dee8aa8c57d4bcd1963df
105
5.133333
3
539
1
0
0
0.952381
0.95
23
https://www.psptb.go.tz/pages/research-consultancy?mid=38
# Ushauri wa Utafiti Huduma ya ushauri Miongoni mwa kazi nyingine za Bodi ni kazi ya kutoa ushauri wa kitaalamu kwa kutoa mafunzo ya aina zote kwa Taasisi za ndani ya nchi, huduma za ushauri katika manunuzi na usimamizi vifaa, usimamizi wataalamu, menejimenti ya mikataba na udalali. Katika kufikia kazi hii, Bodi hutoa huduma ya ushauri katika manunuzi na vifaa usimamizi kuhusiana na yafuatayo: - Kujenga uwezo wa manunuzi na Ugavi wataalamu kupitia mafunzo ya ndani - Kutoa ushauri kuhusiana na manunuzi ya vifaa na wataalamu - Kutoa ushauri juu ya ununuzi na vifaa kada - Utoaji wa huduma ya ushauri kwa watoa maamuzi juu ya masuala ya ujumla kuhusiana na taaluma ya manunuzi na vifaa. - Kutoa wateja na huduma za kitaalamu na ushauri katika maeneo ya Ununuzi na Ugavi - Utoaji wa huduma yoyote ya ushauri kuhusiana na manunuzi na usimamiza vifaa - Huduma za utafiti Bodi kuwa na kazi ya kutunga na kuishauri Serikali juu ya sera kwa ujumla zinazohusiana na taaluma ya manunuzi na vifaa. Kazi hii inaweza kupatikana kwa njia: - Kuandaa tafiti za mafunzo - Kufanya utafiti wa kitaalamu kuhusiana na manunuzi na vifaa vya usimamizi. - Kuendeleza mahusiano ya kimitandao na kuaandaa na wafanya tafiti wa nje ya nchi ili kuboresha shughuli za utafiti - Kukuza wataalamu ili kuwa na mwenendo tafiti kuhusiana na manunuzi na vifaa wataalamu - Kuandaa agenda za tafiti mbalimbali zinazoendelea - Kuchapisha utafiti - Kuandaa na kuchapisha jarida / makala
36edff3ab91abea03389020f14ad4276b3fbf9515d88f4355c61c038bdfaf28a
242
5
5
1,210
1
0
0
0.413223
6.61
40
https://www.psptb.go.tz/pages/research-methodology?mid=97
# Utafiti HABARI MPYA RESEARCH PROPOSAL DEFENSE RESULTS-SEPTEMBER 2024 Research Proposal Defense Results september 2024 LIST OF CANDIDATES TO DEFEND RESEARCH PROPOSALS List of Candidates to Defend Research Proposals -November 2024 28TH PSPTB PROFESSIONAL EXAMINATIONS- RESEARCH PROPOSAL RESULT Research Candidates External marking Scores & Oral Research Time Table Approved Research Activities Action Plan (January To June) 2024 (1) TAARIFA KWA UMMA- UFAFANUZI MAALUM KWA WATAHINIWA WA TAFITI Ufafanuzi Maalum Kwa Watahiniwa wa Tafiti **FIVE (5) DAYS TRAINING ON COMPREHENSIVE RESEARCH METHODOLOGY**RESEARCH METHODOLOGY TRAINING FROM 26TH FEBRUARY TO 01 MARCH, 2024 **A) DAYS TRAINING ON COMPREHENSIVE RESEARCG METHODOLOGY** **RESERCH METHODOLOGY TRAINING FROM 21ST TO 25TH AUGUST, 2023.** **B) 2ND BATCH RESEARCH PROPOSAL RESULTS MAY 2023** **SECOND BATCH FOR RESEARCH PROPOSAL RESULTS.** **C) RESEARCH PROPOSAL RESULTS FOR 26TH BOARD'S** EXAMINATIONS RESEARCH PROPOSAL RESULTS FOR 26TH BOARD'S EXAMINATIONS HABARI ZA ZAMANI Final Research activities ACTION PLAN JAN - JUNE 2023 RESEARCH METHODOLOGY TRAINING FROM 20TH TO 24TH FEBRUARY, 2023. Bodi huendesha warsha za Tafiti mara mbili kwa mwaka kwa walengwa wafuatao; WALENGWA: - Watahaniwa wote waliofaulu mitihani ya ngazi ya tano ya PSPTB - Watahiniwa wote wa Mitihani ya Novemba 2019 wanaosubiri matokeo yao - Wanafunzi wa Vyuo Vikuu, Wahadhiri, Wahadhiri Wasaidizi na Wakufunzi mbalimbali - Watafiti kutoka Asasi mbalimbali na Taasisi za Mafunzo - Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi Na wadau wengine MALENGO NA FAIDA: - Kupata ujuzi wa kufanya Tafiti za Kibiashara - Kuandaa andiko la Utafiti na baadaye ripoti ya Utafiti - Kujengewa weledi wa kukusanya taarifa, kuchakata taarifa, majadiliano na kutafsiri matokeo ya tafiti - Kujengewa uwezo wa kuandika ripoti za Tafiti na kujieleza - Kupewa cheti cha mahudhurio
2095dfb6ea38d2557c5c18094b4c31fe0ef0de06c1808f996c249f6c15a9d2d4
270
5.914815
4
1,597
1
0
0
0.37037
9.63
12
https://www.psptb.go.tz/pages/sit-for-board-s-examination
# KUFANYA MITIHANI YA BODI **MUUNDO WA PROGRAMU YA MITIHANI** **1.****Utangulizi** Mitihani ya taaluma ya Bodi hufanywa mara mbili kila mwaka yaani, Mei na Novemba na imegawanywa katika ngazi kuu tatu nazo ni Cheti cha Awali, (Basic Stage), Cheti cha Msingi (Foundation Stage) na Shahada ya juu ya Ununuzi na Ugavi (CPSP). Katika kila ngazi za mitihani za mwanzo kila moja ina hatua mbili ambazo zimeundwa kikamilifu ili kupima uelewa, maarifa na ustadi kwa watahiniwa husika katika kufanya kazi za ununuzi na ugavi kuendana na viwango vilivyokusudiwa. Muundo wa mitihani ya shahada ya juu unazo hatua tano (Professional Stage I - V) zilizoundwa kikamilifu ili kumwezesha mtahiniwa kuwa na maarifa na ujuzi wa kitaalamu ili kuleta tija katika ufanyaji kazi za ununuzi na ugavi katika hatua husika. Kila somo lililomo katika kila hatua za mitihani zilizotajwa humjengea mtahiniwa maarifa na ujuzi ya kumsaidia kuendelea hatua inayofuata. Kama sehemu ya mtihani, watahiniwa wa ngazi ya juu yaani CPSP baada ya kufaulu mitihani ya hatua ya mwisho (professional stage V) watahitajika kufanya utafiti katika eneo la ununuzi na ugavi na kuwasilisha andiko la utafiti (research paper) kwa Bodi ndani ya kipindi cha miaka miwili kwa ajili ya kusahihishwa. **2.****Yaliyomo kwenye muundo wa mitihani ya Bodi** Katika mitihani ya Cheti cha Awali na Cheti cha Msingi kuna jumla ya masomo matano ya msingi *(core subjects)* na masomo tisa wezeshi *(supporting subjects)* ambayo yameandaliwa na kuunganishwa kikamilifu ili kuwapa wanafunzi ujuzi na ustadi unaohitajika. Mitihani ya Cheti cha Awali inajumuisha hatua mbili kila moja ikiwa na masomo matatu ambapo ukamilifu wake unakusudia kumuandaa **“Technicians” **katika kada ya ununuzi na ugavi**.** Mitihani ya Cheti cha Msingi ina hatua mbili kila moja ina masomo manne, ambapo ukamilifu wake unakusudia kumuandaa **“Full Technicians” **katika kada ya ununuzi na ugavi. Kama ilivyoelezwa awali, mitihani ya ngazi ya juu imegawanywa katika hatua tano, zenye masomo kumi na tano (15) ya msingi *(core subjects)* na masomo matano (5) wezeshi *(supporting subjects)* na yakifuatiwa na somo moja la kufanya utafiti. Mpango huu umekusudiwa kutoa wahitimu wenye uwezo wa kufanya kazi za ununuzi na ugavi katika viwango vya chini, kati na juu hususani usimamizi wa ununuzi na ugavi. Kupata ufupisho wa muundo wa mitihani ya PSPTB, tafadhali bonyeza na fungua kiungo hapa chini chenye maelezo mahususi. NB: Nakala ngumu ya mtaala inapatikana katika ofisi za PSPTB kwa gharama za Shilingi ya Tanzania 5,000 / =
0d524dd5a77f6821570bd5801a019cc5b7fa23c0af91a01b711b462b3bc3ba80
393
5.470738
14
2,150
1
0
0
0.254453
1.78
65
https://www.basata.go.tz/administration/members/gervas-andrew-kasiga
Barua pepe Wasiliana nasi Maswali ` Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Baraza la Sanaa la Taifa Mwanzo Kuhusu sisi Mamlaka Dira na Dhima Historia Utawala Muundo wa Taasisi Wajumbe wa Bodi Menejimenti Idara Huduma za Taasisi Ukuzaji na Maendeleo ya Sanaa Vitengo Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani Kitengo cha Huduma za Sheria Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano Kitengo cha Manunuzi Kitengo cha Tehama na Takwimu Wafanyakazi Machapisho Sheria Kanuni Jarida Vipeperushi Miongozo Tafiti na Takwimu Ripoti Mpango Mkakati Fomu Kituo cha habari Habari Taarifa kwa Umma Maktaba ya picha Maktaba ya Video Mifumo Amis Barua pepe za watumishi Huduma Zetu Usajili na Ada Programu Basata Vibes Sanaa Mtaa kwa Mtaa Sanaa kwa Watoto Notisi Nyimbo Zilizozuiliwa Wasanii waliofungiwa Kumbi zilizofungiwa Vikundi vilivyofungiwa Barua pepe Wasiliana nasi Maswali Home administration members gervas-andrew-kasiga Dkt. Gervas Andrew Kasiga Dkt. Gervas Andrew Kasiga Mjumbe Barua pepe: [email protected] Simu: Wasifu Mjumbe Settings Language Kiswahili English Color Dark Light Default Text Small Normal Large
979a73c2c866a10296134bc067bf7453a9779e1e150d4c7dde0f646c3b58075a
158
5.835443
3
922
1
0
0
0
0.63
16
https://www.basata.go.tz/news/wasanii-jirasimisheni-mpate-fursa
14 Juni, 2024 Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe Dkt. Damas Ndumbaru leo tarehe 14 Juni, 2024 amehimiza wasanii kujiraismisha ili kurahisisha mipango ya serikali ya kuwatafutia fursa mbalimbali kwakuwa sanaa ni ajira inayoingiza kipato halali. Ameyasema hayo wakati anazungumza na watu mashuhuri wakati wa hafla maalum ya kujadiliana mchango wa celebrities katika kujenga afya ya bora ya akili na maadili katika kazi za sanaa kwenye ukumbi wa Serena jijini Dar es salaam. Mhe. Waziri ameongeza kuwa, serikali ya awamu ya sita imekuwa Mstari wa mbele kupambania maendeleo ya wasanii ndo mana imefufua mfuko wa utamaduni ambao unawawezesha wasanii ambapo hadi sasa umefanikiwa kutoa kiasi cha fedha shilingi Bilioni 4.2 kwenda kwa wasanii mbalimbali nchini. Juu ya hapo, tunapaswa kumshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mahaba anayoendelea kuyaonesha kwenye tasnia ya Sanaa kwani kupitia hotuba yake wakati wa tukio la uzinduzi wa albamu ya Msanii Harmonize ametamka rasmi kuambatana na wasanii katika ziara zake ili kuwafungulia fursa za soko la Kimataifa. Hayo yote yanawezekana kufanyika kwa usahihi na ufanisi kulingana na utayari wa kujiweka katika mfumo rasmi hivyo amewasihi wasanii wote kujirasimisha kwa wakati ili muda utakapofika usirukwe kwa sababu za uzembe. Mwisho, amewapongeza wasanii waliohudhuria mafunzo pamoja na watoa mada katika mkutano maalum ambapo makala zote zilizofundishwa kuhusu afya bora ya akili, mikataba katika kazi za sanaa, uzingatiaji wa maadili katika kazi za sanaa na usalama na uzalendo wa nchi yanaakisi maendeleo ya sekta ya sanaa nchini.
9806e95cacb3928f6ca54007ca7ca6b29b6ff47c1f835c51b41e56db7aac9774
241
5.618257
10
1,354
1
0
0
0
2.07
37
https://www.michezo.go.tz/department
#### Departments ##### Idara ya Maendeleo ya Utamaduni **MAJUKUMU YA IDARA YA MAENDELEO YA UTAMADUNI** - Kutunga na kusimamia, kutathmini na kupitia utekelezaji wa sera za maendeleo ya utamaduni sheria,kanuni na miongozo mbali mbali. - Kusimamia na kuratibu utendaji kazi wa taasisi za kiutamaduni zilizo chini ya wizara. - Kuanzisha na kuibua programu za ushirikiano na ubadilishanaji wa maarifa,uzoefu na ujuzi wa kiutaduni baina ya Tanzania na Mtaifa mengine. - Kutoa tuzo kwa kazi za utamaduni kupitia matukio ya kiutamaduni. - Kutoa miongozo mbalimbali kuhusiana na misingi ya maadili ya Taifa. - Kukuza,kuwezesha na kuratibu ujenzi wa uwezo wa rasilimali watu ya kiutamaduni kwa kushirikiana na waajiri wa karibu. - Kuanzisha mbinu za kuendeleza, kutangaza masuala ya mila, desturi na lugha; - Kutoa ushauri juu ya masuala yanayohusiana na maadili katika kuandaa sinema, filamu/uigizaji, maonesho na utoaji wa leseni katika maeneo hayo. - Kuratibu na kushiriki matukio, semina, warsha, makongamano na mafunzo mbalimbali yanayohusu utamaduni na lugha. - Kuwezesha upatikanaji wa fedha kwa watendaji wa kazi za utamaduni. **Idara ya Maendeleo ya Utamaduni ina sehemu kuu mbili.** - Sehemu ya urithi wa utamaduni na maadili ya Taifa. - Sehemu ya Lugha. **1. Majukumu ya sehemu ya urithi wa utamaduni na maadili ya Taifa.** - Kuendeleza, kutafuta, kutathmini na kupitia upya utekelezaji wa sera na sheria za utamaduni za kitaifa. - Kuunda, kuendeleza na kutekeleza mikakati na miongozo kwaajili ya kukuza ubunifu wa utamaduni wa jadi na kitaifa na kufanya kazi na kuisambaza. - Kutetea utekelezaji wa sera ya utamaduni wa kitaifa kwa ajili ya kukuza utamaduni na utambulisho wa Taifa. - Kuandaa na kutoa miongozo ya ujumuishaji wa kanuni na maadili ya kitamaduni katika mipango ya maendeleo ya kijamii,kiuchumi na kisiasa na kufuatilia na kutathmini utekelezaji wake. - Kusoma na kuamua mila mbalimbali zinazokuza na kuathiri maendeleo ya utamaduni wa Taifa. - Kuendeleza mifumo ya kukuza programu za kubadilishana utamaduni wa kimataifa. - Kufanya utafiti na kuandaa orodha ya mila na desturi zinazokubalika na zisizokubalika zinazoathiri maendeleo ya Taifa. - Kuandaa miongozo ya uundaji na usimamizi wa vikundi vya kitamaduni nchini na kufuatilia na kutathmini utekelezaji. - Kuhifadhi utafiti, kumbukumbu na kukuza historia ya mapambano ya ukombozi wa mwafrika nchini Tanzania. - Kuratibu shughuli za utafiti wa mila na desturi. - Kuandaa na kuratibu matukio ya Tamasha za kiutamaduini zinazofanyika nchini. - Kuhamasisha wadau kuanzisha miundombinu ikiwa ni pamoja na Makumbusho, Kituo cha utamaduni, kumbi za kudumu za maonyesho ya utamaduni na warsha za ufundi na bidhaa asilia. - Kushauri juu ya tathmini ya athari za kiutamaduni zinazohusiana na miradi ya maendeleo. - Kuendesha na kuratibu kampeni ya elimu ya juu ya maadili. **2. Majukumu ya sehemu ya lugha.** - Kuendeleza, kufuatilia, kutathmini na kupitia upya utekelezaji wa sera ya utamaduni wa kitaifa (Lugha). - Kuendeleza na kutekeleza mikakati na taratibu za kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili katika utawala wa serikali, elimu, siasa, jumuiya ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani. - Kuandaa na kusambaza sheria na miongozo ya utekelezaji wa sera ya utamaduni (Lugha). - Kutetea utekelezaji wa sera ya utamaduni ili kukuza lugha ya Kiswahili kwa ajili ya kukuza Sanaa za jadi na zisizo za jadi. - Kuwezesha,Kufuatilia na kutathmini utendaji kazi wa BAKITA na Kamisheni ya Kiswahili ya Afika Mashariki - Kuandaa na kutoa miongozo mbalimbali juu ya uanzilishaji na uendeshaji wa vyama vya lugha na fasihi pamoja na kusimamia utekelezaji wake. - Kuandesha na kuratibu semina na warsha kwa vyombo vya habari kuhusiana na matumizi fasaha ya lugha ya Kiswahili. - Kuandaa na kuratibu mipango mikakati ya kuendesha tafiti, uchapishaji na utunzaji wa nyaraka mbalilmbali kuhusiana na lugha za makabila kwa ajili ya kukuza istilahi na msamiati wa lugha ya Kiswahili. - Kuhamasisha na kuratibu uanzishaji wa vituo vya kufundisha lugha ya Kiswahili ndani na nje ya nchi (kwenye Balozi za Tanzania). ##### Idara ya Maendeleo ya Sanaa Idara ya Maendeleo ya Sanaa imeundwa baada ya muundo mpya wa Wizara. Kabla ya hapo Idara ilikuwa ni sehemu ndani ya Idara ya Maendeleo ya Utamaduni. Kwa mwaka wa fedha 2016/2017 idara ilitekeleza majukumu yake ikiwa pamoja na Idara ya Maendeleo ya Utamaduni. Idara ya Sanaa ndiyo yenye dhamana ya kusimamia maendeleo ya Sekta ya Sanaa nchini. Sanaa hizo ni pamoja na filamu, muziki, michezo ya kuigiza, ngoma, dansi, sarakasi na kazi za mikono kama vile uchoraji, uchongaji, uhunzi, usukaji, ufumaji, ushonaji na ususi. Idara ya Sanaa inajukumu la kusimamia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA) na Bodi ya Filamu Tanzania. Idara ya Maendeleo ya Sanaa imegawanyika katika kuu sehemu mbili;- 2.** Sehemu ya haki na Maendeleo ya wasanii **(Sehemu hizi zitaongozwa na Wakurugenzi wasaidizi wawili 2) **MAJUKUMU YA IDARA YA MAENDELEO YA SANAA** Majukumu ya Idara ya Maendeleo ya Sanaa ni haya yafuatayo;- I.Kusimamia na kuratibu uandaaji wa Sera ya Maendeleo ya Sanaa. II.Kuandaana kutoa miongozo ya kusimamia utekelezaji wa shughuli za Sanaa na Ubunifu. III.Kuendeleza, kufuatilia, kutathmini na kurekebisha utekelezaji waSheria na Miongozo ya Sera ya Sanaa, **MAJUKUMU YA SEHEMU YA URATIBU WA TASNIA YA SANAA** Majukumu ya Sehemu ya Uratibu wa Tasnia ya Sanaa ni:- i.Kuendeleza, Kuratibu na kutekeleza mbinu za kiutendaji za shughuli za sanaa . ii.Kuendeleza, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa sera ya kitaifa ya sanaa, sheria na miongozo katika muziki, sanaa za maonesho na ubunifu kwa ujumla. iii.Kudhibiti na kusisitiza matumizi ya maadili ya kitaifa katika shughuli za muziki, sanaa za maonesho na ubunifu kwa jumla . iv.Kuratibu na kuendeleza mifumo ya kutambua na kutoa tuzo kwa wasanii na taasisi bora katika kutekeleza shughuli za maendeleo ya sanaa. v.Kuratibu na kusimamia taasisi za sanaa za Tanzania, wanamuziki, sanaa za maonyesho, na wataalamu wa sanaa wanaofanya vizuri katika Tasnia. vi.Kufuatilia na kutathmini majukumu nakazi ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSuba), bodi ya Ukaguzi wa filamu na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA). vii.Kuratibu na kusimamia nakutoa miongozo yautekelezaji wa Sera ya Taifa ya filamu. MAJUKUMU YA SEHEMU YA HAKI NA MAENDELEO YA WASANII. Majukumu ya Sehemu ya haki na Maendeleo ya Wasanii ni:- i.Kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa Programu mbalimbali za wasanii. ii.Kuratibu na kusimamia mikataba ya wasanii na kazi zao iii.Kuratibu na kutoa ujuzi wa ujasiriamali na kitaaluma. iv.Kuratibu, kubuni na kutekeleza miradi ili kukuza wasanii na kazi zao. v.Kuratibu makundi ya sanaa, vyama na mashirikisho. vi.Kuratibu, kusimamia, kudhibiti na kutoa miongozo ya ulinzi wa kazi za wasanii ikiwa ni pamoja na haki miliki. vii. Kuratibu na kufuatilia haki za wasanii kwa kushirikiana na taasisi inayohusikana hakimiliki na hakishiriki. ##### Idara ya Maendeleo ya Michezo To provide expert**IDARA YA MAENDELEO YA MICHEZO** **1.****Utangulizi** Sekta ya Michezo hapa nchini imekuwa ikisimamiwa na Sera ya Maendelo ya Michezo yam waka 1995. Malengo ya Sera hiyo ni pamoja na kuhamasisha Umma wa Watanzania kushiriki katika Michezo na mazoezi ya viungo; kuwezesha upatikanajio wa Viwanja na zana bora na za kutosha kwa ajili ya kuimarisha Maendeleo ya Michezo nchini, kuandaa na kutayarisha wataalamu wa kutosha katika fani na taaluma mbali mbali za Michezo ya Kimataifa. Malengo mengine ni kuimarisha ushirikiano wa Kimataifa katika utoaji wa Elimu kwa Michezo na kuimarisha utafiti katika Michezo ya jadi kwa lengo la kuiendeleza. Idara ya Maendeleo ya Michezo ndipyo chombo cha juu cha Wizara ambacho kinasimamia utekelezaji wa Sera hiyo hapa nchini Tanzania. **2.****Majukumu ya Idara ya Maendeleo ya Michezo.** Katika kuhakisha Tanzania inanufaika na Sekta ya Michezo, Serikali ilitunga Sera ya Maendeleo ya Michezo yam waka 1995 ambayo ilibainisha malengo mbali mbali ya kutekelezwa kupitia mgawanyo wa majukumu yaliyobainishwa na Sera hiyo kama ifuatavyo: (i)Uhamasishaji kwa Umma wa Tanzania kushiriki katika Michezo na mazoezi ya viungo vya mwili (ii)Upatikanaji wa viwanja vya kutosha kwa ajili ya kuimarisha maendeleo ya Michezo (iii)Upatikanaji wa zana bora za Michezo ili kuimarisha Michezo (iv)Uuandaaji na utayarishaji kwa Wataalamu wa kutosha katika fani na taaluma mbali mbali za Michezo (v)Kuhakikisha Timu na wachezaji wanafanya vizuri katika Michezo na Mashindano ya Kimataifa (vi)Utafiti katika Michezo ya Jadi kwa lengo la kuifufua na kuindeleza. (vii)Ushirikiano na Mataifa mengine katika utoaji wa Elimu kwa Michezo na Michezo (viii)Mgawanyo wa Majukumu katika utekelezaji wa Sera **3.****Muundo wa Idara ya Maendeleo ya Michezo** Idara ya Maendeleo ya Michezo imegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni sehemu ya maendeleo ya Michezo na sehemu inayoshughulikis maendeleo ya miundo mbinu ya Michezo. Kwa mujibu wa Muundo wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Micheo. Idara ya Maendeleo ya Michezo ina Taasisi mbili ambazo zinafanya kazi na Idara. Taasisi hizo ni; chuo cha Maendeleo ya Michezo Mlya na Baraza la Michezo la Taifa (BMT). i.Baraza la Michezo la taifa ni Taasisi iliyoundwa kwa ksheria ya Bunge ya Na.12 ya mwaka 1967. Kwa mujibu wa sheria hiyo Baraza lina majukumu yafuatayo ii.Kuvisaidia na kuviendeleza vyama vya Michezo kwa kuandaa mafunzo kwa viongozi wa vyama na vilabu vya Michezo iii. Kutoa ushauri kwa vyama vya Michezo juu ya ujenzi wa viwanja vya Michezo iv.Kutafuta vifaa vya Michezo na kuvisambaza kwa wanaohitaji v.Kuandaa utaratibu wa kujenga uhusianio wa kimichezo kati ya Vyama vya Michezo na Wachezaji wenyewe vi.Kuchambua na kuthibitisha ratiba za masshindano ya Michezo zinazoandaliwa na vyama vya Michezo vii.Kuandaa Tamasha la Michezo kitaifa kwa kushirikiana na vyama vya Michezo viii.Kuishauri Wizara juu ya uhusiano wa kimichezo na Mataifa mengine ix.Kuandaa na kutekelez mbinu mbali mbali za kusisimua mwamko wa Michezo kwa ujumla, kama vile kutenegeza na kutoa medali za Michezo, kutoa misaada au nafasi za mafunzo ya Michezo (Scholarship), kuendesha zahanati za Michezo x.Kuhakikisha kuwa fedha za vyama vya Michezo zinakaguliwa na matumizi mabaya ya fedha yanaondolewa katika vyama hivyo.ise and services in policy formulation, implementation, monitoring and evaluation ##### Administration and Human Resource Management Division Objectives To provide expertise and services on human resources management and administrative matters to the Ministry. Functions To provide strategic inputs to management on Administration and Human resources Management issues To provide link between the Ministry and the President’s Office Public Service Management on operationalization of the Public Service Management and Employment Policy of 1998 and Public Service Act No. 8 of 2002 The Division is led by the Director and comprise two Sections as follows; Administration Section Human Resources Management Section ##### Idara ya Sera na Mipango **UTANGULIZI** Idara ya Sera na Mipango inatekeleza majukumu yake kupitia Sehemu ya Sera, Sehemu ya Mipango na Bajeti na Sehemu ya Ufuatiliaji na Tathimini. **MAJUKUMU YA IDARA YA SERA NA MIPANGO** Kazi kuu ya Idara hii ni kuratibu shughuli zote zinazotekelezwa na Wizara. Aidha, Idara hii hutoa utaalamu na huduma kwa masuala ya utungaji, utekelezaji, kufuatilia na kutathmini Sera za Wizara. Vilevile, Idara hii ni kiunganishi kati ya Idara na Vitengo vyote Wizarani. Majukumu mengine ni pamoja na: - Kuratibu utungaji wa Sera za Wizara, kufuatilia utekelezaji wake na kufanya tathimini; - Kuchambua nyaraka mbalimbali kutoka Asasi nyingine na kushauri juu ya nyaraka hizo; - Kuratibu maandalizi na utekelezaji wa Mipango na Bajeti ya Wizara; - Kufanya Ufuatiliaji na Tathimini ya Mipango na Bajeti na kuandaa taarifa ya utekelezaji; - Kufanya utafiti, tathimini ya mipango ya Wizara na kutoa uamuzi wa mwelekeo wa mbele wa Wizara; - Kumotisha na kuwezesha utoaji wa huduma kwa Wizara kwa kutumia sekta binafsi; - Kuratibu maandalizi ya michango ya Hotuba za Bajeti na Taarifa za Uchumi za mwaka za Wizara; - Kujenga uwezo wa Mpango Mkakati, Bajeti, Ufuatiliaji na Tathimini katika Wizara; na - Kuhakikisha kuwa Mipango na Bajeti za Wizara inajumuishwa katika Mipango na Bajeti za Serikali **UONGOZI NA UTAWALA** Idara ya Sera na Mipango inaongozwa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango na kusaidiwa na Wakurugenzi Wasaidizi kwa kila sehemu. ##### Procurement and Supply FUNCTIONS OF PROCUREMENT MANAGEMENT UNIT Objective To provide expertise and services in procurement, storage and supply of goods and services for the Ministry This Unit will perform the following activities: - - Develop an Annual Procurement Plan for the Ministry - Advise the Management on matters pertaining to procurement of goods, services and logistics management - Monitor adherence to procurement process and procedures as per Public Procurement Act - Procure, maintain and manage supplies, materials and services to support the logistics requirement of the Ministry - Maintain and monitor distribution of office supplies and materials - Provide Secretariat to the Tender Board as per Public Procurement Act; and - Set specifications/standards for goods and services procured and monitor
c98728845aaa55e7020a15b07b72469bc708018c1e95e4e57fce724023d50093
2,017
5.576103
85
11,247
1
0
0
0.34705
3.57
274
https://www.michezo.go.tz/pages/about-us
#### Who we are Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo iliundwa Kupitia Tangazo la Serikali Na.782 lililochapishwa katika Gazeti la Serikali la tarehe 22 Novemba, 2021. Katika kutekeleza majukumu yake kikamilifu, Wizara kimuundo imegawanyika katika maeneo makuu mawili ambayo ni: i. Usimamizi na utekelezaji wa masuala ya kisekta ii. Uendeshaji, uratibu na usimamizi USIMAMIZI NA UTEKELEZAJI WA MASUALA YA KISEKTA Eneo hili linatekelezwa na Idara ya Maendeleo ya Utamaduni, Idara ya Maendeleo ya Sanaa na Idara ya Maendeleo ya Michezo kwa ushirikiano na Taasisi zilizopo chini ya Idara hizo. UENDESHAJI URATIBU NA USIMAMIZI Eneo hili linatekelezwa na Idara ya Sera na Mipango, Idara ya Utawala na Rasilimali Watu,Kitengo cha Fedha na Uhasibu, Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Kitengo cha Ununuzi na Ugavi, Kitengo cha Huduma za Sheria na Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano pamoja na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini. Kuendeleza utambulisho wa Taifa kwa kuwezesha upatikanaji mzuri wa Habari,Kukuza Utamaduni na Michezo kwa Maendeleo ya Jamii na Uchumi. MAJUKUMU YA WIZARA Ili kufanikisha majukumu yake Wizara inatekeleza Sera za Utamaduni na Michezo pamoja na Malengo yake. SERA YA MAENDELEO YA UTAMADUNI YA MWAKA 1997 Malengo yake: i. Kushirikisha shughuli za Utamaduni wa Taifa kuanzia Shule za Awali, Sekondari na Elimu ya Juu na kuhakikisha kwamba mafunzo ya Utamaduni yanaingizwa katika Mitaala na muhtasari na kufundishwa shuleni na vyuoni. ii. Kuhimiza na kukuza utaifa kwa vijana wetu na wananchi kwa ujumla. iii. Kuhimiza Utu katika Maendeleo ya Taifa. iv. Kuimarisha Uchangiaji wa gharama, Ukuzaji, Utunzaji na Uimarishaji wa Taasisi za Utamaduni kwa watumiaji wa huduma hizo. v. Kuelimisha jamii juu ya masuala mbalimbali yanayohusu Utamaduni na jinsi sanaa inavyoweza kutumika katika kupambana na UKIMWI. SERA YA MAENDELEO YA MICHEZO YA MWAKA 1995 Malengo yake ni: i. Kuhamasisha wananchi kushiriki michezo na mazoezi ya viungo vya mwili ili kuimarisha afya zao. ii. Kuhakikisha timu na wachezaji wetu wanashiriki kikamilifu katika mashindano na michezo ya kitaifa na kimataifa. iii. Kufanya utafiti wa Michezo ya Jadi kwa lengo la kuifufua na kuiendeleza. iv. Kuimarisha ushirikiano na mataifa mengine katika utoaji wa elimu kwa michezo na wanamichezo. v. Kusimamia ujenzi wa miundombinu ya kisasa katika Sekta ya Michezo. vi. Kuimarisha Utawala bora katika michezo. vii. Kutoa Mafunzo ya wataalamu wa michezo. viii. Kupambana na Janga la UKIMWI katika michezo. ix. Kuendeleza na kutambua vipaji vya vijana katika michezo kuanzia umri mdogo. SEKTA YA MAENDELEO YA UTAMADUNI SEKTA YA MAENDELEO YA SANAA SEKTA YA MAENDELEO YA MICHEZO
14f79fb4ca8cbc53b8a0f9144f5ecb3284280b18b9d9c6cab3ec1687d6c420ed
403
5.590571
31
2,253
1
0
0
0.248139
1.24
65
https://www.michezo.go.tz/unit
#### Unit - Kuandaa na kulipa mishahara kwa wakati - Kuandaa na kuwasilisha nyaraka za malipo Hazina - Kuandaa na kuwasilisha taarifa za Mapato na Matumizi Hazina - Kuandaa na kuhifadhi kumbukumbu za nyaraka za Malipo - Kutekeleza malipo kwa Mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu za matumizi ya fedha za Serikali - Kuandaa na kuratibu majibu ya hoja mbalimbali za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. ## Internal Auditing Majukumu ya Kitengo Kitengo cha Huduma ya Ukaguzi wa Ndani kitatathmini uthabiti na matumizi ya udhibiti wa uhasibu, fedha na uendeshaji na kwa zaidi Kitengo kitafanya yafuatayo: - Kupitia na kutoa taarifa juu ya udhibiti sahihi wa upokeaji, uhifadhi na matumizi ya rasilimali zote za fedha za Wizara; - Kupitia na kutoa taarifa ya ufuasi wa taratibu za fedha na uendeshaji zilizowekwa katika sheria yoyote au kanuni yoyote au maelekezo yaliyotolewa chini ya sheria hiyo na utaratibu mzuri wa uhasibu kama inavyofafanuliwa mara kwa mara na Mhasibu Mkuu wa Serikali ili kuepusha kutekeleza majukumu na kuidhinisha. malipo ya nyongeza ambayo yangehakikisha udhibiti mzuri wa matumizi ya Wizara; - Kupitia na kutoa taarifa kuhusu uainishaji na mgawanyo sahihi wa hesabu za mapato na matumizi; - Kupitia na kutoa taarifa kuhusu uaminifu na uadilifu wa taarifa za fedha na uendeshaji ili taarifa zinazotolewa ziruhusu utayarishaji wa taarifa sahihi za fedha na ripoti nyinginezo kwa taarifa za Wizara na umma kwa ujumla kama inavyotakiwa na sheria; - Kukagua na kutoa ripoti kuhusu mifumo iliyopo inayotumika kulinda mali, na, kama inafaa, uthibitisho wa kuwepo kwa mali hizo; - Kupitia na kutoa ripoti kuhusu utendakazi au programu ili kubaini kama matokeo yanawiana na malengo na malengo yaliyowekwa; - Kupitia na kutoa taarifa kuhusu utoshelevu wa hatua za menejimenti katika kujibu ripoti za ukaguzi wa ndani, na kusaidia menejimenti katika utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na ripoti hizo na pia, inapobidi, mapendekezo yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali; na - Kukagua na kutoa taarifa juu ya utoshelevu wa udhibiti uliojengwa katika mifumo ya kompyuta iliyopo katika Wizara. - Pamoja na majukumu yaliyoainishwa chini ya kanuni ndogo ya (1), kitengo cha Huduma ya Ukaguzi wa Ndani kitajibu, kwa kuzingatia vikwazo vya rasilimali, maombi ya dharura ya msaada wa ukaguzi au ushauri kama itakavyoombwa na Afisa Masuuli au Wakuu wa Idara na Vitengo vya Wizara **Objectives** To provide legal expertise and services to the Ministry This Unit will provide the following activities: - - To provide legal services and assistance to the Ministry’s Division, Units and entities under the Ministry on interpretation of Laws, terms of contracts, terms of Agreements, privatization agreements, procurement contracts, guarantees, letters of undertaking, memorandum of understanding, consultancy agreements and other legal documents. - Provide technical support in preparation of legislative instruments including enactments of Parliament and subsidiary legislation(s) and forward to the Office of the Attorney General; - Oversee negotiations of the Culture, Arts and Sports development agreements; - Provide legal assistance and services to the Ministry and its institutions; - Participate to various negotiations and meetings that call for legal expertise on the Culture, Arts and Sports sectors; - Translate legislations within the Culture, Arts and Sports sectors; - Liaise with the Office of the Attorney General on litigation of civil cases and other claims involving the Ministry; and - Provide technical support to Office of the Attorney General on review of various legal instruments such as orders, notices, certificates, agreements and transfer deeds; # ICT Kutoa Utaalamu na Huduma kuhusiana na matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Wizarani. Kitengo hiki kinafanya kazi zifuatazo:- - Kutekeleza sera ya TEHAMA na Serikali Mtandao; - Kutengeneza na kuratibu Mifumo ya TEHAMA Wizarani; - Kuhakisha Kompyuta na program zinawekwa vizuri; - Kuandaa mahitaji katika ununuzi wa vifaa vya TEHAMA - Kutengeneza na kusimamia mfumo wa mawasiliano ya baruapepe; - Kufanya tafiti na kushauri maeneo ya kutumia TEHAMA kama nguzo ya kutoa huduma bora na kwa wakati kwa wananchi. - Kitengo cha Mawasiliano Serikalini - Kuratibu mikutano ya Wizara na vyombo vya habari juu utoaji wa taarifa kwa umma kuhusu masuala yote ya kihabari ya Wizara; - Kuratibu masuala yote ya Mawasiliano ndani ya Wizara; - Kuandaa vipindi katika vyombo vya habari, kusambaza taarifa na machapisho mbalimbali yanayoelimisha Umma kuhusu Sera, Sheria, programu, maonyesho, na maboresho mbalimbali yanayofanyika na kutekelezwa na Wizara; - Kuandaa na kutekeleza Mkakati wa Mawasiliano wa Wizara; - Kuratibu na kuandaa habari na uzalishaji wa makala zinazohusu Wizara na kuzisambaza kwenye vyombo vya habari yakiwemo magazeti, majarida, radio, Televisheni na mitandao ya kijamii; - Kuhuisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za Idara za kisekta kwenye tovuti ya Wizara; - Kuwasiliana na wananchi pamoja na vyombo vya habari pamoja na kushughulikia hoja mbalimbali za wadau zinazoihusu Wizara kwenye Magazeti na Mitandao ya kijamii; - Kushiriki katika maandalizi ya nyaraka mbalimbali za kihabari za sekta za wizara kwa ajili ya warsha na mikutano; - Kuratibu na kuandaa Makala (print and electronic) na majarida ya Wizara; na - Kuhifadhi taarifambalimbali za Wizara. **Functions of the Monitoring and Evaluation Unit** - Monitor and Evaluate implementation of the Policy, Medium – Term Strategic Plan, Annual Plan, Budget, Programs and Projects in line with National planning framework; - Monitor and Evaluate National Key Result Areas (NKRA) for the Ministry; - Undertake impact assessment on plans, program and project under the Ministry; - Develop and implement M&E Framework and System for the Ministry; - Monitor implementation of Evaluation recommendations; - Prepare periodic M&E reports on NKPAs under the Ministry; - Monitor and Evaluate implementation of the Ruling Party Manifesto and Government Directives; - Monitor and evaluate periodic and ad hoc performance of the Ministry; - Monitor performance of the institutional under the Ministry; - Coordinate institutional performance review/public institutional performance Management information system (PIPMIS), and - Be custodian of the Ministry statistics.
9e2bf025e43108c4822883744ca6629559708dee485bf4557d52e4c02c9081e4
959
5.622523
8
5,392
1
0
0
0.312826
5.94
117
https://www.michezo.go.tz/policies/our-security-policies
#### Sisi ni Nani Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ilianzishwa kwa Tangazo la Serikali Namba 1 la Januari, 2016. Katika kutekeleza majukumu yake kikamilifu, Wizara kimuundo imegawanyika katika maeneo makuu mawili ambayo ni : i. Usimamizi na utekelezaji wa masuala ya kisekta ii. Uendeshaji, uratibu na usimamizi USIMAMIZI NA UTEKELEZAJI WA MASUALA YA KISEKTA Eneo hili linatekelezwa na Idara ya Idara ya Maendeleo ya Utamaduni,Idara ya Maendeleo ya Sanaa na Idara ya Maendeleo ya Michezo kwa ushirikiano na Taasisi zilizopo chini ya Idara hizo. UENDESHAJI URATIBU NA USIMAMIZI Eneo hili linatekelezwa na Idara ya Sera na Mipango, Idara ya Utawala na Rasilimali Watu,Kitengo cha Fedha na Uhasibu, Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Kitengo cha Ununuzi na Ugavi, Kitengo cha Huduma za Sheria na Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano pamoja na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini. Kuendeleza utambulisho wa Taifa kwa kuwezesha upatikanaji mzuri wa Habari,Kukuza Utamaduni na Michezo kwa Maendeleo ya Jamii na Uchumi. MAJUKUMU YA WIZARA Ili kufanikisha majukumu yake Wizara inatekeleza Sera za Utamaduni na Michezo pamoja na Malengo yake. SERA YA MAENDELEO YA UTAMADUNI YA MWAKA 1997 Malengo yake: i. Kushirikisha shughuli za Utamaduni wa Taifa kuanzia Shule za Awali, Sekondari na Elimu ya Juu na kuhakikisha kwamba mafunzo ya Utamaduni yanaingizwa katika Mitaala na muhtasari na kufundishwa shuleni na vyuoni. ii. Kuhimiza na kukuza utaifa kwa vijana wetu na wananchi kwa ujumla. iii. Kuhimiza Utu katika Maendeleo ya Taifa. iv. Kuimarisha Uchangiaji wa gharama, Ukuzaji, Utunzaji na Uimarishaji wa Taasisi za Utamaduni kwa watumiaji wa huduma hizo. v. Kuelimisha jamii juu ya masuala mbalimbali yanayohusu Utamaduni na jinsi sanaa inavyoweza kutumika katika kupambana na UKIMWI. SERA YA MAENDELEO YA MICHEZO YA MWAKA 1995 Malengo yake ni: i. Kuhamasisha wananchi kushiriki michezo na mazoezi ya viungo vya mwili ili kuimarisha afya zao. ii. Kuhakikisha timu na wachezaji wetu wanashiriki kikamilifu katika mashindano na michezo ya kitaifa na kimataifa. iii. Kufanya utafiti wa Michezo ya Jadi kwa lengo la kuifufua na kuiendeleza. iv. Kuimarisha ushirikiano na mataifa mengine katika utoaji wa elimu kwa michezo na wanamichezo. v. Kusimamia ujenzi wa miundombinu ya kisasa katika Sekta ya Michezo. vi. Kuimarisha Utawala bora katika michezo. vii. Kutoa Mafunzo ya wataalamu wa michezo. viii. Kupambana na Janga la UKIMWI katika michezo. ix. Kuendeleza na kutambua vipaji vya vijana katika michezo kuanzia umri mdogo. TAASISI ZILIZOPO CHINI YA WIZARA SEKTA YA MAENDELEO YA SANAA SEKTA YA MAENDELEO YA MICHEZO
f57bef7830025e962643ea0225f05f1353c221d7fe9418bc16f2b41f0e4a19e0
399
5.556391
31
2,217
1
0
0
0.250627
1.5
67
https://www.michezo.go.tz/news/mhe-ndumbaro-aongozana-na-bodaboda-kujindikisha-daftari-la-mpiga-kura-songea
#### News Ikiwa ni siku ya nne ya zoezi la uandikishaji wananchi katika Daftari la Wapiga Kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Oktoba 14, 2024 amejiandikisha katika daftari hilo Mtaa wa Mjimwema Manispaa ya Songea. Akizungumza na baadhi ya wananchi waliojitokeza katika eneo hio Mhe. Ndumbaro amewahamasisha vijana na wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi katika maeneo kujiandikisha, ili wapate fursa ya kugombea na kuchagua viongozi wanaowataka katika mitaa yao. Aidha Mhe. Ndumbaro amekagua uandikishaji katika mitaa mingine miwili mtaa wa Merikebo Kata ya Bombambili na Mtaa wa Matarawe kati Kata ya Matarawe ambapo zoezi hilo linaendelea vizuri, na litahitimishwa Oktoba 20,2024 kote nchini.
307c7a28c399d358cd9800a16b3be29266616d94603ef1a2c8818d46956d8cea
125
5.544
7
693
1
0
0
0.8
3.2
18
https://www.michezo.go.tz/news/bi-rosemary-maganda-ashinda-katibu-mkuu-tughe-tawi-la-utamaduni
#### News Chama Cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kimemchagua Bi. Rosemary Maganda kuwa Katibu wa Chama hicho, kwa jumla ya kura 26 kati ya kura 27 walizopiga. Uchaguzi huo umefanyika Oktoba 11, 2024 katika Ofisi za wizara Mtumba chini ya Msimamizi Bw Kelvin Aloysius Mapembe kutoka TUGHE Mkoa wa Dodoma, na kuhudhuriwa na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Bi. Zahara Guga kwa lengo la kujaza nafasi iliyoachwa wazi na mtangulizi wake ambaye amehama wizara. Wajumbe hao pia wamemchagua Bi. Anna Lyamkuu kuwa Katibu wa akina Mama kwa jumla ya kura zote 11 zilizopigwa, ambaye pia anajaza nafasi ya mtangulizi wake aliyehama wizara. Mara baada ya uchaguzi huo, Bi.. Rosemary alikabidhiwa vitendea kazi tayari kuanza kuongoza chama hicho, akiahidi kufanya kazi kwa weledi haki na kutatua changamoto zilizopo kwenye chama hicho.
510acd9e37dd75bcacfcf1c8bf6ea1ee4b970a2fb788e6d17c631e06da31d166
144
5.298611
7
763
1
0
0
0.694444
4.17
15
https://www.michezo.go.tz/news/naibu-waziri-mwinjuma-aonesha-muonekano-wa-tuzo-za-muziki-tanzania
#### News Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, Oktoba 10,2024 Jijini Dar es Salaam ameonesha rasmi muonekano wa Tuzo za Muziki Tanzania (TMA) mbele ya Waandishi wa Habari. Akizungumza na wanahabari hao, Mhe. Mwinjuma amesisitiza dhamira ya dhati ya Serikali katika kuimarisha viwango vya tuzo hizo, ambapo mwaka huu zitatolewa Jumamosi, tarehe 19 Oktoba 2024, katika ukumbi wa The Dome Masaki. "Sisi wasaidizi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tunaona mapenzi ya dhati ya mama yetu kuhusiana na michezo, sanaa na utamaduni wa nchi hii, hivyo hatuwezi kufanya vitu chini ya kiwango, ndio maana tuzo hizi zilikuwa zinaendelea kuhakikiwa" amesema Mhe. Mwinjuma. Kwa upande wake, Katibu wa Baraza la Sanaa la Taifa, Dkt. Kedmon Mapana, amefafanua namna ambavyo mwitikio wa wasanii katika tuzo hizo imekua mkubwa. "Mwaka huu tumepokea kazi zaidi ya 1440, ikilinganishwa na mwaka jana, katika vipengele 36 vinavyoshindaniwa," aliongeza Dkt. Mapana.
8b17d5555abf9020202b9359531ef8a0d3f49cb3c310eb9a72bf690fa240dabc
149
5.550336
12
827
1
0
0
0.671141
4.03
18
https://www.ccm.or.tz/ccm-kuhusu
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilianza rasmi Februari 5, 1977 kutokana na kuunganishwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) kilichokuwa chama tawala Tanzania Bara, kikiongozwa na Rais wa Kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Chama cha Afro-Shirazi Party (ASP) kilichokuwa chama tawala Zanzibar kikiongozwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar Sheikh Amaan Abeid Karume. CCM imekuwa ikishinda chaguzi za Urais toka mfumo wa vyama vingi uliporejeshwa nchini Tanzania huku pia kikipata idadi kubwa ya wabunge wa Bunge la Muungano na Baraza la Wawakilishi. Baada ya kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi CCM imeendelea kuiongoza Tanzania kutokana na kushinda chaguzi zilizofanyika tangu1995. Viongozi walioweza kushinda kwa tiketi ya CCM kwenye chaguzi hizo ni Benjamin Mkapa,Jakaya Mrisho Kikwete na Dk. John Joseph Pombe Magufuli. Viongozi walioshika Uenyekiti wa CCM miaka waliyoongoza ikiwa kwenye mabano, ni; CCM inazo Jumuiya tatu ambazo zinafanyakazi kwa kuyaunganisha makundi ya Vijana (Umoja wa Vijana wa CCM), Wanawake (Umoja wa Wanawake Tanzania- UWT) na Jumuiya ya Wazazi Tanzania. Jumuiya hizi kila moja ina viongozi ambao moangilio wake unafanana na ule wa CCM yenyewe kuanzia ngazi ya Mwenyekiti Taifa hadi ngazi za matawi. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
5eb0b03c7ad0de2b474a97128095bc517cb9a47b6dd21f58fe135307963f2312
271
5.738007
10
1,555
1
0
0
0
0.74
29
https://www.ccm.or.tz/ccm-idara
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Idara ya Organaizesheni ni moja kati ya Idara nne za CCM. Idara hii imeanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 Toleo la 2017 Ibara ya 107 (1). Idara hii ndiyo injini ya Uendeshaji wa Chama kwani ndio Idara inayohusika na ** Masuala yote ya Wanachama;** kwani Chama kisicho na Wanachama ni sawa na gunia tupu ambalo haliwezi kusimama. Idara hii ndio inayoshughulika na Idara ya Organaizesheni ndio inayosimamia ** Jumuiya za Chama na Sehemu ya Wazee.** CCM ilianzisha Jumuiya za CCM ili ziwe ni mkondo wa kufikisha Sera zake na Siasa ya CCM kwenye Makundi yote ya Kijamii kwa upande mmoja, na kuwa mkondo wa kuitafutia CCM Marafiki na Wanachama kutoka kwnye makundi hayo kwa upande wa pili. CCM pia inathamini sana mchango wa Wazee katika maendeleo ya Taifa letu, ndio maana ikaanzisha sehemu ya Wazee ili kuwawezesha Wazee kurithisha kwa Taifa busara, hekima na ujasiri wao ndani ya Jamii. Wahenga walisema, Idara ya Organaizesheni ndio inayosimamia** masuala yote ya uchaguzi wa ndani ya CCM na ule wa kushika Dola.** Viongozi wa Cham a cha Kijamaa huchaguliwa kwa kura za wanachama na huongoza Chama kwa ridhaa yao. Lakini pia Chama chochote cha Siasa duniani lengo lake kuu huwa ni kushinda uchaguzi ili kushika dola na kuunda Serikali. Kwa kuwa toka Uhuru wa Tanganyika na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar nchi hii imekuwa chini ya Uongozi madhubuti wa CCM, ndiyo kusema Idara hii imetimiza vema majukumu yake. Idara ya Organaizesheni ndiyo inayosimamia ** Katiba Muundo Kanuni, na Taratibu za Chama na Jumuiya za CCM.** Hii ndiyo kusema Idara hii ndiyo inayohakikisha wakati wote kuwa Katiba ya CCM, Kanuni zote za Chama na Jumuiya zake, Muundo wa Chama na Taratibu mbalimbali zikiwemo taratibu za Sehemu ya Wazee zinakiwezesha Chama kutekeleza madhumuni ya kuundwa kwake. Idara hii ndio hufanya marekebisho ya miongozo hii kwa mujibu wa mahitaji ya Chama kwa wakati husika. Bila shaka utaona kuwa utulivu uliopo CCM ukilinganisha vyama vingine vya Siasa hapa nchini unatokana na utekelezaji mzuri wa wajibu huu. Hii ndio sababu tukasema Idara hii ndiyo ** injini** ya Chama. Idara ya Uchumi na Fedha ni miongoni mwa Idara tano za **Chama cha Mapinduzi** zinazoongozwa na Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa ambazo zimeundwa kwa mujibu wa Ibara ya 105 ya Katiba ya CCM ya Mwaka 1977, Toleo la 2017. Idara hii inaongozwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa wa Uchumi na Fedha ambaye ni **Dkt. Frank George Haule Hawassi**. Majukumu ya msingi ya Idara yameainishwa na kutajwa bayana kwenye Ibara ya 107(4) (a)-(e) ya Katiba ya CCM, kama ifuatavyo: Ili kurahisisha na kuleta ufanisi wa utendaji kazi za Chama, muundo wa Idara ya Uchumi na Fedha umegawanywa katika vitengo vitatu muhimu ambapo kila kitengo kimegawanywa pia katika sehemu (Sections) na kupangiwa majukumu mahsusi ya kila siku ya kusimamia, kufuatilia na kutekeleza. Vitengo vya Idara ni hivi vifuatavyo: Pamoja na majukumu ya Kiidara, Idara pia inayo majukumu mengine ya msingi ya kusimamia na kuratibu shughuli zote za Baraza la Wadhamini wa CCM kwa niaba ya Katibu Mkuu wa CCM zikiwemo shughuli za vikao, usimamizi na ufuatiliaji wa utekelezaji wa maazimio ya vikao vya Baraza la Wadhamini wa Chama Cha Mapinduzi. Kwa kuzingatia utajiri mkubwa Chama kilionao hususan katika eneo la Rasilimali Ardhi na Rasilimali Wanachama, Idara ya Uchumi na Fedha ina wajibu wa msingi wa kuhakikisha rasilimali hizi zinatumika kikamilifu katika kukiimarisha Chama kiuchumi na kimapato hatua ambayo itakiwezesha Chama kuhudumia kwa ufanisi majukumu yake ya kisiasa na uendeshaji wa Ofisi. Idara ya mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ni moja kati ya Idara za CCM Makao Makuu inayoundwa na Ibara ya 107 kifungu cha 3 ya Katiba ya CCM ya mwaka 1977 Toleo la 2017. Idara hii inafahamika zaidi kama idara inayoshughulika na kujenga uhusiano wa kimataifa, hata hivyo ukweli ni kwamba idara hii inashughulikia mambo mengi na muhimu ndani ya nchi yanayojenga taswira njema ya CCM kwa wananchi. Kwa kifupi tunasema, idara hii inajihusisha na kazi za Chama nje ya Chama ndani ya Umma. Kwa mujibu wa Katiba ya Chama Cha Mapinduzi, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa inajukumu la msingi la kufuatilia hali ya Kisiasa Nchini. Kwa lugha nyepesi ina kazi ya kufuatia hali ya maisha ya wananchi wa Tanzania, kijamii na kiuchumi kwa ujumla. Idara hii pia ndiyo yenye jukumu la kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM Nchini, kuona kwamba tumefanikiwa kwa kiasi gani kutekeleza Ilani yetu, ni kwa kiasi gani tumeondoa kero na changamoto zinazowakabili wananchi wetu na kukishauri Chama namna ya kukabiliana nazo. Ukiacha mbali jukumu la kufuatilia maendeleo ya Jumuiya za Kijamii nchini, na kushughulikia na kusimamia masuala ya Itifaki ndani ya Chama, Jukumu lingine kubwa na muhimu la Idara hii ni kuratibu uhusiano na ushirikiano wa CCM na Vyama vya Siasa vya Kidugu , Kirafiki na vya Kimapinduzi. Aidha, Idara ina jukumu la kufuatilia hali ya kisiasa katika nchi jirani na nchi nyinginezo duniani na kufuatilia maendeleo ya kijamii ya Kamati za Urafiki na Mshikamano kati ya Watanzania na wananchi wa nchi Rafiki. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
41aadbd2670dd3d58ddaae439e2c770ad7d77deeb0bcdae39171f29bdcf69617
920
5.179348
32
4,765
1
0
0
0
1.85
146
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/K5J
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. BALOZI NCHIMBI AJIANDIKISHA KUPIGA KURA SERIKALI ZA MITAA, ATOA WITO WATU KUJITOKEZA KWA WING Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amejiandikisha kwenye daftari la wakazi katika mtaa wake, eneo la Kilimani, jijini Dodoma leo tarehe 18, Oktoba 2024. Akizungumza baada ya kujiandikisha, Balozi Nchimbi aliwasisitiza wananchi umuhimu wa kujitokeza kwa wingi kuandikishwa, akisema kuwa ni hatua muhimu katika kuhakikisha ushiriki wao kwenye mchakato wa kidemokrasia. Uandikishaji wa wapiga kura wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kwenye daftari la wakaazi, ulianza tarehe 11 Oktoba, 2024 na utamalizika tarehe 20 Oktoba 2024. Balozi Nchimbi amewahimiza wananchi kutumia siku zilizobaki kutimiza haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi bora wa Serikali za Mitaa mwezi ujao, akisisitiza kuwa kila kura inahesabika na inaweza kuleta mabadiliko makubwa kwenye jamii, ikizingatiwa kuwa viongozi watakaochaguliwa watakuwa na jukumu la kusimamia maendeleo ya mitaa yao. Balozi Nchimbi amesisitiza umuhimu makundi yote katika jamii kushiriki kikamilifu, hususan vijana na wanawake, kutambua nafasi yao ya kipekee katika mchakato huu, ikiwa pia ni sehemu muhimu kwao kujihusisha na siasa kwa lengo la kuleta maendeleo katika kijamii. Pamoja na kuwasisitiza wananchi wajiandikishe na kujitokeza kupiga kura siku ya uchaguzi, Balozi Nchimbi alisema uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni fursa kwa wananchi kuchagua viongozi wenye maono na uwezo wa kuongoza na kusimamia shughuli za maendeleo kama vile elimu, afya, maji safi, na miundombinu. Aidha, Katibu Mkuu ameendelea kuwataka wananchi na wadau wote wa uchaguzi, kudumisha amani na mshikamano, kuepuka kuchochea chuki katika jamii, na kuzingatia taratibu za kisheria, ili kuhakikisha maslahi ya taifa na tija kwa wananchi, vinakuwa mbele, kabla, wakati, na baada ya uchaguzi. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
3284f8c49eb7b1465f576119a425c92d64591fbc126414d32d7c9af407170407
353
5.86119
11
2,069
1
0
0
0
1.7
44
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/J7v
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. NAIBU KATIBU MKUU CCM-BARA AFANYA MAZUNGUMZO NA KANSELA KUTOKA UBALOZI WA NORWAY TANZANIA Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Ndg.John Mongella amekutana na kufanya mazungumzo na Kansela kutoka Ubalozi wa Norway Ndg.Ingrid Norstein kwenye Ofisi za Makao Makuu ya CCM Jijini Dodoma leo tarehe 09 Oktoba,2024 Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
444ff4587a03fa6bda8d2e40058c322c97aa22b63cce6c60c05752661b85d02f
131
5.664122
3
742
1
0
0
0
0.76
12
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/GQ3
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. KISHINDO CHA SHINYANGA MAPOKEZI YA NCHIMBI Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amewasili na kupokelewa rasmi Mkoa wa Shinyanga, leo tarehe 9 Oktoba 2024, tayari kuanza ziara ya siku tatu katika maeneo mbalimbali ya wilaya za mkoa huo. Balozi Nchimbi ambaye ameambatana na Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Amos Gabriel Makalla na Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (Suki), Ndugu Rabia Hamid Abdalla, ameingia Shinyanga akitokea Mkoa wa Simiyu, ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020 - 2025, kusikiliza kero na changamoto za wananchi kisha kuzitafutia majawabu na kuhamasisha uimara wa CCM kuanzia ngazi ya mashina. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
7db10f104e90f5901aa398692a4f0312b335c21706ebead9c5153f972b65d6a4
201
5.457711
6
1,097
1
0
0
0
2.99
20
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/E64
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## KATIBU MKUU CCM AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MASWA MASWA Wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Mji wa Maswa wakifuatilia na kushiriki kwa makini mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, katika Viwanja vya Madeco mjini hapo, leo tarehe 8 Oktoba 2024. Balozi Nchimbi, ambaye ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Amos Gabriel Makalla, pamoja na Katibu wa NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndugu Rabia Abdallah Hamid, yuko katika ziara ya siku tatu katika Mkoa wa Simiyu, aliyoianza tarehe 6 Oktoba, mwaka huu. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
bf630b09a956e33f382f022f620d3c5fa082227fcc6ebcc20a7aff49ceaf7561
186
5.38172
6
1,001
1
0
0
0.537634
2.69
21
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/DJ5
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## SIMIYU NA CCM, NCHIMBI AKIWASILI ITILIMA Mapokezi makubwa wananchi na wanaCCM wa Itilima wakimpatia mapokezi makubwa Katibu Mkuu Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi alipowasili eneo la Lugulu kwa ajili ya kuwasalimia, akiwa njiani kuelekea wilayani Maswa, leo tarehe 8 Oktoba 2024, ikiwa ni siku ya tatu ya ziara yake ya kikazi Mkoa wa Simiyu, ambayo ameambatana na Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Amos Makalla na Katibu wa NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndugu Rabia Abdalla Hamid. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
0c307b61af45d1e05da6504036756cf42f979a5c6fef62cd16927926c0b192f6
172
5.436047
5
935
1
0
0
0.581395
2.91
18
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/BRW
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## DKT NCHIMBI AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MWANDOYA-KISESA Wananchi wa Kata ya Mwandoya, Jimbo la Kisesa, Wilaya ya Meatu, mkoani Simiyu, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, alipokuwa akizungumzia masuala na hoja mbalimbali kutoka kwa wawakilishi wao, Ndugu Basu Kayungilo, Diwani wa Kata ya Mwandoya na Ndugu Luhaga Mpina, Mbunge wa Kisesa, leo tarehe 7 Oktoba 2024. Balozi Nchimbi alisimama Mwandoya kuwasalimia wakazi wa eneo hilo na kuzungumza nao masuala ya maendeleo yanayohusu jimbo hilo la Kisesa, akiwa njiani kuelekea Mwanhuzi, Meatu, ambapo ni mwendelezo wa ziara yake ya siku 3, mkoani humo. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
fa38b35f58baf9f948cdf237eaec9606b7524a540567e25145245b6c84e0fd97
185
5.648649
6
1,045
1
0
0
0.540541
2.16
16
https://www.orpp.go.tz/
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imepongezwa kwa namna ambavyo imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha Vyama vya Siasa vinajiendesha kama taasisi na kwa kuzingatia sheria na taraatibu za kidemokrasia. Soma zaidi.. Karibu kwenye tovuti ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa . Kupitia tovuti hii, utapata taarifa za uhakika juu ya shughuli za Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini na taarifa za uhakika juu ya Vyama vya Siasa. Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imejikita katika usimamizi wa Sheria ya Vyama vya Siasa Na 5 ya mwaka 1992 na Sheria ya Gharama za uchaguzi ya mwaka 2010 ili kuhakikisha uwepo na ukuaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini. Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imepongezwa kwa namna ambavyo imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha Vyama vya Siasa vinajiendesha kama taasisi na kwa kuzingatia sheria na taraatibu za kidemokrasia. Soma zaidi.. Baraza la Vyama vya Siasa limeafiki kutoa pongezi za dhati kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo ameendelea kuimarisha Demokrasia nchini kwa kuboresha Baraza la Vyama vya Siasa nchini. Soma zaidi.. Watumishi Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa watakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya vifaa vya TEHAMA na kuwa makini wanapokuwa katika mitandao ya kijamii ili kuhakikisha wanalinda unyeti wa ofisi hiyo. Soma zaidi.. Rais Samia amekipongeza Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini kwa kazi nzuri walioifanya ya kuchambua maoni ya wadau kwa kipindi cha miezi 10. Soma zaidi..
5fb13ab6ced51fa65f7b8950f37b8b5f0d83af89948c906692cd8f8f442d126b
254
5.125984
11
1,302
1
0
0
0
1.97
29
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/A9p
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## DKT NCHIMBI AHANI MSIBA WA ALIYEKUWA MWENYEKITI WA CCM BARIADI Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akiambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Amos Gabriel Makalla na Katibu wa NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndugu Rabia Hamid Abdalla, amefika kuwapatia pole familia ya Bi. Juliana Wilemahongo, aliyefariki dunia tarehe 15 Septemba 2024. Bi Wilemahongo hadi anafikwa na mauti, alikuwa ndiye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bariadi, akiwa amejitolea kutumikia nafasi hiyo ya uongozi kwa vipindi vitatu. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
db159cf489c2eae4fa002ee9bac4828f8dfdf2507eebe101821a058bf297efc9
178
5.578652
7
993
1
0
0
0.561798
2.25
18
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/zxO
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## SHIKAMOO SIMIYU, YAJA NA MITANO TENA Maelfu ya wananchi wa mji wa Bariadi na vitongoji vyake waliofurika kwenye mkutano mkubwa wa hadhara mjini hapo wamemtuma Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, kufikisha salamu zao kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa wanamhitaji agombee na aendelee kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka mingine mitano katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Umati huo mkubwa wa wananchi ulionesha matamanio hayo kwa kutamka maneno “mitano tena” huku wakinyoosha mikono juu baada ya kuulizwa iwapo kauli zilizotolewa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali kuhusu mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020-2025 katika sekta mbalimbali za maendeleo kwenye maeneo yao ni za kweli, na wangependa kutuma salamu gani kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuthibitisha kuwa uongozi wake umewagusa. Akizungumza na maelfu ya wananchi na wanachama wa CCM katika mkutano huo uliofanyika katika Uwanja wa CCM Bariadi, mkoani Simiyu, Balozi Nchimbi aliwaahidi kufikisha salamu hizo kwa uzito ule ule walivyomtuma, kwanza kwa wingi wao walivyojitokeza mkutanoni na pili kwa kunyoosha mikono mingi hewani, vyote vikidhihirisha mapenzi yao kwa CCM na Rais Dkt. Samia, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM. “Leo kila mtu ameona jinsi ambavyo Simiyu mlivyotikisa. Ni mapokezi ya heshima na ni salamu tosha kuwa CCM inakubalika na Dkt. Samia anakubalika sana, na ujumbe wa salamu zenu nimeupokea nitaufikisha. Tumefurahishwa na taarifa za utekelezaji na usimamizi wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Imetekelezwa na kusimamiwa vizuri sana. Nawapongeza Kamati ya Siasa ya Mkoa, ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Ndugu Shemsa, pamoja na watendaji wote wa Serikali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa. Wanafanya kazi nzuri sana,” alisema Balozi Dkt. Nchimbi huku akiitikiwa kwa shangwe na vigelegele. Aidha, Balozi Nchimbi amewaambia wananchi wa Simiyu kuwa Dkt. Samia alivyopokea dhamana ya kuongoza nchi, wapo waliokuwa hawakuamini kuwa miradi iliyoachwa na mtangulizi wake, Hayati John Magufuli, hasa ile mikubwa ya kimkakati, ingekamilika. Lakini kwa sasa kila Mtanzania ni shahidi kuwa miradi yote inaendelea vizuri katika hatua mbalimbali na mingine imekamilika na inatumika. Balozi Nchimbi pia amewaambia wananchi kuwa adhabu sahihi ya wanasiasa waliofilisika kisera na hoja, wanaohamasisha vurugu katika jamii kwa siasa za udini, ukabila, ukanda na kuchoma moto vitu, ni kuwanyima kura na kuipigia kura nyingi CCM. Balozi Nchimbi pia amesisitiza wananchi kuwa mstari wa mbele kwenye kulinda amani ya nchi yetu, na inapotokea mtu yeyote anayetaka kuvuruga amani, akemewe kwa ‘macho makavu’ usoni na akataliwe bila kumuonea haya. Balozi Nchimbi yupo mkoani Simiyu ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake mkoani humo, akitarajiwa kufanya ziara kwa siku tatu kabla ya kuelekea Mkoa wa Shinyanga, akiwa ameongozana na Katibu wa NEC-Itikadi Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Ndugu Amos Makalla, pamoja na Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndugu Rabia Abdalla Hamid. 🗓️06 Oktoba 2024 📍Bariadi, Simiyu Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
94fa48a2e8a78d05dd9590f71a829f9adfcc2b78a92ad9b0b75800d89c4f8088
552
5.576087
26
3,078
1
0
0
0.181159
0.91
77
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/yJg
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## UDINI NI HATARI, KUCHOMA NGUO NI UTOTO Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amewahimiza Watanzania kuendelea kushirikiana na CCM, akisisitiza kuwa chama hicho kimeonyesha kwa vitendo uwezo wa kuongoza nchi na dhamira ya kuwahudumia wananchi wanyonge. Dkt. Nchimbi alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Lamadi, Wilaya ya Busega na Kata ya Dutwa, wilayani Bariadi, mkoani Simiyu, kwa nyakati tofauti leo, tarehe 6 Oktoba 2024. Hii ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika mkoa huo, ambapo alieleza kuwa CCM imekuwa ikiandaa viongozi wake kwa ufanisi. “Kiongozi aliyeandaliwa vizuri hueleza mipango yake waziwazi anapopewa nafasi: ‘Nikitwaa madaraka, nitafanya moja, mbili, tatu.’ Lakini kiongozi ambaye hajakomaa, anapewa nafasi ya kuzungumza na kuanza kuhamasisha maandamano, kuchoma nguo, au kuzomea watu, hapo unajua bado hajakomaa na anahitaji muda wa kujifunza zaidi.” “Katika CCM, hatuna viongozi wanaoshikilia madaraka kwa miaka 40. Viongozi wanachaguliwa, wanapungua, na wengine wanapewa nafasi. Ukiangalia baraza la kwanza la mawaziri la Tanganyika, leo hii hakuna hata mmoja aliyebakia kwenye baraza. Kila uongozi unaleta sura mpya. Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu wa miaka mitano iliyopita, leo hayupo. Hii ndiyo CCM.” Balozi Nchimbi alisisitiza kuwa hii ndiyo sababu CCM kinaendelea kuwa chama chenye nguvu, kijana kuliko vyama vingine nchini, kwani uhai wa chama unategemea wanachama na viongozi wake. “Huwezi kusikia mwanachama mkongwe wa CCM akishabikia udini au ukabila. Lakini kuna viongozi wa vyama vingine ambao wameonyesha kushabikia hayo kwa sababu hawana historia ya kuijenga nchi hii, wala hawajui maumivu ya watu wake. Wao hawaitazami nchi kwa mbali, ndiyo maana wanaweza kutoa matamshi bila kujali madhara yanayoweza kutokea,” aliongeza Balozi Nchimbi. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
3a24a66f4b31232ad67864e5e70bc0e443bf3aea84d8ba2775a9d4058c8b58ab
357
5.798319
17
2,070
1
0
0
0.280112
1.12
40
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/wRz
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## HODI SIMIYU, NCHIMBI AKIANZA ZIARA YA SIKU 3 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akizungumza na wananchi wa Lamadi, Wilaya ya Busega, Mkoa wa Simiyu, leo tarehe 6 Oktoba 2024, ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake ya siku tatu mkoani humo. Balozi Nchimbi ambaye ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Amos Makalla na Katibu wa NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (Suki), Ndugu Rabia Hamid Abdalla, ameanza ziara mkoani Simiyu kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020 - 2025, kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi, kukagua uhai wa Chama kuanzia ngazi ya mashina na pia kuhamasisha wananchi kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, utakaofanyika mwezi Novemba, mwaka huu. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
f42301ea4b53653c5077cec4a4e4930536f50da2132ad8f9eca41dc4d4a5b7fa
219
5.319635
6
1,165
1
0
0
0.456621
3.65
20
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/v9M
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM KATIKA MIKOA YA SIMIYU NA SHINYANGA Katibu mkuu wa CCM Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi pamoja na serkrtariet ya CCM Taifa wanatarajia kuanza ziara katika mikoa ya simiyu na Shinyanga kuanzia tarehe 6-11 Oktoba 2024 Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
05418b1d1b2935edb3dde5d9da6335d3622adf65c4b5da4dea4c42d106017314
125
5.496
4
687
1
0
0
0
1.6
13
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/rMW
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. WATUMISHI CCM WANOLEWA KUHUSU FURSA ZA MASOMO NJE YA NCHI Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), kimefanya mafunzo kwa watumishi wa chama na jumuiya zake kuhusu umuhimu wa kujiendeleza kielimu kupitia fursa zinazopatikana kimataifa. Mafunzo hayo yamefanyika Oktoba 3, 2024 katika ukumbi wa ofisi za Makao Makuu ya CCM, Dodoma na kuhudhuriwa na watumishi wa CCM, Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Jumuiya ya Wazazi (WAZAZI) na Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM). Akifungua mafunzo hayo ya siku moja, Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. John Mongella amewataka watumishi wa CCM kuchangamkia fursa za kujiendeleza kielimu ili kuwa weledi katika nafasi wanazozitumikia ndani ya chama na jumuiya zake. Amesema chama kupitia idara ya SUKI, kitajitahidi kutafuta fursa hizo, lakini mtumishi mmoja mmoja hana budi kuzitafuta kwa njia mbalimbali ikiwemo kutumia mitandao ya kijamii. Naibu Katibu Mkuu, Ndg. Mongella alifuatana na Katibu wa NEC, ambaye ni Mkuu wa Idara ya SUKI, Ndg. Rabia Abdalla Hamid na Katibu wa NEC, Organaizesheni, Ndg. Issa Gavu. Kwa upande wake, Ndg. Rabia amesema kujiendeleza kielimu ni muhimu kwa kuwa kunamfanya mtumishi kujipatia maarifa mapya kulingana na mabadiliko mbalimbali yakiwemo ya sayansi na tekinolojia. Ndg. Rabia alizishukuru nchi ambazo zimekuwa zikitoa fursa za mafunzo kwa watumishi na makada wa CCM, ikiwemo Uingereza ambayo kupitia Taasisi ya Chevening imekuwa ikitoa ufadhili wa masomo kwa Watanzania. Ndg. Rabia amewapongeza watumishi wa CCM, UWT, WAZAZI na UVCCM kwa kuhudhuria mafunzo hayo, ambayo yamewaongezea mwanga kuhusiana na ufadhili wa masomo unaotolewa na Taasisi ya Chevening kwa kushirikiana na serikali ya Uingereza. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
fd2026984e27cbe54ce917e1c6bda020dcf3b070f9fded684d3e115088489848
346
5.638728
18
1,951
1
0
0
0
0.58
38
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/qMk
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## CCM YAIOMBA SHIRIKA LA KTI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI YA TANZANIA KUWAWEZESHA VIJANA NA WANAWAKE Katibu wa NEC Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (MCC) Ndg. Rabia Abdallah Hamid, Septemba 19, 2024 Chini Uingereza amefanya mazungumzo na Bw. Will Straw, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Kings Trust International (KTI) na kuiomba Taasisi hiyo kuendelea kushirikiana na serikali katika kuwawezesha vijana na wanawake. Aidha, Ndugu Rabia amewasilisha ombi kwa Taasisi hiyo kuona uwezekano wa kuanzisha mashirikiano na Tanzania hususani kwa ajili ya programu za kuwezesha wanawake. Alieleza kwamba, uwezeshwaji vijana ni moja wapo ya ajenda ya kipaumbele ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Ameongezea kwamba, katika kuendeleza uchumi wa vijana na wanawake Mhe. Dr. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amefanya jitihada kubwa kuwezesha vijana na wanawake kupitia programu mbalimbali kama vile utoaji wa ardhi kwa vijana na kuwapatia ruzuku kujishughulisha na kilimo; kuwapatia vifaa salama vya uvuvi ili kukuza uvuvi endelevu; kuwapatia vifaa vya kupikia kama vile majiko ya gesi ili kujilinda na athari za mabadiliko ya tabianchi. Taasisi hiyo inajishughulisha na kuwezesha vijana kupata ujuzi mbalimbali ili waweze kuingia kwenye soko la ajira. KTI, ilianzishwa mwaka 1976 na Mwana wa Mfalme, Charles ikiitwa kama Prince’s Trust na imekuwa ikifanya kazi hizo za kuhamasisha mafunzo mbalimbali kwa vijana ili kukuza vipaji vyao na kuwawezesha kupata ujuzi mbalimbali katika masuala ya biashara, ujasiriamali, ubunifu na teknolojia. Mwaka 2015, Taasisi hiyo ilipanua wigo wa huduma zake na kuanza kufanyakazi katika nchi 25 za Jumuiya ya Madola (JYM). Hivyo, ilibadilishwa jina na kuitwa Prince Trust International (PTI). Kupitia program zake, Taasisi hiyo imeendelea kuwawezesha vijana kujitegemea na kuchangia maendeleo ya jamii wanazoishi. Mwezi Julai 2024, Taasisi hiyo ilibadilishwa jina na kuitwa Kings Trust International (KTI) kufuatiwa kutawazwa kwa Mfalme Charles III wa Uingereza. Kupitia Mkutano huo, Bw. Straw amemueleza Ndg. Rabia kazi zinazofanywa na Taasisi yao ya kuwasaidia vijana kupata ujuzi na ufundi wa ziada ya mafunzo ya darasani. Ameongezea kwamba vijana hao kupitia mchezo wa Enterprise Challenge wanafundishwa kubuni mawazo ya kibiashara ambayo baadae hushindanishwa na washindi kupewa mitaji midogo ya kuweza kutekeleza miradi au biashara walizobuni. Aidha ameongezea kwamba, nchini Tanzania, Taasisi hiyo inafanyakazi na Asante Africa Foundation kupitia After School Clubs katika shule 20 nchini, ambapo wanafunzi wanapewa vifaa kama computers, laptops na kupatiwa mafunzo ya ubunifu wa mawazo ya biashara. Lengo la kuwapatia ujuzi wa ziada ni kuwawezesha kuingia katika soko la ajira. Pamoja na hayo Taasisi hiyo inafanya kazi na Mo Dewji Foundation kusaidia vijana kupata ujuzi kupitia mitaala inayoendanana soko la ajira ya sasa na utaalam wanaopata unasaidia kupata ufadhili wa masomo kupitia scholarships. Vilevile, ameelezwa kwamba KTI ipo katika mazungumzo na Benk iza CRDB na NMB kwa lengo la kushirikiana katika kuwezesha vijana wa Kitanzania kupata ujuzi wa ujasiriamali, ufundi, ubunifu, teknolojia na kuweza kujitegemea na kuchangia katika uchumi wa nchi. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
cb1b3f08ad076d89ee17b689fa47a121becd927c7c065c4429639605c329a903
556
5.845324
24
3,250
1
0
0
0.179856
1.44
82
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/pXm
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## CCM YASISITIZA UHUSIANO WA KIMATAIFA KUIMARISHA UCHUMI NA MAENDELEO YA WATU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amesema kuwa Serikali na Nchi ya Tanzania, chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan itaendelea kuweka msisitizo katika kuimarisha uhusiano wa kimataifa wenye manufaa ya kiuchumi na maendeleo ya watu. Balozi Nchimbi amesema kuwa urafiki na uhusiano wa kidiplomasia unapaswa kuendelea kuwa mojawapo ya njia sahihi katika kuboresha ushirikiano wa pande mbili kimataifa, kati ya nchi na nchi, au nchi na majukwaa mbalimbali ya kimataifa. Katibu Mkuu huyo wa CCM amesema hayo alipokutana na mabalozi wanaowakilishi nchi zao hapa nchini, kutoka nchi za Brazil na India, pamoja na Mkuu wa Idara ya Mambo ya Nje ya Chama Tawala cha Msumbiji (FRELIMO) na Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Friedrich Ebert Stiftung (FES), nchini Tanzania. Katika mazungumzo na viongozi hao, yaliyofanyika kwa nyakati tofauti tofauti, leo 19 Septemba 2024, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, Balozi Nchimbi amesema mojawapo ya utekelezaji wa Ilani ya CCM unaofanywa na Serikali ya CCM, inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ni pamoja na kuendelea kuboresha uhusiano wa kimataifa, hasa kupitia diplomasia ya uchumi, kwa ajili ya kuimarisha uchumi, maendeleo ya watu na kubadilishana uzoefu kwenye uongozi na demokrasia. Wakati wa mazungumzo na Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Mhe. Gustavo Martins Nogueira na Balozi Nchimbi, viongozi wote wawili walionesha msisitizo na utayari wa kuendelea kuboresha uhusiano kati ya Tanzania na Brazil kwa ajili ya manufaa ya pande zote mbili, hasa katika nyanja za afya, kilimo na michezo. Kwenye mazungumzo ya Balozi Nchimbi na Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Bishwadip Dey, viongozi hao wamezungumzia umuhimu wa kuendelea kuenzi ushirikiano wa kimkakati kati ya nchi hizo mbili katika nyanja mbalimbali, zikiwemo teknolojia, biashara na elimu, ikizingatiwa India ni mojawapo ya nchi zilizopiga hatua kubwa za kimaendeleo katika maeneo hayo. Katika mazungumzo ya Balozi Nchimbi na Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa FRELIMO, Komredi Alcinda Antonio de Abreu, pande zote mbili zimesema urafiki na udugu wa damu uliopo kati ya Tanzania na Msumbiji utaendelea kuenziwa kwa kushirikiana kadri inavyohitajika, kama ilivyo ada tangu wakati wa kupigania ukombozi wa kisiasa wa Nchi za Kusini mwa Afrika, na sasa mkazo umeelekezwa kwenye ukombozi wa kiuchumi na kuendelea kuboresha hali za maisha ya watu. Aidha, katika mkutano wa Balozi Nchimbi na Mkurugenzi Mkaazi wa FES nchini Tanzania, Bwana Christian Denzin, ambaye alimtembelea Katibu Mkuu wa CCM kwa ajili ya kujitambulisha, pande zote mbili zimekubaliana kuendeleza ushirikiano wa muda mrefu kati ya CCM na shirika hilo la nchini Ujerumani, hasa katika kuimarisha uwezo na uzoefu katika nyanja za uongozi na demokrasi, kupitia miradi mbalimbali ya mafunzo ya viongozi. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
8bc2664cdc831f5fd17c839e6c991845ce88ab1bf2de45776421c0e4fc54a373
533
5.575985
14
2,972
1
0
0
0.187617
0.56
63
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/o6k
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## KATIBU MKUU WA CCM AZUNGUMZA NA MKURUGENZI MKAAZI WA SHIRIKA LA FES UJERUMANI Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Friedrich Ebert Stiftung (FES) la nchini Ujerumani, Bwana Christian Denzin, aliyefika ofisini kwa Katibu Mkuu wa CCM kwa ajili ya kujitambulisha na kuzungumza mbalimbali ya kuimarisha uhusiano kati ya CCM na FES, leo tarehe 19 Septemba 2024, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar ES Salaam. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
7644df80c32f2dfa5ebce48b16e84cd1947b8074c8917295d7e1c6a139202995
170
5.494118
5
934
1
0
0
0.588235
1.76
16
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/nNP
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ## KATIBU MKUU WA CCM AFANYA MAZUNGUMZO NA MKUU WA IDARA YA UHUSIANO WA KIMATAIFA FRELIMO Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Chama Tawala cha Msumbiji (FRELIMO), Komredi Alcinda Antonio de Abreu, kuhusu masuala mbalimbali ya kuimarisha uhusiano kati ya Msumbiji na Tanzania, kwa upande mmoja na CCM na FRELIMO kwa upande mwingine, leo tarehe 19 Septemba 2024, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
e752de18793f8f50a5f0793d6e1ff52b56cb5dad2c528311e37a4d1fb7fc9f0a
174
5.413793
5
942
1
0
0
0.574713
1.72
18
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/mMn
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. KATIBU MKUU WA CCM AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA INDIA NCHINI TANZANIA Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Bishwadip Dey, kuhusu masuala mbalimbali ya kuimarisha uhusiano kati ya India na Tanzania, leo tarehe 19 Septemba 2024, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
740e14a46293b67a8abb1ebe2081b6a230a55ef519b46c5b5adfba1fbe3e0e97
150
5.526667
6
829
1
0
0
0
1.33
13
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/lMV
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. KATIBU MKUU WA CCM AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA BRAZIL NCHINI TANZANIA Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Mhe. Gustavo Martins Nogueira, kuhusu masuala mbalimbali ya kuimarisha uhusiano kati ya Brazil na Tanzania, leo tarehe 19 Septemba 2024, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
a6c8184c8e6da857f332b3f5892d51454ffb3d42fe04c8a32126fe57213c4e8a
151
5.576159
6
842
1
0
0
0
1.32
13
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/kOK
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. NUKUU ZA KATIBU MKUU WA CCM AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI Mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Dkt Emmanuel Nchimbi akizungumza na wahariri na waandishi wa habari leo 13 Septemba 2024, Lumumba Dar es Salaam Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
7c57a56dd6205e491542479dace78f799ca8acb7cbccbb01a0c07f41e983cd07
120
5.475
3
657
1
0
0
0
1.67
12
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/wRg
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. HAPI APOKELEWA KIBAHA VIJIJINI AWAONYA VIONGOZI WASIOWAJIBIKA ATAKA WASILAUMU CHAMA KATIBU Mkuu wa Umoja wa Wazazi Tanzania Jumuiya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu. Ally Salum Hapi (MNEC) akiwa Kibaha Vijijini amepigilia msumari suala la viongozi waliopo madarakani kuhakikisha wanafanya kazi na kutoa mrejesho kwa wananchi waliompatia madaraka hayo kuwaongoza hususani katika kipindi hiki ambacho wataingia katika kugombea nafasi zao na kuomba ridhaa kwa wananchi kuwachagua badala ya kuja kulalamika baada ya kushindwa katika chaguzi. Hapi alisema katika wakati huu ambao wanaelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa chama hakitaunga mkono wagombea wasiotokana na wananchi ambao watakuwa na wakati mgumu katika kuwatafutia kura "Hatutaki wagombea wa kuunga unga, tunataka mgombea ambaye wananchi watahitaji awaongoze na ndiyo tutashinda katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu ujao" alisema Hapi Hapi amewataka wanaccm na viongozi kujenga utaratibu wa kukaa katika vikao kutatua changamoto zinazowakabili kwa kufuata utaratibu uliowekwa na chama cha mapinduzi Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Mkoa wa Pwani Mwishehe Mlao amewanyoshea kidole wale wote wanaoendelea kusababisha mivutano ndani ya chama hicho na kufanya wananchi wasikipende chama huku mwenyekiti wa chama wilaya ya Kibaha vijijini akisema hakuna migogoro bali ni jeuri ya baadhi ya wanaccm. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
6bb417d07c4759de5223a8017ef2d99cae315d5f02cae856813f26db94b7138e
284
5.93662
6
1,686
1
0
0
0
0
39
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/v9L
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. COMRADE MONGELLA AWASILI KAHAMA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM John Mongella, Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, amewasili mjini Kahama leo, tarehe 7 Septemba 2024, kwa ziara ya siku moja wilayani humo. Ziara hii inalenga kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama ya 2020-2024. Mongella pia amekutana na Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kahama kwa madhumuni ya kuboresha utendaji wa kazi za chama. Ziara yake mkoani hapa inatarajiwa kudumu kwa siku saba. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
87b226fe7419cf9ffb386fbbee94adaf53e2f04d7002fa554b18fcc1b176b5b8
161
5.47205
7
881
1
0
0
0
1.86
16
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/pXX
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. RATIBA YA ZIARA YA NAIBU KATIBU MKUU WA CCM ZANZIBAR 9-12 SEPTEMBA 2024 Ratiba ya ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM zanzibar Dkt. Mohammed Said Mohammed (dimwa) pamoja na wajumbe wa Kamati Maalum ya Halmashauri kuu ya CCM Taifa, Zanzibar kutembelea na kukagua uhai wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya zote kisiwani - Pemba kuanzia tarehe 09 septemba, 2024 hadi 12 septemba, 2024 Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
5be35e6628ffe2dbb7ff0942a838992d2c8e3545885b8e0b57b5020c5bb18fac
149
5.38255
4
802
1
0
0
0
4.7
13
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/o6A
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. MONGELLA AKUTANA NA WAJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA CCM SHINYANGA MJINI Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, John Mongella, leo Septemba 6, 2024, amekutana na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Shinyanga mjini, wajumbe wa baraza la jumuiya, na mabalozi katika ukumbi wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini. Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CCM pamoja na viongozi wa serikali, akiwemo wakuu wa idara wa Manispaa ya Shinyanga. Mongella ameanza ziara ya siku saba mkoani Shinyanga kwa lengo la kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020-2024 na kuimarisha uhai wa chama. Katika ziara hiyo, atafanya mikutano ya hadhara na ya ndani ili kusikiliza changamoto zinazowakabili wananchi wa mkoa wa Shinyanga. Ziara hiyo itamfikisha katika maeneo ya Shinyanga Vijijini, Kahama, Msalala, Kishapu, na Ushetu, ambako atakutana na viongozi wa chama na wananchi kujadili namna bora ya kuimarisha utekelezaji wa sera za chama kwa maendeleo ya mkoa. Pia, ziara hii inalenga kuwahamasisha wanachama wa CCM kushiriki kikamilifu katika shughuli za chama na kushughulikia kero za wananchi. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
02adc89f852887c9c087c7de8c8d8f6eb3ee83ee82653a6644d63b2d6b312d5e
256
5.550781
9
1,421
1
0
0
0
1.17
28
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/nNY
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. CCM NI CHAMA IMARA , CCM NDO CHAMA CHA MATUMAINI ENDELEENI KUKIAMINI . Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu Amos Makalla akizungumza maelfu ya Wananchi waliofurika katika eneo la Mundarara wilayani Longido amesema kutokana na utekelezaji bora wa Ilani kumekuwa na ongezeko la Wanachama wengi kujiunga na CCM hata wa Upinzani wanazidi kujiunga CCM hii inadhirisha kuwa CCM ni Chama imara na Chama cha matumaini na ndo kina wajibu wakushughulika na shida za Wananchi. 🗓️ O5 Septemba, 2024. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
2ba549e50a5098e211729ddb68f5ba6f61097679123b5fab66a1beacc8fb76bb
167
5.48503
6
916
1
0
0
0
2.4
21
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/mME
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. NAIBU KATIBU MKUU CCM BARA NDG JOHN MONGELLA APOKEA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM 2020-2024 MKOA WA SHINYANGA Naibu Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, John Mongella, akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga mara baada ya kuwasili mkoani hapo kwa ziara ya chama ya siku saba leo, tarehe 6 Septemba 2024. Mongella ni mlezi wa CCM Mkoa wa Shinyanga. Pamoja na kutia saini kitabu cha wageni, Ndugu Mongella pia amepokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Chama 2020-2024 kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha, ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
99a03a180b4d4a982303c868197b1dd5dbb95897d968e426792bf530dd81e86a
191
5.21466
6
996
1
0
0
0
2.09
20
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/lM7
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. DKT SAMIA AMELETA MAPINDUZI MAKUBWA SEKTA YA ELIMU - CPA MAKALLA Shule za High School zilikuwa chache lakini leo zipo kila Mkoa, Miongoni mwao za Wasichana zikiwa na Michepuo ya Sayansi Katibu wa NEC-Itikadi Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu Amos Makalla leo Septemba 05, 2024 amekagua Ujenzi katika Sekondari ya Samia ya Wasichana Mchepuo wa Sayansi iliyopo Wilayani Longido Mkoani Arusha. CPA. Makalla akiambatana na Viongozi wa Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) amezungumza na Wanafunzi na Walimu kwenye Sekondari hiyo, ambapo amesema Rais na Mwenyekiti wa Chama hicho Dkt Samia Suluhu Hassan amefanikiwa kuleta mapinduzi Makubwa Kwenye Sekta ya Elimu hapa nchini. "Nataka niwaambie kitu kimoja kuwa, tumefika hapa kwa Sababu enzi hizo nasi tulisoma kama Ninyi, kwa hiyo mnapaswa kuongeza Jitihada kwenye masomo ili nanyi muwe Viongozi Bora kwa Siku zinazokuja" "Pongezi nyingi zimuendee Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuleta Mapinduzi makubwa kwenye sekta ya Elimu, kwa Sababu Zamani high school zilikuwa Chache, lakini Rais Dkt Samia amefanya mapinduzi kwenye Elimu, ambapo kwa Sasa Kila Mkoa unayo shule ya Mfano ya Wasichana Mchepuo wa Sayansi, hayo ni maono yake na Sisi kama Chama hatuna budi kupongeza na kuunga mkono Jitihada zake" amesema CPA. Makalla. 🗓️05 Septemba,2024. 📍 Longido Samia girls Secondary school Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
7df66fd85bfcedd4e2f24ca2b0e09927b4989e7a8eaff69e7f96399adad9c7d3
291
5.52921
9
1,609
1
0
0
0
1.72
37
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/kOr
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. NAIBU KATIBU MKUU CCM (BARA) JOHN MONGELLA AANZA ZIARA MKOANI SHINYANGA Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, John Mongella, leo tarehe 05 Septemba 2024 ameanza ziara ya siku saba mkoani Shinyanga. Lengo kuu la ziara hii ni kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020-2024, kuimarisha uhai wa chama, na pia kusikiliza changamoto zinazowakabili wananchi wa mkoa huo. Mongella, ambaye ni mlezi wa chama mkoani Shinyanga, anatarajiwa kufanya mikutano ya ndani na hadhara, pamoja na vikao na watumishi wa chama na jumuiya zake. Katika ziara hiyo, atatembelea maeneo ya Shinyanga Mjini, Shinyanga Vijijini, Kahama, Msalala, Kishapu, na Ushetu, ambapo atakutana na viongozi na wananchi kujadili namna bora ya kuimarisha utekelezaji wa sera za chama kwa maendeleo ya mkoa huo. Kupitia ziara hii, Mongella anatarajiwa pia kuhamasisha wanachama wa CCM kushiriki kikamilifu katika shughuli za chama na kuwa mstari wa mbele katika kutatua kero zinazowakabili wananchi. Ziara hii ni sehemu ya mikakati ya CCM ya kuhakikisha inaendelea kuwa karibu na wananchi na kujibu na kutatua kero zao kwa vitendo. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
0dccb37ffc6ed73477159fb22f37f9ff8984c95bacb98de1eef38076dc770612
256
5.550781
9
1,421
1
0
0
0
1.17
33
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/jOY
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. MWENEZI MAKALLA ATEMBELEA MPAKA WA TANZANIA NA KENYA 'NAMANGA ONE STOP' ARIDHISHWA KWA KAZI NZURI . "Nimeridhika na kazi mnayoifanya hapa 'Namanga One Stop Border Post' nimejionea foleni ya magari sio kubwa, pamoja na kazi nzuri mnayoifanya endeleeni kuhakikisha suala la foleni linaisha kabisa huku mkiondoa urasimu pamoja na yote muongeze Ushirikiano kwani kwa sasa tupo Vizuri Sisi na majirani zetu wa Afrika Mashariki". "Jambo la Mwisho wapeni Ushirikiano hawa wafanyabiashara wa hapa mpakani wasikwame wanapotaka kufanya kazi na kizuri nimeambiwa kiwanda cha Nyama kinafanya kazi". Katibu wa NEC-Itikadi Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu Amos Makalla amesema hayo wakati alipotembelea mpaka wa Namanga leo wakati akiwa kwenye Ziarani Mkoani Arusha. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
5391e53a7becfaa1efd3d200522259e9836e81e1baab0ffddfa27e78016464aa
197
5.746193
7
1,132
1
0
0
0
0.51
23
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/gQZ
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. CCM HAIHUSIKI NA MANENO YALIYOSEMWA ALIYEKUWA MKUU WA LONGIDO - CPA MAKALLA CCM inashinda Chaguzi zake kwa haki na sio Kwa kubebwa bebwa na itaendelea kushinda kwa sababu tumejipanga vizuri kushinda chaguzi zijazo Sisi ni Chama kiongozi tumekubali kutokwenda Ngorongoro wenzetu waige Mfano wetu . "Nimekuja Arusha kwa ajili ya kumalizia maeneo ambavyo wakati tunakuja kwenye ziara ya Katibu Mkuu hatukufika Ngorongoro,Karatu na Monduli ,lakini niliomba nafasi kwenda Ngorongoro kuzungumza na wananchi lakini tulivyoomba kibali tulikatazwa na sababu sie ni Chama kiongozi tumekubali na wenzetu wajifunze kwetu na hii ni Ujumbe kuwa tunaheshimu utawala wa kisheria". "Hata yule jamaa wa Longido aliyoyasema sio maneno ya Chama mie kama Msemaji wa Chama niseme yalikuwa maneno yake na ukimsikiliza alikosa hoja huko vichani sijui alifata nini sisi Chama cha Mapinduzi hatujamtuma na hatuhusiki na maneno sisi tunajipanga kushinda kwa haki na imekuwa kawaida ya kushinda kwa haki hivyo niwaambie Wananchi na Watanzania yalikuwa maneno yake na sio msimamo wa Chama". Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu Amos Makalla amesema hayo wakati akizungumza Katika kikao cha ndani na Viongozi na Wanachama wa Mkoa wa Arusha. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
456b58d36cb5e667236d18ef85c845785cbf95a24929178dfa81ff5876dfe28d
271
5.664207
7
1,535
1
0
0
0
0.74
44
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/0XV
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. KATIBU MWENEZI WA CCM AWASILI MKOANI ARUSHA KUANZA ZIARA YA SIKU SITA Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo CPA Amos Makalla akizungumza na Mwenyekiti CCM Mkoa Arusha Loi Thomas Ole Sabaya(katikati) na Katibu wa CCM Mkoa Arusha Mussa Dadi Matoroka mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro kuanza ziara yake ya siku sita katika Mikoa ya Arusha na Manyara Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
e2d334c7a63ba12783da941eb01d386bd6f8519e04933bf1a565d2c40fc5393f
150
5.413333
3
812
1
0
0
0
0
17
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/9L8
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. ZIARA YA KATIBU MWENEZI WA CCM MKOANI ARUSHA NA MANYARA Ratiba ya Ziara ya Katibu Mwenezi wa CCM Taifa CPA Amos Makalla katika mikoa ya Arusha na Manyara kuanzia Tarehe 4 hadi 9, Septemba 2024. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
1656703b81709ddbcb81bcef7c1f46545a24c83139cd2792564dde9c89d42777
120
5.383333
4
646
1
0
0
0
2.5
13
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/7W8
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. MWENYEKITI WA CCM DKT SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU MAALUM JIJINI DAR ES SALAAM Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kikao cha Kamati Kuu Maalum ya CCM, inayokutana jijini Dar Es Salaam, Jumapili Septemba 01, 2024. Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
7c09586a8e01154d707ad87e81e185e8e648247c30d8230641a22e64ee8cb05e
137
5.489051
5
752
1
0
0
0
1.46
12
https://www.ccm.or.tz/habari/post/soma-zaidi/6YL
Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. MCHAKAMCHAKA WA MWENEZI MAKALLA AANZA NA UZINDUZI WA SHINA LA WAKEREKETWA LA WAVUVI BEACH MJI MWEMA ACHANGIA MILIONI MOJA Katibu wa NEC Itikadi Uenezi na Mafunzo CPA Amos Makalla amefungua shina la Wakereketwa la Wavuvi Beach Mji Mwema Kigamboni. CPA Makalla akifungua shina la Wakereketwa amesema "nawapongeza sana Viongozi wa Chama kwa kunileta hapa kufungua Shina hili la wakereketwa kwani Chama Cha Mapinduzi nguvu yake kubwa ipo kwenye mashina kama ilivyo kwenye jumuiya zake kama vile Vijana ambao ndio wanaleta Hamasa nanyi watu wa Shina Uchaguzi huu ni mtatumika kukiombea kura Chama Cha Mapinduzi kwani tumelifungua wakati muafaka lakini nitawachangia Milioni Moja kwa ajili ya kuendeleza Shina". 🗓️ 27 Agosti, 2024. 📍 Kigamboni Niwapongeze Umoja wa Wanawake Tanzania kwa mambo matatu makubwa; UWT imefanya kazi kubwa ya kutayarisha viongozi, kubadilisha mitazamo ya wanawake wa Tanzania na kusimama kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi. Ni ukweli usiopingika kwamba mchango wa mwanamke una nafasi muhimu katika uchumi, siasa na mustakabali wa Taifa, ukizingatia nafasi ya ulezi na ujenzi wa uchumi.
aca3305a420549624c5079548131aa7d9abd2a7b3fb6ce1176bb062677a32dfc
198
5.616162
6
1,112
1
0
0
0
2.02
20